Thursday, July 28, 2011

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na Waziri Mstaafu, Fredrick Sumaye, nje ya ukumbi wa Nkurumah baada ya kuaga mwili ya marehemu Profesa Samuel Mushi, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Katikati ni Rais Mstaafu wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa.

. Genevieve apaa tena

MWIGIZAJI nyota wa filamu nchini Nigeria  Genevieve Nnaji hivi
karibuni ameteuliwa kuwa Mwanamke anavaa vizuri zaidi ‘Most Elegant
Woman’ baada ya kuwashinda wanawake nyota 30 waliopigiwa kura na
Jarida la mitindo la Encomium Magazine.



Akizungumzia siri ya mafanikio yake hayo, galacha huyo wa filamu
alisema kwamba hata yeye hajui hasa lakini pengine filamu anazoigiza
kwa umakini ndizo zilizompa nafasi hiyo kwani katika filamu hizo
amekuwa akijitahidi za sana kujikita katika mitindo ya uvaaji.

“ Unapokuwa msanii utambue kuwa ni kioo cha jamii, hivyoo unapaswa
kufanya mambo ukijua nyuma yako kuna kundi kubwa linalokutazama,
kukuiga na kujifunza kutioka kwako, kwangu mimi uanamitindo umekuwa
damuni tangu nikiwa mdogo kwa hiyo huwa ninajitahidi kuvaa vizuri
katika filamu zangu,” alisema.

Galacha huyo ambaye  hupendelea kula wali, na kutumia manukato ya Coco
Chanel, alisema kitu anachopenda katika uanamitindo ni ‘ handbag ‘.

Alipoulizwa kuhusu tuzo hiyo ya ‘Most Elegant Woman’ alisema
anajisikia vizuri na kwamba imemchukua muda mrefu kwake kushinda tuzo
kama hiyo. Pia alizungumzia maisha yake ya ndoa na kuweka wazi kwamba
ataolewa atakapopata mwaanamume  anayefaa lakini haina maana kwamba
anatafuta mwanamume.


2. Stella Damasus, Mofe Duncan wavuma tena

WASANII waliovuma katika ‘kashfa’ ya mapenzi Dj Mofe Duncan na Stella
Damasus ambaye ni mwiogizaji wa Nollywood wameibuka  na kuacha maswali
kwa mashabiki hasa wanaopenda kufuatilia mambo ya watu.

Stella Damasus na Mofe Duncan, walijikuta wakianikwa kwenye vyombo vya
habarii kuhusu uhusian wao wa mapenzi baada ya kubambwa wakiwa katika
mazingira ya kutatanisha walikuwa wakisherehekea harusi na mshikaji
wao Dakore-Olumide mwezi januari.

Vyombo vya habari viliandika mara kwa mara kuhusu uhusiano wao wa
mapenzi  ambapo hata hivyo kwa nyakato tofauti, wawili hao walikana na
kusema kwamba uhusiano wao ni wa kibiashara za si zaidi ya hapo na ni
tofauti na watu wanavyowazungumzia.

Hata hivyo Mofe ambaye ni Dj waa Radio  5ive28 Entertainment  pamoja
na Stella wameibuka ten pamoja safari hii wakiwa wameigiza pamoja
katika filamu inayoongozwa na Kampuni ya  SDA Production,  na wote
wanafanya programu itakayorushwa kwenye televisheni muda sio mrefu.


3.Omotola bado aandamwa


MWIGIZAJI galacha wa kike Nigeria Omotola Jalade bado anaandwamwa na
shutuma za kuvaa nusu uchi pamoja na kuwakilisha Afrika kati tuzo za
heshima za filamu duniani zinazojulikana kama Grammy Awards.

Hata hivyo kuna mgawanyiko wa mashabiki na wananchi wengine
wakijiuliza kama kweli msanii huyo anastahili kupewa lawama hizo hata
baada ya kuiletea sifa nchini yake Nigeria na Afrika nzima heshima
kubwa ya kukanyaga zulia jekundu.

“Mimi sidhani kama anastahili lawama zote hizo, inatupasa kuangalia
ushiriki wake katika tuzo hizoo ambao ndio kitu kikubwa zaidi, Tuzo za
Grammy ni kubwa na zenye hadhi, lakini pia hata mavazi aliyovaa yapo
katika mitindo si kwamba alivaa uchi, alisema mmoja wa mashabikki.

"Kama lilikuwa ni suala la kumwekea mikono mwanamume si jambo la
ajabu, na wla haimaanishi kwamba ni mpenzi wake,” alisema shabiki
mwingine.

Omolata alifanikiwa kukanya Zulia Jekundu  ‘Grammy Award 2011 Red
Carpet’ jambo ambalo limepokewa kwa hisia kwa wadau wote wa filamu
nchini humo lakini pia kuiletea heshima kubwa nchi yake.

Galacha huyo aliongozana na meneja wake katika kampuni anayofanyia
kazi ya Bishop Entertainment and Bungalo/Universal Records na ameeleza
kuwa hiyo imempa changamoto kubwa ya kufanya vizuri zaidi katika
tasnia ya uigizaji nchini humo na kimataifa.



1.
Elton John kumsaka baba wa mwanaye

LONDON, Uingereza

MWIMBAJI Elton John amesema yupo mbioni kumsaka mwanamume ambaye ni baba wa kibiolojia wa mtoto wake wa kiume.

Elton mwimbaji wa kibao cha 'Rocket Man' na mumewe David Furnish wamekuwa wazazi wa mtoto mwenye umri wa miezi minne Zachary Jackson kupitia kwa mama wa kuajiliwa (Surrogate mother) siku ya Christmas Day na kwa mara ya kwanza walisisitiza wasingependa kufahamu nani miongoni mwao ni baba wa ukweli.

Ingawa mwanamuziki huyo (64) sasa ameamua kupitia vipimo vya DNA kama Zachary hahitaji kufahamu nani ni damu ya karibu kwa sababu za kitaalamu.

Elton aliliambia gazeti la Daily Mirror: "Zac atatakiwa kufahamika kwa jitihada kubwa za kutafuta vipimo kama hivi. kama atakuwa ni wa David nitafurahi sana. Lakini kwangu sitajali na kinyume chake."

Lakini pia alithibitisha kuwa amemtumia zawadi familia ya mwanamke asiyejulikana aliyesimamia malezi ya mtoto wake.

Mapema baada ya Zachary kuzaliwa, rafiki wa David alisema wachuma hao hawakuwa na sababu ya kumsaka baba wa kibaolojia wa mtoto huyo ambaye angekuwa na kuwafahamu wazazi wake aliofanana naye.


                             
2
Cheryl Cole kuwa jaji shindano la X Factor

LONDON, Uingereza

MWANAMUZIKI Cheryl Cole amethibitishwa kuwa jaji katika shindano maarufu la muziki nchini Marekani la 'The X Factor'.

Simon Cowell amemthibitisha mwimbaji huyo wa kibao cha 'Promise This' kuwa ataungana naye kusimamia shindano hilo pamoja na jaji wa zamani wa shindano la 'American Idol' Paula Abdul katika mpango huo.

Simon alisema: "Pamoja na Cheryl, niliposikia ningekutana naye faragha mara moja na kumpa kazi katika 'The X Factor'. Niliona yeye ni makini, mbunifu na anafahamu anachokizungumza."

"Unaweza kukutana na mtu maalumu mara moja katika maisha, Cheryl ni mtu maalumu, ana uwezo mkubwa katika mawasiliano, ni jaji mwenye uwezo na anajipenda.Nadhani atafanya kitu kizuri Amerika."

"Nilimwonesha tepu yenye mwongozo ambao ungerekodiwa kuhusu Cheryl Uingereza kwa Darnell alisema , 'Ningependa kumsiki pia katika shindano la 'American Idol'.' Kiukweli wana mapenzi makubwa naye."

Dernell (51) alisisitiza mrembo huyo mwenye miaka 27 kuanza kutumiwa katika televisheni kama jaji mapema bila kujali uwepo wa Jennifer Lopez, Cee Lo Green na Mariah Carey ambao wanaaminika kutajwa kuwemo katika mpango huo.




1.
Elton John kumsaka baba wa mwanaye

LONDON, Uingereza

MWIMBAJI Elton John amesema yupo mbioni kumsaka mwanamume ambaye ni baba wa kibiolojia wa mtoto wake wa kiume.

Elton mwimbaji wa kibao cha 'Rocket Man' na mumewe David Furnish wamekuwa wazazi wa mtoto mwenye umri wa miezi minne Zachary Jackson kupitia kwa mama wa kuajiliwa (Surrogate mother) siku ya Christmas Day na kwa mara ya kwanza walisisitiza wasingependa kufahamu nani miongoni mwao ni baba wa ukweli.

Ingawa mwanamuziki huyo (64) sasa ameamua kupitia vipimo vya DNA kama Zachary hahitaji kufahamu nani ni damu ya karibu kwa sababu za kitaalamu.

Elton aliliambia gazeti la Daily Mirror: "Zac atatakiwa kufahamika kwa jitihada kubwa za kutafuta vipimo kama hivi. kama atakuwa ni wa David nitafurahi sana. Lakini kwangu sitajali na kinyume chake."

Lakini pia alithibitisha kuwa amemtumia zawadi familia ya mwanamke asiyejulikana aliyesimamia malezi ya mtoto wake.

Mapema baada ya Zachary kuzaliwa, rafiki wa David alisema wachuma hao hawakuwa na sababu ya kumsaka baba wa kibaolojia wa mtoto huyo ambaye angekuwa na kuwafahamu wazazi wake aliofanana naye.


                             
2
Cheryl Cole kuwa jaji shindano la X Factor

LONDON, Uingereza

MWANAMUZIKI Cheryl Cole amethibitishwa kuwa jaji katika shindano maarufu la muziki nchini Marekani la 'The X Factor'.

Simon Cowell amemthibitisha mwimbaji huyo wa kibao cha 'Promise This' kuwa ataungana naye kusimamia shindano hilo pamoja na jaji wa zamani wa shindano la 'American Idol' Paula Abdul katika mpango huo.

Simon alisema: "Pamoja na Cheryl, niliposikia ningekutana naye faragha mara moja na kumpa kazi katika 'The X Factor'. Niliona yeye ni makini, mbunifu na anafahamu anachokizungumza."

"Unaweza kukutana na mtu maalumu mara moja katika maisha, Cheryl ni mtu maalumu, ana uwezo mkubwa katika mawasiliano, ni jaji mwenye uwezo na anajipenda.Nadhani atafanya kitu kizuri Amerika."

"Nilimwonesha tepu yenye mwongozo ambao ungerekodiwa kuhusu Cheryl Uingereza kwa Darnell alisema , 'Ningependa kumsiki pia katika shindano la 'American Idol'.' Kiukweli wana mapenzi makubwa naye."

Dernell (51) alisisitiza mrembo huyo mwenye miaka 27 kuanza kutumiwa katika televisheni kama jaji mapema bila kujali uwepo wa Jennifer Lopez, Cee Lo Green na Mariah Carey ambao wanaaminika kutajwa kuwemo katika mpango huo.


                      
3
Binti wa Smith amfurahisha Rais Obama

NEWYORK, Marekani

RAIS  Barack Obama amempigia kinanda mwimbaji chipukizi wa Pop nchini humo Willow Smith ambaye alig'ara vilivyo katika onesho maalumu lililofanyika Ikulu ya White House.


Willom mwenye umri wa miaka (10) alifanya onesho hilo katika Ikulu ya White House katika sikukuu ya Pasaka ambako mwimbaji huyo wa 'Whip My Hair' ameripotiwa kumfurahisha vilivyo binti wa Obama, Sasha.



Willow aliimba kibao chake kipya cha 'Rockstar' na kingine cha  '21st Century Girl' na mwengine uliomg'arisha uitwao 'Whip My Hair'.


Mwimbaji huyo pia alimwimbia Obama kibao cha 'Only Girl (In the World)', ulioimbwa na wanamuziki Rihanna na Lady Gaga 'Just Dance'.


Mtoto wa Obama mwenye umri wa miaka 9 alionekana mwenye zaidi ya furaha pale wazazi wake walipomsomea Willow kitabu cha Chicka Chicka Boom Boom katika tukio hilo lililoanza saa moja asubuhi kwa siku nzima.


Mama wa Willow Jada Pinkett Smith na mke wa Obama, Michelle Obama kwa pamoja walifurahia kwa kugonganisha glasi mbele ya umati mkubwa wa watu kabla ya kumaliza sherehe kwa kula keki maalumu iliyotengenezwa mfano wa yai.


                            
4
Russell Brand kuwalea wanaye Uingereza


NEW YORK, Marekani

MWIGIZAJI Russell Brand amesema hataki watoto wake walelewe kimaadili ya bara la Amerika.

Russel raia wa Uingereza kwa sasa anaishi katika Jiji la Los Angeles pamoja na mke wake nyota wa pop Katy Perry na kuyafurahia maisha lakini anataka kuwalea watoto wake katika maadili ya nchi alikotokea.

Alipoulizwa kama angerudia na kuishi kwa Uingereza alisema: "Kwa siri nataka kufanya jambo hili.Nina wasi wasi kuwasiki watoto wangu wakinijibu wakizungumza kimaadili ya Amerika."

Hata hivyo nyota huto amesema anahitaji kufanya kazi kwa bidii ili kuuza mawazo yake katika Jiji la  California ambako Katy ana soko kubwa.

Aliliambia jarida la Seven: "Nina uhakika naweza kumfanya auze nakala ndogo tukiwa Uingereza. Watu wanataka kuwa juu siku zote, si ndio?.," alihoji Russell.

Russell na Katy walifunga pingu za maisha Oktoba mwakajana baada ya miaka mingio ya uchumba wao kupita lakini nyota huyo amesema ataendelea kumfanyia mambo asiyoyatarajia mkewe hata kama ataonyesha kubadilika ingawa akili yake ni kuona uhusiano wa uhakika



5
'Wasanii jifunzeni Kiingereza'
Na Shaban Mbegu

BAADA ya kushiriki katika filamu ya 'Devils Kingdom' msanii kutoka nchini Nigeria, Ramsey Noah amewataka wasanii nchini kuhakikisha wanajifunza na kujua kuzungumza lugha ya kiingereza kwa ufasaha.

Akizungumza na Maisha jijini Dar es Salaam Noah alisema  wasanii nchini wawezekufikia katika hadhi ya kimataifa ni lazima wajifunze lugha hiyo ambayo ndio inatumika kwa asilimia kubwa katika utengenezaji wa filamu.

Alisema katika medani hiyo ya filamu kila kitu huwa kinaelekezwa na kuzungumzwa kwa lugha hiyo,na ndio inayotambulika kimataifa zaidi.

"Japokuwa kila nchi ni lazima inakuwa na lugha yake, lakini kama msanii una malengo ya kuwa wa kimataifa ni lazima ujue kuzungumza na kuandika kiingereza kwa ufasaha kwa kuwa ndio lugha inayotumika zaidi katika filamu duniani", alisema.

Akizungumzia filamu hiyo alisema pamoja na kukumbana na changamoto ya kutofautiana lugha na washiriki wenzake, ametumia usanii wake kuhakikisha anatimiza wajibu wake kama mhusika mkuu katika filamu hiyo inayohusu mambo ya kishirikina.

Mbali na wasanii hao, ndani ya filamu hiyo pia kutakuwa na wasanii wengine akiwemo Patchou Mwamba, Kajala Masanja, Kimlola Kimlola, Stanley Msungu, Bakari Makuka na wengine



6
Sabrina kuja na 'Justis'
Na Laurent Samatta

NYOTA wa filamu nchini Sabrina Omari Kameya 'Salome', amesema anatarajia kutoa kazi yake mpya inayoitwa  'Justis', filamu ambayo itakuwa ya maajabu ya kila aina lakini haina mazingira ya uchawi.

Akizungumza na Maisha hivi karibuni nyota huyo alisema filamu haina mapenzi lakini kikubwa kinachoelezewa humo ni hukumu ambayo itakuwa inatolewa na muhusika mkuu ambaye atakuwa anauwezo wa kujibadilisha jinsia.


Alisema yeye ni mwanamke lakini atakuwa anacheza kama mwanaume wakati mwingine atabadilika na kuwa babu au bibi, kutokana na hukumu itakayokuwa inatolewa kwa watu waovu.

'Watanzania wamezoea kila msanii anataka na filamu ya mapenzi lakini kwa upande wangu nataka kuleta changamoto na ndiyo maana kazi hiyo itakuwa na maajabu lakini siyo ya kutisha au uchawi," alisema.



7
Songombingo kutoka June
Na Andrew Ignas.

KUNDI la muziki wa dansi la Talent Bendi imetarajia kuingia kambini Mei 24 mwaka huu kwa ajili ya kurekodi Video yao ya 'SONGO MBINGO'ambayo inatarjia kutoka mwanzoni mwa mwezi June mwaka huu.

Akizungumza na Maisha hivi karibuni Mkurugenzi wa bendi hiyo Husein Jumbe alisema kuwa kundi lake litaingia kambini  Mei maeneo ya Mbagala ili kukamilisha kurekodi Video yao hiyo.

"Lengo letu kwa sasa ni kuhakikisha tunamalizia kurekodi video zetu zote zilizobakia katika albamu hii ya Subiri Kidogo na tunatarajia kuingia kambini ili kutoa video ya 'SONGO MBINGO'"alisema Jumbe.


Alisema kuwa pia baada ya kukamilisha kurekodi video zao ambazo zitakuwa zimebakia katika albamu yao wataanza kuandaa nyimbo mpya ya albamu ya pili katika kundi la Talent bendi.


Hata hivyo Msanii huyo amewataka wasanii wachanga ambao wapo mitaani lakini wenye vipaji vya muziki kujiunga na bendi yake ambayo imeundwa na vipaji vingi vya wasanii wachanga.

8
Kshabab kuja na 'Karazinga'

Na Agnes Mwaijega

MSANII chipukizi wa kizazi kipya nchini aliyetamba na kibao cha komando ,Adam Kigoda 'Kshabab' amesema anatarajia kutoa single mpya pamoja na video yake mwezi huu.


Akizungumza na Maisha alisema wapenzi wa muziki wategemee kuona mabadiliko makubwa katika kazi hiyo aliyoirekodi.


Alisema 'single' hiyo iitwayo 'Karazinga' iko katika mtindo wa zouk,rumba na kiarabu na itamfanya atambulike zaidi kuliko ile ya awali.

"'Single' niliyoirekodi mara ya kwanza haikunitambulisha,nina imani kuwa hii  ya sasa itanitangaza kwa sababu nimeifanya kwa umakini mkubwa," alisema

Alisema amepata prodyuza mpya ambaye pia ni meneja wake anayesimamia kazi zake kwa umakini mkubwa.


9
PASHA kuja na warembo
Na Andrew Ignas.

MWANAMUZIKI wa muziki wa kizazi kipya nchini ambaye alitamba na kibao cha Hidaya Hija Mtepa'PASHA'ameanza maandalizi ya video ya nyimbo yake ya Warembo ambayo inatarajia kutoka mwezi Mei mwaka huu.

Akizungumza na maisha jana muimbaji huyo alisema kuwa kwa sasa yupo mbioni kurekodi video yake mpya ambayo inafanya kupitia Visual Lab.


"Nimeshaanza maandalizi ya Video yangu ya Nyimbo ya Warembo ambayo itakuwepo katika Albamu ya Hidaya ambayo natarajia kuitambulisha hivi karibuni"alisema Pasha..


Alisema kuwa katika albamu yake hiyo ya Hidaya itakuwa na nyimbo 10 na tayari mpka sasa amesharekodi nyimbo chache ambazo ni Hidaya,Warembo,na nyinginnezo.


Hata hivyo muimbaji huyo amewahasa wanamuziki ambao wanatabia za kuiba myimbo au mashairi ya wasanii chipukizi.

10

Daimond mbioni kuachia albamu ya pili

Na Laurent Samatta

MUIMBAJI wa muziki wa kizazi kipya nchini, Naseeb Abdul 'Daimond', baada ya albamu yake ya kwanza kufanya vizuri hivi sasa yupo katika maandalizi ya kutoa albamu ya pili ambayo bado hajaipa jina.

Akizungumza na Maisha jijini Dar es Salaam, nyota huyo wa kibao cha 'Mbagala' alisema albamu hiyo inatarajia kuwa na nyimbo nane ambazo ni Moyo wangu, Mboni zangu, Chanda chema, Lala salama na nyingine.

Alisema albamu hiyo anaamini itafanya vizuri lakini kikubwa alichokipaga kabla hajatuoa albamu hiyo anataka kufanya ziara mikoa yote ya Tanaznia Bara na nje ya nchi kwa lengo ya kuitagaza kupitia buradani atakazokuwa anazitoa ili iweze kuuza vizuri.

"Albamu bado sijaipa jina kwa sababu kila wimbo nilionao ni mzuri hivyo naamini baada ya maandalizi yote kukamilika nitaweza kujua ni upi uweze kubeba albamu yangu," alisema.

Alisema hata hivyo katika suala la kukuza muziki hapa nchini kwa upande mwingine wananchi wanachangia kushusha thamani ya msanii husika kwa sababu hawana tabia ya kununua kanda halisi badala yake wananunua iliyotolewa kopi kitu ambacho hakieleti maandeleo.

WANAFUNZI WAANDAMANA KUPINGA PILISI GARI LAO KUGONGA MMOJA WAO

 Polisi wakiwatuliza wanafunzi walio andamana
 Polisi wakiangaika kuwapakia wanafunzi waliofika katika kituo hicho kwa maandamano
 Wanafunzi wakiandamana kuelekea staki shairi
 Polisi wakizungumza na wanafunzi waliofika katika kituo cha polisi
 Askari wakiwakamata wanafunzi kwa kosa la kushinikiza maandamano na kuwapeleka kituoni
 Wanafunzi wakipakia wanafunzi wakapiwa kwenye Defender

DC Ilala ashtushwa na maandamano ya wanafunzi

Mkuu wa wilaya ya Ilala leonidasi Gama akizungumza na wazazi ambao walifika katika maandamano ya wanafunzi waliogoma katika shule za Air wing na Minazi mirefu

Friday, July 22, 2011

RAIS WA WASAFI DIOMND PLATINUM AKIWA KATIKA POZI

MAUNDA CHIPUKIZI WAJIFUNZE MUZIIKI WA LIVE

DADA wa gwiji wa muziki ya miondo ya zouk nchini ambaye ni mkurugezni wa bendi ya B -Band Banana Zoro 'Maunda Zoro' amewataka wasanii wachanga kuhakikisha wanaweka mazoea ya kujifunza muziki wa kisasa ambao ni wa live Band badala ya kubweteka na wa studioni tu.

Akizungumza na Maisha Mwanamuziki huyo amesema wasanii wachanga wanatakiwa kujifunza aina ya muziki wa kutumia vyombo badala ya ule waliokuwa wamezoea ambao ni wa kurekodi studioni.

"Siwakatazi kurekodi studioni ila ni vema pia kujifunza kuimba kwa mtindo huu wa kisasa ambao ni wakuimba kwa Band kwakuwa unawakuza na kuwafanya kufahamika zaidi "alisema Maunda.

Hata hivyo amewasifu wasanii wanaotokea'cakatika jumba la kukuza vipaji vya muziki nchini maarufu kama 'THT kutokana na ubora wa kazi zao wanazifanayanya.

Aidha kwa upande mwingine amevitaka vyomba vya habari ambavyo vinachochea kupungua kwa maadli ya jamii kuachana na tabdia hizo na badala yake wapiganie mambo yatakayo saidia maendeleo.

mwisho.

CHAZ BABA AKAIWA KATIKA POZI

Wednesday, July 20, 2011

WIKI YA MALIASILI KATIKA KUADHIMISHA MIAKA 50

Ukuzaji utalii wa ndani ulenge kutoa elimu ngazi ya Mitaa.

Na Humphrey Shao

IKIWA wizara ya maliasili ipo katika wiki ya kuadhimisha wiki ya miaka 50 ya uhuru wa Tanganyika kwa kufanya maonyesho Viwanja vya Mnazimmoja Dar es salaam lakini bado hali ni tete katika kuhamasisha utalii wandani.

Nathubutu kusema hivi kuwa wizara hii imeshindwa kuwa na mipango mathubuti ambayo ingewezesha kusaidia kuhamasisha utalii wa ndani kwa kupitia serikali za mitaa.

Ninasema hivi kwa makusudi kuwa ni lazima wizara hii itambue kuwa serikali za mitaa ndio inayo miliki watu kuanzia ngazi ya chini na ndio inayo wafikia watu kwa urahisi kuliko chombo chochote hivyo kinastaili kipewe nafasi katika kufanikisha malengo la utalii.

Ukiangalia hivi sasa mbinu zinazo tumika kuamasisha utalii wa ndani ni zile zinafanyika kwa wageni katika nchi zilizo endelea wakati aziendani na mfumo wetu wa nchi hii.

Katika taifa letu wenye viti wa mitaa wameshindwa kutumiwa ipasavyo kufikisha ujumbe kwa watu ingali wao wanamadaraka makubwa na nguvu katika jamii inayo tuzunguka.

Sisiti kusema mbinu zinazo tumika katika kuahamasisha utalii wa ndani ni za kisiasa zaidi na kulipana posho kuliko jambo lenyewe na uzito wake.

kwani ukisoma idadi ya nambari ya watalii wa ndani wengi wao ni wale wanafunzi wa shule ya msingi na wachache sekondari ambao wamekuwa wakiburutwa na walimu wao awaelewi chochote na mapato yao ayawezi kutufikisha popote katika taifa hili ambalo linaitaji kutegemea utalii kama sehemu ya uchumi wake.

Hivyo basi endapo tutatumia serikali za mitaa kuhamasisha utalii wa ndani tutaweza kuwafikia wananchi wengi kwa urahi mijini na vijijini hali itakayo saidia kuongeza pato la nchi amabalo limekuwa liki lalamikiwa kushuka kila siku.

Ukizunguka hapa nchini sehemu kubwa ya utalii ipo katika mitaa amabyo inaishi watu lakini watu wa eno hilo awaelewi umuhimu wa sehemu hizo na faida zake katika urithi wa taifa .

kwa mfano mwanafunzi anaweza kumaliza miaka mitatu katika chuo cha usimamizi wa fedha(IFM) bila kuingia makumbusho ya Taifa jinsi gani inavyoo onyesha wizara hiyo kushindwa hata kuwaunganisha wanafuzni wa elimu ya juu kuhusiana na utalii wa ndani.

Hii inadhiirisha uzemebe uliopo kwa watendaji ambao wanapanga mipango yakutoa elimu juu ya utalii wa ndani kwa kuiga mipango ya nchi zilizo endelea.

Ukijaribu kutembelea Maeneo ya Mtae Wilaya ya Lushoto kuna utalii mkubwa unafanyika katika magofu yaliyoachwa na wajerumani lakini wakazi wa eneo hilo awatambui nini kinaendelea katika eneo la na kufurahia wakiona wazungu wakipita barabarani.

Hii inatishia hatari ya kizazi kinacho zaliwa kuafanya uharibifu maeneo hayo kwa kutofahamu umuhimu wake na thamani yake katika historia ya nchi hii kutokana na wizara kushindwa kujipanga kutoa eleimu ya kutosha.

Kufanya maonyesho mijini na aitoshi kusema kuwa mtafanikiwa katika utalii wa ndani bali nguvu ya ziada inahitajika kwa kushirikiana na viongozi wa mitaa kama ilivyo kwa sekta zingine.

Mfano mdogo ni tume ya uchaguzi ambayo wakati wa uchaguzi ukasimu madaraka kwa viongozi hao wa mtaa hali inayoonyesha kupata mafanikio makubwa katika swala hilo ambalo ingekuwa gumu kwa wao kupeleka watumishi kila mtaa.

Hapa pia ikumbukwe ni vema kuzingatia kuwa watu bado awaelewi umuhimu wa utalii kutokana na hali ngumu ya maisha na kutoa mabiwa faida za utalii katika kujikwa mua hali hiyo ngumu.

Endapo watu watapata nafasi na fursa kupitia viongozi wao wa mitaa na kuelezwa umuhimu wa utalii kasi ya watalii wa ndani itakuwa kwa kasi kubwa sana.

Swala hili linajidhiirisha katika maonyesho ya kimataifa ya kibiashara ya Sabasaba mabapo watu wengi uwa na kiu ya kufahamu aina za wanyama na kuwatazama kama kitu kigeni ndani ya nchi yao .

Lakini hiyo ni kwa wanyama vipi kuhusu utalii ambao auhamishiki kama Olduvai Gorge watu wataelewa nini kuhusu hilo hivyo ni wakatai muafaka wizara kubadilisha mfumo wa utalii wa ndani.

Kama hilo nalo gumu hata hili la kutumia sinema na video kila mtaa kama ilivyokuwa tukionyeshwa sinema za yesu katika viwanja vya wazi hapo zamani? nadahani hii ndio njia pekee ambayo inatakiwa kuafuatwa na badala ya blaa bla za ofisini na miradi ambayo inashindwa kufikia malengo.

Waziri wangu maige lazima uwe macho na watendaji wako sio kila dokezo linafaa katika kufanikisha utalii wa ndani madokezo mengine ni ya kisanii na yanataka kufuja fedha za serikali.

Hivyo basi ni lazima kutumia jicho la tatu katika mpango huu ambao utaongeza pato la taifa letu na kuachana na tabia ya kuomba omba fedha kutoka kwa waisani.

mwishoooooooo

logo mpya kwa wadau wa jirushe inataraji kuja hivi punde

Monday, July 11, 2011

Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Rwekaza Mukanda (kulia) akimvisha kofia na Joho, Prof. Pius Yanda, baada ya kutangazwa kuwa Mwenyekiti wa kwanza wa Kigoda cha Kumbukumbu ya Mwalimu yerere, wakati wa hafla ya uzinduzi wa kigoda hicho kilichozinduliwa kwenye Ukumbi wa Nkurumah Chuo Kikuu cha Dar es Salaam leo . Kushoto ni Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Taalum, Prof. Makenya Maboko.

kesi kinyerezi kusikilizwa juni 21

Na Humphrey Shao

MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es salaam imeahirisha kesi ya ugawaji wa viwanja katika eneo la kinyerezi iliyofunguliwa na wananchi dhidi ya Manispaa ya Ilala hadi Julai 11 mwaka huu.

Ilidaiwa na karani  wake Bw. Obed Abdalla kuwa kesi hiyo iliahirishwa jana mahakamni hapo kutokana na jaji anayesikiliza kesi hiyo Agostine Shangwa kupata udhuru.

Kesi hiyo ilifikishwa mahakani hapo June 28 na wananchi wa eneo la kinyerezi wakidai manispaa ya Ilala kuendesha mradi wa kuuza viwanja vyao kinyume na taratibu.

Wananchi hao wanawakilishwa na wakili wa kujitegemea Bw. Mathias Kisegu.

Katika uamuzi wa awali baada ya kusikiliza malalamiko hayo jaji Agustino Shangwa aliagiza manispaa hiyo kusitisha ugawaji wa viwanja hivyo hadi pande zote mbili zitakaposikilizwa na kutolewa uamuzi.

Katika utetezi wa awali Mwenyekiti wa Kamati ya wananchi wa kinyereziDkt Silas Kishaluli alieleza mahakama hiyo kuwa walifikia  hatua ya kufungua kesi baada ya  mazungumzo na Mkurugenzi wa Manispaa hiyo Bw. Gabraeli Fuime kupata muafaka juu ya hilo kushindikana.

Alisema hali hiyo ndiyo iliyowasukuma  kufungua kesi ili mahakama itoe tafsiri sahihi ya kisheria kuhusu hatua zinazokusudiwa kuchukuliwa na Manispaa hiyo bila kuzingatia maslahi yao.

Manispaa ya Ilala ilitangaza kupima viwanja katika eneo la kinyerezi kama sehemu ya utekelezaji mradi wa viwanja 20000 vilivyo tangazwa na serikali kwa lengo la kupunguza uhaba wa viwanja vya makazi katika jiji la Dar es Salaam.

TWENDE KAZI HAROOOO

Polisi akimuhamulu mtuhumiwa wa wizi wa shilingi, 160000,  kukaa chini uku mwenzie akipata kipondo katika hospital ya Mnazi Mmoja Dar es Salaam jana.

judo KUNA PENGO LA MILIONI 12

Na MWANDISHI WETU

ZIKIWA zimebaki siku tano kufanyika kwa mashindano ya kanda tano Afrika Mashariki ya mchezo wa judo chama cha mchezo wa judo nchini (JATA), kimesema kinahitaji kiasi cha sh.milioni 12 ili kuweza kukamilisha maandalizi ya mashindano hayo.

Mashindano yanatarajia kufanyika Julai 17 hadi 18 katika ukumbi wa Land Mark uliopo Ubungo Dar es Salaam ambapo jumla ya nchi sita zitashiriki ambazo ni Burundi, Kenya, Uganda, Zanzibar ambayo itashiriki kama nchi pekee, Zambia na Tanzania ambao ndio wenyeji.

Akizungumza Dar es Salaam jana, Katibu mkuu wa JATA Kashinde Shabani alisema, fedha hizo ni kwa ajili ya mahitaji muhimu ya kimashindano ikiwa ni pamoja kuhudumia timu hizo zitakazoshiriki.

"Tukiwa kama wenyeji tunajukumu la kuhakikisha mashindano haya yanafanyika kikamilifu ikiwa ni kwa ajili ya kulinda hadhi ya nchi na heshima ya kupewa hadhi ya kuwa wenyeji hivyo tunaomba Serikali na wadau mbalimbali kuchangia kupatikana kwa fedha hizo ili kufanikisha mashindano hayo," alisema Shabani.

Katibu huyo alisema, maandalizi mengine kwa ajili ya timu ikiwa ni pamoja na vifaa vya michezo yameisha kamalika kwani kwa upande wa vifaa wamealazimika kukusanya vifaa vilivyopo katika klabu mbalimbali za mchezo huo nchini kwa ajili ya kufanyia mashindano hayo baada ya vile vilivyopo bandari kutokujilikana hatma hadi sasa licha ya juhudi mbalimbali za Serikali kufanyika.

Mwisho

JESHI LAPOLISI LA WATIA HATIANI WATUHUMIWA 32


Na Humphrey Shao

JESHI la Polisi Kanda maalum ya Dar es salaamlimefanikiwa kuwakamata watuhumiwa 32 kwa mokosa yakiwemo kwa kupatikana na silaha pamoja na watuhumiwa wa uhalifu wa kuiba na kuvunja nyumba.

Akizungumza na wandishi wa Habari jiji Dar es salaam jana Kamanda wa upelelezi wa kanda ACP Ahamedi Msangi alisema kuwa watuhumiw hao walikamatwa katika operesheni endelevu inayofanywa na kandamaalum ikiwa ni juhudi za kupambana na uhalifu na kuweka jiji katika hali ya usalama.

Alisema kuwa Mnamo tarehe02 julai 2011 majira ya saamoja na dakika kumi na tisa usiku huko maeneo ya Mbezi kwa yusuph wialaya ya kinondoni askari wa jeshi la Polisi wakiwa doria walifanikiwa kupata silaha aina ya Mark iv yenye namaba za usajili steven model58-d12GAS ikiwa imekatwa mtutu wake pia tulifanikiw akukamata silaha nyingine aina ya Short gunyenye namaba za usajili S.NO.MV-18733H maeneo ya pugu sekondari siku ya 5 julai 2011 amabayo ilitaka kutumika kupora bodaboda .
a
"pia tumefanikiw akukamata watuhumiwa wa ujambazi 6 kwa kutumia pikipiki pamoja na pikipiki 5 kutoka maeneo ya Temeke ,Ilala na Kinondoni na kuwaweka chini ya ulinzi kwa ajili ya uchunguzi zaidi "anaeleza Kamanda Msangi .

Alisema kuwa watuhumiwa hao ni Tito Mkasiogwa(30),John Ndogo(18),Ally Jumamosi(18) wengine ni Ibrahim Shabani (20),Mwalimu Omari(36) na Rashidi Kassim.

Katika tukio lingine kikosi cha kupambana na uwizi wa magari kanda ya Dar es salaam wamefanikiwa kukamata magari 10 ambayo yaliibiwa jijini na kupatikana katika miji ya Kahama na Shinyanga, ambapo magari hayo yalikuwa yameuzwa kwa watu binafsi.

Alitaja kuwa magari hayo ni Toyota Nadia yenye namba za usajili T889BJJ,Toyota RAV4 T488AYY,Premio Corona T.682AEB,Spacio T796 BLZ,Corola T170 ABD,Cresta GX100 T916AEE,

Hata hivyo jeshi lapolisi kupitia Kaimu kamanda wa kaanda maalumu Abdul Issa limewatahadharisha wakazi wa jiji na makampuni ambayo yanasafirisha pesa kiholela bila kusindikiwa na polisi kuwa inahatarisha uaslama wa fedha hizo .

Kamanda huyo amaeleza kuwa kutokana na tukio la kuibiwa fedha marakwa mara ni vem,a watu wakawa wa siri ama kufika jeshi la polisi hili kuweza kupata msaada wa kusindikizwa na huduma hiyo inatolewa bure na jeshi hili kuloko watu kurisk pesa hizo.

KARUNDE BAND WAKIFANYA VITU VYAO KATIKA MOJA YA MAONYESHO YAO YALIYO FANYIKA WEEKEND HII

 MWAPWANI YAHAYA MUIMBAJI WA KALUNDE
DEO MWANAMBILIMBI AKIWANAWAIMBAJI WENGINE WA KALUNDE KATIKA MOJA YA MAONYESHO YAO

RMDAU RABIA BAKARI AKIJIRUSHA WEEKEND HII KATIKA MESS YA JESHI

Sunday, July 10, 2011

BUNGE LA KUNWA NA VITAMBULISHO VYA TAIFA

Na Mwandishi Wetu

   
BUNGE la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limeridhishwa na uwezo wa kiteknolojia alionao mkandarasi aliyeshinda zabuni ya kutengeneza Vitambulisho vya Taifa.


RAi hiyo ilitolewa na timu ya wabunge waliotembelea Kampuni ya Iris Corporation Berhad ya Malaysia iliyoshinda zabuni ya kutengeneza Vitambulisho vya Taifa, jana walipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), jijini Dar es Salaam.


Akizungumzia ziara hiyo, Mkuu wa Msafara huo, Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Anna Abdallah alisema Serikali imechelewa kutoa Vitambulisho vya Taifa hivyo haina budi kuharakisha mchakato huo kwa sababu vina faida nyingi kwa ustawi wa maendeleo ya kiuchumi na kijamii Tanzania.

“Sisi wabunge tunasema Vitambulisho vya Taifa ni lazima vitolewe haraka kwa sababu ni muhimu kutambuana, huwezi kumtofautisha mtanzania na watu wa mataifa mengine kwa rangi au sura tu, Lazima tuwe na Vitambulisho vya Taifa,
“wenzetu Malaysia wanatoa vitambulisho hata kwa watoto wadogo kwa nini sisi tushindwe,” alisema.


Akizungumzia kuhusu Kampuni ya Iris alisema, “Ni kampuni namba moja duniani kutengeneza vitambulisho vya kisasa. Hata mataifa ya Ulaya yanakwenda kujifunza kwa kampuni hiyo. Tutegemee kitu kizuri,” alisema.

 
Mbunge wa Mlalo (CCM), Brigedia Jenerali mstaafu, Hassan Ngwilizi alisema Kampuni ya Iris ina uwezo mkubwa na italisaidia Taifa kutengeneza Mfumo wa Utambuzi na Usajili wa Watu na hatimaye kutoa Vitambulisho vya Taifa vyenye ubora wa hali ya juu.

Alisema teknolojia itakayotumiwa kutengeneza Vitambulisho vya Taifa na Iris ambayo pia imetumiwa nchini Malaysia ni ya kisasa ambayo inaweza kuhifadhi taarifa nyingi katika kitambulisho kimoja.
“Wenzetu wamepiga hatua, wameweza kuweka hata hati ya kusafiria (Passport) katika Kitambulisho chao cha Taifa,” alisisitiza.
 
Akizungumzia kuhusu mradi wa Vitambulisho vya Taifa, Mbunge wa Maswa (CHADEMA), John Shibuda alisema Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) inapaswa kuungwa mkono na kupewa kipaumbele ili ipate fedha na kuanza utekelezaji wa mradi huo.

“Vitambulisho ni mbegu ambayo itazaa matunda mengi, tuiwezeshe NIDA ili tuvune matunda yake haraka. Ni mradi utakaoleta neema kwa sababu ukianza kutekelezwa ndani ya mwaka mmoja tunaweza kupata zaidi ya trilioni mbili.

“Nchi kama Kenya haitegemei wafadhili, wanakusanya kodi inavyopaswa kwa sababu wana Vitambulisho vya Taifa,” alisema.

Wabunge waliozulu Iris Corporation Berhad ni Anna Abdallah ambaye alikuwa kiongozi wa msafara, Brigedia Jenerali mstaafu Ngwilizi, Hamad Rashid Mohamed (CUF), Betty Machangu (CCM), Moses Machali (NCCR-Mageuzi), Jasson Rweikiza (CCM), Rebecca Mngodo (CHADEMA) na Anastazia Wambura (CCM).

Wengine ni Rachael Mashishanga (CHADEMA), Mohamed Sanya, Mussa Hassan Mussa na John Shibuda.

Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa ilisaini rasmi mkataba na Mkandarasi, Iris Corporation Berhad ya Malaysia Aprili 21, 2011. Mkataba huu ulitiwa saini na Katibu Mkuu Wizara ya Fedha kwa niaba ya Serikali.

Mchakato wa kumpata mkandarasi wa Vitambulisho vya Taifa ulivyokuwa
Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mei mwaka 2008, ilitangaza zabuni ya kujenga Mfumo wa Taifa wa Utambuzi na Usajili wa Watu.

Baada ya zabuni hiyo kutangazwa kwenye vyombo vya habari, Kampuni mia moja na nne (104) zilijitokeza kununua vitabu vya zabuni

Kati ya Kampuni hizo (104), Kampuni 54 zilirudisha zabuni hizo.

Kamati ya tathmini ya zabuni hii ambayo ilihusisha wataalamu mbalimbali kutoka taasisi mbalimbali za Serikali vikiwemo vyombo vya Ulinzi na Usalama ilikaa na kufanya mchujo wa awali ambapo Kampuni nane (8) zilipita katika mchujo huu, mbili kati ya hizo kwa masharti maalum.

Bodi ya Manunuzi ya Wizara ilipitisha Kampuni sita (6) baada ya zile mbili zilizopewa masharti kushindwa kutimiza masharti hayo.

Kampuni zilizopitishwa ni Unisys – Afrika Kusini, Giesecke & Devrient FZE- UAE, Iris Corporation Berhad – Malaysia, Marubeni Corporation in Joint Venture with Zetes and NEC – Japan, Tata Consultancy Services in Joint Venture with On Track Innovation LTD – India na Madras Security Printers – India

Baadaye Mamlaka ya Usimamizi wa Zabuni za Umma (PPRA) iliamua kufanya uchunguzi wa mchakato wa zabuni hii baada ya kuwapo malalamiko mballimbali toka kwa wananchi kupitia vyombo vya habari.

Katika matokeo ya uchunguzi wake, PPRA ilielekeza Kampuni ya Madras Security Printers iondolewe kwenye mchakato kwa kuwa mbia wake Kampuni ya Bharat Electronics ilikuwa imeingia ubia (Joint Venture) na Kampuni nyingine katika mchakato huu kinyume na masharti yaliyowekwa katika kitabu cha zabuni.

Kampuni tano zilizobaki zilipelekewa “RFP” kwa ajili ya awamu ya pili ya mchujo.

Kampuni tatu kati ya tano zilizobaki zilijitoa katika mchakato kwa hiari na zikabaki Kampuni mbili ambazo ni Iris corporation Berhad na On Track Innovation LTD ambazo zilishindanishwa katika vipengele vya Ufundi/Utaalamu (Technical Evaluation) na Fedha (Financial Evaluation).
Kampuni ya On Track Innovation baada ya kufanyiwa tathmini ilionekana haikuweza kukidhi vigezo vya kiufundi na kiutaalamu vilivyowekwa hivyo basi iliondolewa katika mchakato na kubakiza kampuni moja ya Iris Corporation Berhad.

Baada ya kufanyiwa tathmini ya bei, Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa iliunda timu ya kwenda kuifanyia uchunguzi (Post Qualification) Kampuni ya Iris ili kuweza kujiridhisha juu ya uwezo wake wa kutekeleza mradi huu kwa mujibu wa kanuni ya 94 ya GN 97 ya Kanuni za Manunuzi ya Umma, 2005, na Machi 14-16, 2011 timu hiyo ilikwenda Malaysia kufanya uchunguzi.

Timu hii iliundwa na wataalamu kutoka vyombo mbalimballi vya Serikali vikiwamo vyombo vya Ulinzi na Usalama pamoja na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Aidha Mamlaka iliunda kamati ya majadiliano kwa mujibu wa Sheria ya Manunuzi ya Umma. Kamati hii pia iliundwa na wataalamu kutoka taasisi mbalimbali za Serikali ikiwemo Wizara ya Fedha pamoja na Ofisi ya Mwnasheria Mkuu wa Serikali.

Majadiliano na Mzabuni huyu yalifanyika kwa muda wa wiki mbili ambapo taarifa ya Kamati hii ilipitiwa na kuridhiwa na Bodi ya Manunuzi ya Mamlaka.
Baada ya Bodi kuridhia taarifa hiyo, Mzabuni huyu alipewa barua ya “award” na kisha rasimu ya Mkataba ikapelekwa kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Aidha rasimu hii ilipelekwa kwa Katibu Mkuu Wizara ya fedha kwa ajili ya kuidhinisha kipengele cha msamaha wa kodi kwa bidhaa zote zitakazohusu Mradi huu.

Baada ya kupata idhini ya Ofisi hizi mbili ndipo Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa ilisaini rasmi mkataba na Mkandarasi.
Mwisho.

WARAKAWA MR 2 'SUGU' BAADA YA KUTOKA MIKONONI MWA POLISI LEO8 Julai 2011


WARAKAWA MR 2 'SUGU' BAADA YA KUTOKA MIKONONI MWA POLISI LEO8 Julai 2011
, Polisi walinikamata kwa kile walichokiita kuwa ni kufanya mkutano bila kibali.

Hata hivyo, mtiririko wa matukio unaonyesha kwamba polisi walisukumwa na sababu nyingine kwa kuwa suala la taarifa kupelekwa polisi kama sheria zinavyohitaji lilishashughulikiwa na viongozi wa CHADEMA mkoa na wilaya ya Mbeya Mjini".
"Leo tarehe 9 Julai 2011 pamoja na kutolewa kwa dhamana polisi wameonyesha nia ya kutaka kuzuia tamasha la wazi la bure ( ‘Burudani Nyumbani’) ambalo wasanii mbalimbali walikuwa walifanye kwa mwito wangu kwa ajili ya kutoa burudani na kuhamasisha maendeleo".
Polisi wameonyesha vitendo vya kutaka leo kufanyike tamasha la fiesta pekee wakati ambapo matamasha haya yote mawili yameandaliwa na wadau tofauti katika maeneo tofauti.
Mpaka wakati huu ninapotoa taarifa hii wananchi wengi wamejikusanya katika uwanja wa Ruanda Nzovwe ambao ni maarufu kama Uwanja wa Dr Slaa wakisubiri tamasha hilo lakini polisi wameonyesha dhamira ya kutaka kuwatawanya.
Maneno na vitendo vya Jeshi la Polisi vinaelekea kuwa na uhusiano na kauli ambayo niliitoa hivi karibuni kupitia mtandao wa Facebook ya kutohitaji tamasha la Fiesta kufanyika Mbeya.Katika mazingira haya ni muhimu nikaeleza tu kuwa kauli yangu kuhusu Fiesta ilikuwa na madhumuni ya kuanzisha mjadala kuhusiana na suala zima la wizi na unyonyaji uliopo kwenye Sanaa, ambao sio tu unawanyima haki Wasanii, bali pia kukosesha mapato kwa Serikali ambayo yangetokana na kodi kupitia Sanaa ikiwemo muziki.
Nilifanya hivyo baada ya tamasha hilo kutangazwa kufanyika katika eneo ambalo wananchi wamenipa wajibu wa uongozi wa kuwatumikia na kuwawakilisha.
Hivyo kwa niaba ya wananchi wa Mbeya Mjini wanaokosa mapato katika sanaa na wasanii wa Mbeya wanaokosa fursa kutokana na vikwazo nilichukua uamuzi wa kuwakilisha kupaza sauti kama ambavyo nimekuwa nikipaza sauti katika masuala mengine yanayogusa umma kama viwanda, kilimo, barabara za Mbeya Mjini na Haki za wanafunzi wa Elimu ya Juu pamoja na makundi mengine katika jamii.
Niliamua kupaza sauti katika hili kupitia Fiesta, kwa kuwa waandaji wake kimsingi ni sehemu ya vyanzo vya maovu kwenye maendeleo ya muziki hapa nchini. Fiesta ikiwa kitovu cha uonezi kwani hata Wasanii wanaoshiriki halipwi ipasavyo au hawalipwi kabisa. Na hii ni kutokana na wao kutumia njia haramu kuhodhi (monopolise)biashara ya muziki hapa nchini, huku wakiwanyima nafasi watanzania wengi kutumia vipaji na ubunifu wao kwenye biashara ya muziki.Waandaji wa Fiesta ndio wenye redio ya Clouds, Kampuni ya promotion ya Primetime, na pia wanahusika na N.G.O ya THT, waandaji wa matamasha ya injili, ikiwemo kuwa na ushirika katika Tamasha la Pasaka.Huku wakiwa na ushawishi wa hila kwenye Kili Music Awards (One Call Promotion) na mambo mengine yote muhimu yanayohusu Sanaa. Ikiwemo ujumbe wa bodi kwenye Tamasha la majahazi, Zanzibar. Lisingekuwa jambo baya kama wangetumia nafasi hizo kwa haki na maendeleo ya sanaa.

Kutokana na haya, kwa miaka mingi himaya (“empire”) hii imetumia nafasi yake dhalimu kukandamiza watu wengine hasa Wasanii. Kwa mfano kama Msanii hayupo kwenye hiyo “himaya” yao basi hana nafasi ya kutimiza ndoto yake. Na iwapo Msanii hakubaliani na taratibu zao au malipo finyu wanayowalipa Wasanii, basi watahakikisha wanampiga vita na hatimaye kuhujumu usanii wake ili atoweke, kwa kuwa tu hakubaliani nao. Msanii hana haki ya kufanya majadiliano ya kibiashara mbele yao. “Empire” hii imehodhi mpaka makampuni ya udhamini hapa nchini, ambapo makampuni haya yamekuwa magumu kutoa udhamini kwa wadau wengine kwa kuwa tu wao ni washirika wa “Empire” hii.
Walifikia hatua ya kuhodhi mpaka biashara ya usambazaji kwa “Wadosi” ambapo bila ya wao kuruhusu basi Msanii yeyote kazi yake haipewi nafasi ya kusambazwa wala kusikika. Hata kama nyimbo au album yake ni nzuri kwa kiasi gani.Kibaya zaidi wamehodhi mpaka nia njema ya Rais Kikwete katika kusaidia Sanaa na Wasanii. Mfano ni Studio ambayo Rais kupitia Bunge Tukufu la Jamhuri ya Muungano alitangaza kuwa amewapa Wasanii wa Tanzania, lakini baadaye tukashangaa kusikia ipo mkononi! Pia Rais aliahidi na kutoa nyumba ya Serikali kwa Wasanii ambayo ingetumika kuendeshea Studio husika, lakini nyumba hiyo ya Serikali iliyotolewa na Rais sasa iko chini yao na ndio makao ya THT! Wamefanikiwa kumhadaa Rais kuwa wao ndio “Care takers” wa Sanaa ya Tanzania akawaamini na wao wanaitumia vibaya imani njema ya Rais kwao kufanya dhuluma.

Yote niliyoyataja juu, japokuwa hayo ni kwa uchache tu! Yanalalamikiwa sana na wasanii wengi na wadau hapa nchini, japokuwa wengi wameshindwa kujitokeza waziwazi kutoka na vitisho vya watu hawa. Vitendo hivyo wanavyofanya vimeleta madhara katika tasnia ya sanaa na matokeo yake ni kudumaa kwa maendeleo ya muziki hapa nchini. Vijana wengi wanaojihusisha na sanaa wamepoteza matumaini.
Wengi walipata tegemeo la ajira kupitia muziki, lakini hali haipo hivyo tena. Vijana wengi wasanii wamekata tamaa kwa ajili ya ukandamizaji wa “empire” hii.
Na sio tu wasanii na wadau wengine wanawapoteza katika hili. Kwa watu hawa kuhodhi na kuvuruga kabisa biashara ya muziki, hata Serikali inapoteza fedha nyingi kupitia kodi.
Kwa mujibu wa utafiti wa Dr. Jehovaness Aikaeli ambaye ni mchumi wa UDSM, hata katika hali hii mbaya ya biashara ya muziki, Serikali imepoteza Tsh.
Milioni 18, kwa kutokusanya kodi kupitia muziki tu, ukiachilia mbali filamu na sanaa nyingine.
Na iwapo hali itaboreshwa basi kodi hiyo itapanda mpaka wastani wa Tshs.
Bilioni 50 kwa mwaka! Hizi sio pesa kidogo kwaserikali, hasa ukizingatia bajeti ya Wizara inayohusika na Utamadnuni ni Tsh bilioni 14, kwa mwaka, fedha ambazo mara nyingi hawapewi zote kutokana na Serikali kutokuwa na fedha ya kutosha! Lakini hapa utaona kukwa kodi ya mwaka peke yake ingetosha kwa bajeti ya Wizara na ziada kubwa ingebaki kwa miradi ya maendeleo kama kujenga Art Theatres n.k
Napenda ieleweke wazi kwamba mimi binafsi ni “Mhanga” au “victim” wa uharamia wa “himaya” hii kwa miaka mingi, tukupitia migogoro kadhaa ya kibiashara lakini kilichonisikuma kuchukua hatua hii; sio nafsi yangu pekee bali wajibu nilionao hivi sasa kama mwakilishi umma.
Izingatiwe kuwa baada ya mimi kuchaguliwa kuwa Mbunge na wananchi wa Mbeya tena kwa kishindo, Serikali kupitia Wizara inayohusika na utamaduni na pia Baraza la Sanaa (BASATA), walinipongeza kwa barua huku wakinitaka niendelee na harakati za kupigania sanaa na wasanii kwa kutumia nafsi au jukwaa langu jipya Bungeni na nje ya Bunge.
Jukumu ambalo nililikubali kwa mikono miwili kwani harakati za muziki huu si kitu kipya kwangu, ulianza kabla ya Ubunge na ndio ninachokifanya na hasa ukizingatia mimi pia sasa ni Waziri Kivuli (Shadow Minister) wa Wizara ya Habari, Vijana na Michezo.
Kwa lugha nyingine ujumbe nilioutoa wa kukataa Fiesta ni ishara ya mgomo wenye nia ya kutuma ujumbe wa madai ya msingi.
Na historia inaonyesha kuwa, Wasanii wa Nigeria walianza kulipwa vizuri kama wanavyolipwa sasa baada ya kuanzisha migomo dhidi ya mapromota wanyonyaji wa nchini kwao.
Na kama ni suala la kukuza uchumi na ajira, Ni nini mchango wa Fiesta na matamasha mengine kwa halmashauri za mji na majiji wanayopita na kuvuna mamilioni ya fedha kila siku?
Wenu katika kutaka haki,
Joseph Mbilinyi (Mb)
9/7/2011-Mbeya Mjini
Mr. 2 akihojiwa baada ya kutoka mokononi mwa polisi mkoani Mbeya leo mchana. Stori na Picha kwa hisani ya Mbeya Yetu Blog

Wednesday, July 6, 2011

HABARI ZA SABASABA

EPZA yagundua gari la wagonjwa la kisasa

Na Humphrey Shao
MAMLAKA ya Ukanda maalum wa (EPZA)limezindua gari ndogo la miguu mitatu la kubebea wagonjwa lenye vifaaa mbalimbali vya huduma ya kwanza kabla a mgonjwa kufikishwa hospitali na thamani yake  ni sh milioni 10.

Ugunduzi wa gari hilo lilitokana na kuangalia changamoto katika sekta  ya afya  ambalo linahitaji jina halisi  la kitanzania  kama sehemu ya kuenzi kazi za ndani
Akizunhumza na Tanzania Daima  katika maonyesho ya saba saba Mhandisi Ismail Sadiq alisema kuwa gari hilo lina matairi matatu  ambalo linaweza  kuhimili hata katika maeneo tofauti katika miundombinu.

Sadiq alisema licha ya kuwepo kwa miundimbinu mibovu na kuweza kurahisha  mgonjwa kuwahishwa katika huduma za afya.

Mhandisi  Sadiq alisema kuwa, asilimia kubwa ya malighafi iliyotumika kutengeneza hilo imetoka hapa hapa nchini na kufanyiwa uunganishwaji na watanzania hali ambayo ni kupiga hatua katika tknolojia ya kisasa.

Alisema, lengo ni kurahisisha huduma za matibabu kabla ya mgonjwa kufikishwa hospitalini, jambo ambalo linaweza kupunguza idadi ya vifo ya wagonjwa haoi.
"Tumetengeneza gari hili la wagonjwa kwa kuzingatia miundombinu ya nchi yetu, kwa sababu wagonjwa wengi wanafariki kabla ya kufikishwa hospitalini kutokana na ubovu wa miundombinu pamoja na magari ya wagonjwa katika vituo vya afya na hospitali zetu,"alisema Sadiq.

Aliongeza, gari lina uwezo wa kubeba abiria wanane nyuma na mmoja mbele na kwamba linaweza kutembelea umbali wa kilomita 120 kwa saa katika barabara tofauti,hivyo basi serikalimawadau mbalimbali wanaotoa huduma za afya nchini inapaswa kuwasiliana nao ili waweze kununua na kuzisambaza kwenye hospitali na vituo vya afya.

Alisema,EPZA, wanatarajia kutengeneza aina tofauti za magar kwa ajili ya matumizi tofauti ili wananchi waondokane na uhaba wa usafiri katika maeneo yao, jambo ambalo wanaamini linaweza kupunguza tatizo la usafiri nchini.

Alisema,kutokana na hali hiyo wananchi wanapaswa kutambua kuwa, hapa nchini kuna watalaam mbalimbali ambao wanaweza kufanya kazi tofauti bila ya kutafuta watalaam wa nje, hivyo basi serikali inapaswa kushirikiana nao ili waweze kuongeza ujuzi.

Sadiq alisema ,wananchi wanapaswa kuwa wazalendo kwa kununua bidhaa au mali zinazolishwa na wazalendo wenzao ili waweze kukuza uchumi na kuinua kipato.

mwisho
Makampuni 7 kushindanishwa kujenga daraja la kigamboni -Dk.Dau


SHIRIKA la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) limesema  kati ya makampuni 16 yaliyojitokeza kwa ajili ya mchakato wa kutafuta mdhabuni wa  ujenzi wa daraja la Kigamboni zote ni za kigeni na hakuna kampuni hata moja ya kitanzania iliyoomba tenda hiyo.


Akizungumza na Waandisi wa habari katika Maonyesho ya 35 ya Kimataifa ya Biashara yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Nyerere  Dar es Salaa, Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Dkt. Ramadhani Dau alisema kuwa kati ya kampuni hizo saba zimeteuliwa kwa ajili ya kushindanishwa.

"Kazi sasa tumeanza kutangaza  tenda kwa  kampuni kwa ajili ya ujenzi wa Kigamboni na  kampuni 16 yamejitokeza  kila mmoja kuomba kazi hiyo ua ujenzi, lakini tumeteua kampuni saba pekee ambazo tunazishindanisha itakayopatikana ndiyo itakayopewa kazi ya ujenzi huo,"alisema.

Alisema kuwa ifikapo Oktoba mwaka huu watakuwa wameshapata maamuzi ya nani atakayejenga na kwamba kabla ya mwisho wa mwaka huu ujenzi huo utakuwa umeanza na utachukua kati miaka miwili au miwili na nusu kukamilika kwake.

Dau alisema kuwa katika mchakato huo wa kutafuta mkandarasi kwa ajili ya ujenzi huo watakuwa makini kuakikisha kwamba yule anayepatikana ni mzoefu na ujenzi wa madaraja na wapi alikwishawai kujenga.

"Tutahakikisha kwamba tunafuatilia madaraja aliyojenga kama yamejengwa na kampuni yake, ni lazima tuwe makini katika uchaguzi kwani mradi huu ni mkubwa na wa kipekee nchini mwetu,"alisema.

Alisema kuwa hao mradi huo, pindi utakapoanza utatoa ajira kwa Watanzania na wale wengi watakaoshiriki katika ujenzi huo watapata uzoefu na kusisitiza kwamba Kampuni za Tanzania hazikujitokeza kuomba tenda hiyo kwa sababu hawana uzoefu na kwamba nchi zilizojitokeza zina uzoefu kwa sababu wana madaraka katika nchi zao.

Dkt. Dau alisema kuwa miaka 50  ya Uhuru, NSSF wamefanya mambo mengi na Kusini mwa Jangwa la Sahara ni Shirika pekee lililofanya hivyo na wanachama sasa wanachukua mafao siku 14 badala ya 30 kama ilivyokuwa nyakati za nyuma.

Alisema kuwa Kauli mbiu ya Maonyesho haya mwaka huu ni sherekea miaka 50 ya uhuru na wanajikita vipi katika kilimo Kwanza , ambapo alisisitiza kwamba NSSF itaendelea kuunga mkono Kilimo Kwanza katika maeneo mbalimbali.

Mwisho
IKIWA imebakia siku moja kumalizika kwa Maonyesho ya Kimataifa ya Biashara (sabasaba) wananchi wanaotembelea maonyesho hayo waliutaka Uongozi wa Tan Trade kuongeza siku tatu ili waweze kuendelea kujionea bidhaa mablimbali zilipo katika maonyesho.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti na gazeti hili wananchi hao waliokutembea maonyesho hayo waliofurika katika banda la Maliasili walisema siku nane azitoshi kwa maonyesho ya sabasaba.
Mkazi wa Ubungo Enock Yusin alisemaMaonyesho ya sabasaba ni makubwa Tan Trda walitakuwa kuyatengea muda wa siku 14 ili kila Mwananchi aweze kuja kujionea .
"Leo ni tarehe sita imebakia siku ya kesho na kesho kutwa kitu ambacho ni wananchi wachache watapata nafasi ya kuja kutembelea moanyesho hayo lakini yangeweza kuongezwa siku yakiwa kama wiki mbili maamini wananchi waliopo mikoani wangeweza kupata nafasi ya kufika na kujionea"alisema Yusini
Yusin alisema kwa maonyesho kama hayo mtu ambae atapata nafasi ya kutembelea ni vigumu sana kufika katika maonyesho hayo na kuweza kutembelea katika mabanda mbalimbali yaliyopo katika maonyesho.
"Uhalisia wa watu waliofika kwa muda huu katika banda la Mali asili naamini atakapo rudi nyumbani atweza kudisikia na kusabisha wengine kuvutiwa kuja kujionea hali kuwa maonyesho yameisha"alisema
Naye Mwananchi aliyetembelea katika maonyesho hayo Elizabeth Swai aliyetembelea maonyesho hayo pamoja na familia yake aliishauri Mamlaka ya Biashara Tanzania (Tan Trade) kutafuta uwezekanao wa Maonyesho hayo kufanyika katika mikoa mingine ya Tanzania tofauti na Dar es Salaam.
Alisema Maonyesho ya sabasaba yanawakutanisha watu wengi ikiwemo wafanyabiashar na wajasiliamali kwa kutumia nafasi hiyo Tan Trde ingechukua majukumu ya Maonyesho hayo kufanyika na mikoa mingine.
"Naamini maonyesho hayo yangeweza kufanyika kama Dodoma,Mbeya Arusha naamini katika kilio cha wananchi wanaotegemea kujiajiri kisingekuwepo"alisema Swai
Maonyesho hayo yaliyohudhuriwa na nchi 17,kampuni 1200,tasisi binafsi 28,tasisi za umma 68 yanatarajia kufikia kilele chake siku ya Ijumumaa amabpo yatafungwa na balozi kutoka katika nchi moja iliyoshiriki maonyesho hayo.
MWISHO
Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT), chombo kinachoziunganisha halmashauri zote 133 za  Tanzania bara, jana imetangaza mpango dhabiti ukaosaidia kuzitetea, kuziwakilisha na kuzipa huduma Halmashauri hizo ili ziweze kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi na kasi.
Mpango huo kabamba umetangazwa rasmi na Katibu Mkuu wa ALAT, Habraham Shamumoyo katika maonyesho ya 35 ya Biashara ya Kimataifa yanayoendelea mjini Dar es Salaam (DITF). ALAT imeungana na waonyeshaji  na watoa huduma mbalimbali katika maonyesho hayo ambayo ufanyika kila mwaka katika viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere.
Akiongea katika maonyesho hayo, Katibu Mkuu wa ALAT alieleza ya kwamba wamejipanga kushiriki kikamilifu katika maonyesho ya kimataifa, kwa sababu ya dhamana kubwa walionayo ALAT na wanachama wake katika kusimamia utelekelezaji wa mipango ya maendeleo ya kitaifa nchin inzima.
“ALAT na halmashauri wanayo kila sababu ya kushiriki ili kuelimisha wananchi, wadau na wafanyabiashara wa ndani na nje juu, majukumu ya Jumuiya na namna inavyofanya kazi,” alisema Shamumoyo.
Aliongeza kwamba mbali hilo, ushiriki wao katika maonyesho utasaidia watu kuelewa mpango dhabiti wa ALAT wenye lengo la kusaidia Halmashauri zote nchini ili ziweze kusimamia na kutelekeleza majukumu yao kwa udhabiti kwa lengo la kuharakisha maendeleo kwa Tanzania, ambao wengi wao wanaichi katika lindi kubwa la umaskini.
Kwa mujibu wa Katibu wa ALAT, ili kuweka ukaribu na wananchi, jumuiya hiyo imewakaribisha baadhi ya wanachama wake katika maonyesho hayo  ili kuweza kuonyesha huduma wanazotoa kwa wananchi na kuweza kupokea malalamiko na ushauri mbalimbali kutoka kwa wananchi.
Hata hivyo, aliongeza, halmashauri zinazoshiriki katika maonyesho haya, zinapata faida nyingi, na kuzitaja baadhi ya faida kama vile kujitangaza na kutangaza fursa zilizopo za uwekezaji ndani na nje ya nchi, kuwasiliana na mashirika mbalimbali yaliyoshiriki kutoka  afrika ya mashariki, kati na kusini na hata duniani kote ili kuweza kupata fursa za kujiendeleza katika nyanja mbalimbali, kuwawezesha wajasiliamali wa Halmashauri kupata fursa ya kuonyesha na kuuza bidhaa zao na kutengeneza mahusiano na wadau mbalimbali na hatimaye  kufanya majadiliano ya kibiashara.
“Faida nyingine kama vile kuiwezesha Halmashauri kupata fursa ya masoko ya nje ya bidhaa zinazozalishwa katika Halmashauri  hasa katika nchi za Afrika Mashariki kati na Kusini, kutoa fursa ya pekee kwa wajasiliamali na wafanyabiashara katika Halmashauri kuweza kukutana na wenzao kutoka kwingineko duniani katika kubadilishana ujuzi na uzoefu wa kibiashara,” alisema katika wa ALAT.
Katika maonyesho haya Halmashauri za Ilala, Temeke, Kibaha mji na Tandahimba zimeshiriki pamoja na wajasiriamali wao, kwa mujibu ya taarifa iliyotolewa na ALAT jana katika maonyesho.
 Mwisho

Tigo waachangia katika sekta ya Elimu
Kampuni ya simu za mkononi, Tigo itafanya kampeni maalum ya kuchangia elimu inayofahamika kama ‘Tigo tuchange’ itakayofanyika Julai 9, 2011 jijini Dar es Salaa.
Akiongea jijini Dar Es Salaam, afisa Uhusiano wa Tigo Jackson Mmbando alisema kwamba kampeni hiyo itahwausisha wateja wote wa Tigo wanaotumia huduma ya Tigo Rusha ambapo watanunua muda wa maongezi kupitia huduma hiyo.
Kampeni kwa muda wa saa moja kuanzia saa tatu  asubuhi mpaka saa nne. “Ukinunua muda wa maongezi kwa kutumia huduma ya Tigo Rusha ambao utazidi kiasi cha shilingi mia tano tayari utakuwa umechangia kusiadia elimu hapa nchini,” alisema Mmbando.
Halikadhalika alisema kuwa ukinunua muda wa maongezi utazawadiwa mara mbili ya muda wa maongezi wa kiasi ualichonunua. Kiasi cha pesa kitakachopatikana kitatumika kununulia vitabu ambavyo vitaenda kusaidia katika shule za msingi hapa nchini.
Alisema kwamba Tigo wameamua kufanya utaratibu huo wa kusaidia sekta ya elimu baada ya kugundua kuwa sekta ya elimu bado kuna huitaji wa vitabu katika baadhi ya shule za msingi hapa nchini.
Baada ya kukusanya pesa Tigo itashirikiana na Taasisi ya Elimu Tanzania ambao ndiyo watatoa orodha ya shule ambazo zinahitaji msaada wa vitabu. “Tumefurahishwa na hili wazo lenu na tunaahidi kuwaunga mkono hadi mwisho na wazo lenu limekuja waka muafaka ambao kweli watoto wetu wanahitaji vitabu,” alisema Charles Mapima Meneja wa elimu TEA
Mbali na vitabu, Mapima alisema kwamba kuna matatizo mengi ndani ya sekta ya elimu kama ukosefu wa mabweni ya wasichana katika na  vitabu kwa shule za msingi na sekondari. 
“Tigo imeonyesha kuwa na nia yakusaidia shule za msingi na kuwapa vitabu. Tuna takwimu kwamba kila kitabu inatumika na wanafunzi hamsini katika shule ya msingi mmoja,”   alienda kusema Mapima 
End

MAKAMU WA RAIS WA JAMUHURI WA MUUNGANO WA TANZANIA DR.GHALIB BILAL ALIPOKUWA AKIFUNGUA MAONYESHO YA BIASHARA SABASABA


MAKAMU wa Rais wa Jamuhuri wanmuungano wa Tanzania Dr.Ghalib Bilal alipokuwa akifungua kampuni ya GS 1 ambayo inashughulika na utambuzi wa Bidhaa mbalimbali za kitanzania(Picha Na Tiganya wa Maelezo)

MAKAMU WA KWANZA WA RAIS WA SERIKALI YA MAPINDUZI ZANZIBAR ALIPOTEMBLEA AMAONYESHO YA SABASABA



MAKAMU wa kwanza wa Rais wa serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mahalimu Seif Sharifu Hamad kushoto na upande wa kulia ni waziri wa fedha mustapha mkulo wakati walipotembelea amabanda katika maonyesho ya biashara hyan kimataifa ya sabsaba(Picha kwa Hisani ya Tiganya Maelezo)

WAZIRI MKUU WA TANZANIA MIZENGO PINDA ALIPOTEMBELEA MAONYESHO YA 35 YA BIASHARA SABASABA

Waziri mkuu wa Tanzania Mizengo Pinda akizungumza na mtoto anayesomeshwa na mfuko wa Pensheni wa PPF ambapo waziri mkuu aliyataka mashirika mengine kuiga mfano wa shirika hilo kwa kuangalia kuanzisha mfuko wa Pensheni ya masomo kwa yatima wanaofiwa na baba zao au wachangiaaji wanao fariki(Picha Na Tiganya wa Maelezo)

Monday, July 4, 2011

H.Baba akiwa katika pozi

H BABA

H baba wasanii tujitambue sisi kwanza

Na Humphrey Shao

KAMA unazungumzia wasanii wanaofanya vizuri jukwaani katika mtindo wa muziki wa Bongo Fleva hapa nchini utasita kumtaja kijana kutoka mkoa wa Mwanza Hamisi Ramadhani(H baba) kutokana na staili yake ya potezapoteza.

H baba ambaye alizaliwa mnamo mwaka 1987 mkoani mwanza anaeleza kuwa licha ya muziki huu wa kizazi kipya kufanya vizuri katika ukanda wa Afrika Mashariki na kati bado kunatatizo la wasanii kutambua majukumu yao katika jamii inayowazunguka.

H baba ambaye kila siku anatembea na falsafa kuwa mama ndio chanzo cha mambo yote hivyo anahakikisha mapato anayopata anagawa nusukwanusu na kumpelekea mama yake.

Anasema kuwa hali hiyo ilishindwa kueleweka mara baada kutakiwa na timu ya Azam kwani alihitaji kiasi cha shilingi milioni ishirini ikiwa kumi kwa mama na kumi kwake yeye lakini walishindana kutokana na kiasi hicho kuonekana kuwa kikubwa.

Baada hapo ndipo aliamua kujikita zaidi katika muziki wa Bongofleva ambao ndio sehemu yake ya maisha na anafanya muziki kuwa ndio chaguo la kwanza la kuingiza mapato katika maisha yake ya kila siku.

Anasema licha ya muziki huu kuonekana kuwa unamafanikio makubwa kwa wasanii wenyewe na hata kupenya katika jamii kwa kasi kubwa lakini bado mafanikio yake sio kama vile yalivyo katika hisia za wapenzi wa muziki huu.

Anaeleza kuwa muziki huu umepungua chati kwa sasa kutokana na bahadhi ya watu waliopo katika tasnia hii kuhodhi muziki huu kama wa kwao hali inayo hatarisha ustawi wa wanamuziki wa kweli na wasisi wa muziki huu.

Anaeleza moja ya chanagamoto wanazo kumbana na nayo wasanii wamuziki huu ni malipo duni ambayo yanatolewa na mapromota ambao ni matapeli wa maneno na kuwasainisha mkataba feki wasanii.

"Hali ilivyo katika muziki hapa nchini ni mbaya kwani wasanii awajitambui na wamekuwa watu wakudhulumiwa kila siku kama mimi ninavyokueleza albamu yangu ya mpenzi bubu sijalamba hata shilingi kumi zaidi ya propaganda"alisema H baba.

Anaeleza kuwa changamoto nyingine wanayopata wasanii wa hapa nchi ni hile matamasha ya kimataifa yanayo andaliwa nchini kutotoa kipaumbele kwa wasanii wanaoweza kufanya vizuri na kuchagua kwa kujuana hali inayo shusha muziki wetu kwa wageni.

Anaeleza kuwa hata vyombo vya habari vya ndani vimeshindwa kutoa thamani kwa msanii wa nyumbani pindi kazi yake inapoibiwa na kusapoti mwizi wa kigeni.

"ninathubutu kusema kuwa nyimbo inayowika sasa hivi ya Abha Prakatatumba ni kopi ya wimbo wangu wa mpenzi bubu ambao ulitoka miaka mitatu iliyopita lakini leo watu wamekopi sisi nyumbani tunaona kitu kipya"alisema H baba.

Anasema kuwa wasanii wengi wa kitanzania sio wabunifu katika utunzi hali inayo hatarisha ustawi wa muziki huu ambao tunaita wa kizazi kipya kwa ni karibu wasanii wote wanaimba mada moja.

Anaeleza kuwa ni vema wasanii wakawa wachambuzi na watafaiti wa mada mbalimbali zinazo igusa jamii hili waweze kutumia muziki huu kuelimisha umma unao tuzunguka.

Anaelezakuwa kutokana na hali hiyo ameamua kuja na staili mpya inayokwenada kwajina la Bongo Bolingo Fleva ambayo anamini itampa sura mpya katika muziki huu whuko tunako elekea.

Anasema kuwa lengo la kufanya mtindo huo wa bongo bolingo ni kuhakikisha kuwa anafanikiwa kuteka soko la Afrika Magharibi na ufaransa ambako bolingo inapendwa.

Anasema kuwa umahairi wake wa kutumbuiza kwa uhakika kwa muda wa masaa matatu kitakuwa moja ya kigezo kitakacho wavutia wapenzi wake wamataifa hayo mapya pindi ataka[po penya kutumbuiza.

Anasema kuwa yeye ndio msanii pekee Afrika Mashariki aliyeweza kuvunja rekodi ya msanii kutoka Uganda Joseph Camerion kwa kufanikiwa kufanya show kwa muda wa saa tatu akimzidi mganda huyo nusu saa.

Anaeleza kuwa yeye kama yeye sasa ametanuka kisanaa na ategemei sanaa ya muziki pke yake kwani sasa anakairi uwezo wake wa kufanya filamu umeongezeka kwa kasi kubwa kuliko hapo awali kwani amepata kushirikishwa filamu nyingi sana na zimefanya vizuri sokoni.

H baba ambaye ni mtoto pekee katika tumbo la mama yake anaeleza kuwa katika maisha yake ya kila siku yupo tofauti na watu wengine kwani atumiii kilevi cha aina yoyote na ana mpenzi mmoja ambaye ni mchumba wake anayefahamika kwa jina la Frola mvungi.

Anasema kuwa kama msanii unajieshimu na unajua nini unafanya unafasi ya kuficha mchumba wako ninani kama unaficha basi ujue kuna walakini katika mwenendo wako wa kila siku.

Anasema kuwa yeye amekuwa akiishi maisha ya kawaida sana kiasi cha kusema kuwa anashangaa watu ambao wamejiunga katika mtandao wa Face book kwa ajili kufanya ufuska hali iliyomfanya yeye kuchukia mtandao huo.

Nakama kuna kitu ujui kuhusu mimi mimi sipendi kwenda klabu ukinikuta klabu ujue siku hiyo hapo ninashoo kwani nahisikkwenda klabu nitapoteza heshima yangu na kujishusha mwenyewe.
Na Humphrey  Shao

WANANCHI wa ishio Kigamboni kata ya gazaulole wamehakikishiwa kupata huduma za kijamii katika mradi mpya wa upimaji viwanaja unao endeshwa na Halmashauri ya Manispaa ya Temeke.

Hayo yameelezwa na Mkuu wa wilaya hiyo Bi. Chiku Galawa alipotembelea eneo hilo hili kutoa ufafanuzi kwa wakazi wa eneo hilo na kuwataoa hofu ya kuwa eneo hilo limeuzwa kwa watu kutoka nje ya nchi.

Mkuu Huyo alisema kuwa mradi huo wa upimaji viwanja unalengo la kuboresha makazi ya watu waishio eneo kwa kuweza kufikiwa na huduma muhimu za kijamii kwa urahisi na kuepukana na tatizo la makzi holela ambalo linaweza kutishia ustawi wa mji huo.

“Ni vema mkawa makini na kutoa ushirikiano kwa wapimaji pindi watakapo kuja na kuepuka maneno ya uchochezi ambayo yanaweza kuleta migogoro amabayo aina tija kwa maendeleo ya yenu na Temeke kwa ujumla”alisema Bi.Galawa.

Alisema kuwa mradi huo ambao unalengo la kumnufaisha mkazi wa gezaulole mojakwamoja kwa kupatiwa hati rasmi ya kiwanja mabacho kitapimwa hali itakayowapa fursa ya kuweza kuchukua mikopo sehemeu mbalimbali.

Pia alieleza kuwa wananchi ambao maeneo yao yatatwaliwa yatalipwa kuanzia Mazao,Kiwanja na nyumba ambazo zimejengwa katika shamaba husika pamoja na kupatiwa kiwanja kipya kilichopimwa.

Alisema kuwa zoezi hilo litakapokamilika kutasidia ukuaji kwa kasi wa eneo hilo kutokana idadi ya watu kuongezeka hali itakayofanya gharama za viwanja vyao kupanda na kuweza nyumba zao kupangishwa .

mwishoooo
TRA load development councils.

By Humphrey Shao
TAX Payment for any nation on earth is the main source of income and a way of strengthening relations between citizens and their nation the world many countries have depend on income taxes and various external and internal as the axis to operate the government in general.

But here at home wondered whether the government failed authorities consider them a strong response to all those who allegedly cast them to our Board on a matter of getting revenue, does the law say in it? Then I decided to sink further monitor this issue.

These complaints are often provided in the various sessions of the committees, the House of Councillors, even in those of the rank held by the county executives of counties in our municipality.

In accordance with the laws of the state financial street of  1982 Section 14, states that each council should ensure it adds revenue from its own resources to provide community service.

Property taxes are one of the main sources of hot entry earnings drugs agreed by the Council and central government after the cancellation of various tax sources that are brought public nuisance.

Revenue collected from buildings is the source easy to earn money councils as this source Monitored well can board our grips and myths of dependence from donors and grant money that often comes late in a project implementation or delivery, and left to provide the balance after a year The money involved is finished.

Repayment tax very soon a long history of 3,000 years iliyopitaenzi rule by Kingship were takiw I send you money for them if they do not rent.

In America about 200 years passed  buildings tax were collected for the purpose of getting money for the use of the land army during the war with France.

President Theodoro Roosevelt (1901-1909) and President Woodrow Wilson (1913-1921) both from America, were seen in state be appropriate to develop the collection of taxes on buildings due to its beneficial one if earnings enable the host operating income also recorded by the government  for social services used by rich and poor together.

Here I get to talk in detail fasi and official relationship of Temeke Municipal Joyce Msumba explains how Temeke Municipal failed to achieve its goal due to the revenue authorities in the country (TRA) failure to collect sufficient funds derived from property taxes.

She states that she submitted a statement of income and expenditure for the deputy director of the Municipal Temeke Engeniere Gaston Gassana before the councilors, Executive, People and mamber of the Press on the council of the month March 2011 and the committee of permanent head of the department  Machicho Jane explained by estimates of Shs 2,139,373,000,00 collect from property taxes for fiscal year 2010/2011 Temeke suceed to collect Tshs 415,483,488,00 which is equivalent to only 19% percent.

The situation has sparked many questions they asked when the council as the executive council of the TRA that they questioned why and what is the problem, how TRA Board  failure and income.

Msumba explained that the TRA act as Teller's window stay and wait while the taxpayers of the buildings is understood any merchant or any resident of Temeke does not pay  tax window without using force or be educated

She explains that there are no mobilization, education and monitoring large taxpayers, especially those from Tanzania Revenue Authority.

She explains that In Tanzanaia Assessment done to identify a number of buildings in 1993 and 1994 and repeated in 1998 under a World Bank fund.

"Council of Temeke Manispa  evaluation using only its own executives in 2001 to 142,000 in 2003 to identify houses and records its in normal rate of under ten thousand shillings without  quality, location or owner homes clad with how it was able  because there are the houses of mud and grass on and there are those of brick and corrugated glass, "said Msumba.

She explains that unfortunately in 2008 July TRA reverted role corrected taxes on buildings and parliament Glorious Republic of Tanzania, and they took the figures for the number of buildings as and Count as taxpayers they this board nuisance major taxpayers with housing grass.

She argues that this move was made in parliament and also the venerable Rainald A. Rope (MP) suggested that the exercise of arbitrary assessment held a big annoyance for taxpayers and the scrutinized anew.

This means that with the vision of 2025, the National Strategy for Growth and Poverty Reduction (PRS II), the Millennium Goals (MDGs), the CCM election manifesto of 2005, the goals of the revenue authority in the country.

Tanzania in an improvement of five years 2008 / 9 to comply with the law of fedaha 2012/13na local 'chapter 290', one of the goals is to handle and forgiving taxes on their homes than the elderly aged 60 years that their economic situation doesnot  pay taxes and be given authority and leadership of local government involved that really can not afford to pay taxes and reduce the nuisance.

Authority in collaboration with TRA  City Council and Borough of Ilala, Kinondoni and Temeke did re-evaluation of the buildings last year from May 2010 and continuing until now, under the local government and 0.2 in 1983 and revised in 2008 give the authority responsible for listing all buildings and deal value to identify all buildings in the city and what is its value.

Msumba  states that Temeke Municipal Councils are among the Fortune with a large corporate buildings, Industry, Port and the international sports arena of the State, which alone are good sources of property taxes but to note is that the companies and other factory owners to avoid paying property taxes and the revenue authority not to consider them  any crack.


She explains that according to the TRA tax collections of buildings from owners of large buildings in Industry and Temeke Municipality between July 2008 until March 2011 that is 500,000,000,00 between 1.3 billion paid to municipalities that are required from companies which Temeke leaving small taxpayers.

She explains that if the TRA could well councils manage tax collection  here for property taxes when they enable councils to improve infastructure method, garbage disposal and public education.

He notes that the revenue authorities have failed to keep clear records of who calipers and who has not paid the rent of his building and bring inconvenience to the borough failed to cease its .

So then from this situation, I suggest authority to hava capacity offices of the Division in order to receive the rent of buildings and instead of relying on the office just to keep executives of revenue among offices of the Council is to reduce nuisance taxpayers, it is also necessary to improve their memory.

So it's time to go to the TRA started using modern technology developers who pay for identified and non identified pay and non pay atua consider them with enough to declare in the media.


ENDSSSSSSSSS

Sunday, July 3, 2011

mashekh wakitafakali jambo wakati wa arobaini ya aliyekuwa mnajimu mkuu Afrika mashariki Shekh Yhaya Husein

Makala ya mama mipango

Mariamu Ismail"Mama Mipango" Mshairi mwenye kiu ya kupandisha chati ngoma za asili.

Na Humphrey Shao.

Hivi karibuni kulikuwa na Tamasha la mwezi la jukwaa la sanaa ambalo lilifanyika katika ukumbi wa Baraza la Sanaa la Taifa(BASATA) na kushirikisha wasanii wa kada mbalimbali ndipo nilipopata nafasi ya kuzungumza na msanii huyu mkongwe anaye fahamika kwa jina la Mama mipango.

Mama mipango anaanza kunieleza hasa nini maana ya ngoma na kusema kuwa Ngoma ni lea ya utaratibu uliowekwa na watumiaji wenyewe .

Ngoma ni uchezaji wa wa viungo vya mwili kwa mnyambuliko na utaratibu maalum kufatia mapigo ya ngoma yenyewe ala kulingana na kabila husika na desturi zake.

Anaeleza kuwa hapo zamani mababu zetu walitumia ngoma kama chombo cha mawasiliano kwa makabila mengine walitumia kwenye sherehe mbalimbali kama chombo kikuu cha kutoa burudani.

Anasema kuwa ngoma zilitumika kwenye jando na unyago hata baada ya kazi kama chombo cha kutolea mafunzo ,maonyo au kuasa jamii ijikosoe kwa njia ya nyimbo zinazo tungwa na waimbaji maharufu .

Anaeleza kuwa nyimbo za ngoma zilitumika kama ishara ya jambo fulani hali iliyopelekea kufikisha taharifa katika vijiji vingi sana hii ni kwa sababau ngoma inasikika sana.

Hivyo basi viongozi wanapaswa kutumia ngoma kama chombo mawasiliano na kutoa ujumbe kwa jamii kwa kuanza kutumia zilizopo nchini na wasanii wa ngoma za asili kama chombo muhimu cha kuwaleta wananchi pamoja.

"Kwa hivyo basi ni tofauti sana kati ya ngoma na sanaa nyingine duniani ngoma inamvuto wa pekee kwa ni chombo ambacho kinachoweza kutumika kutambulisha utaifa wa mtu fulani"anaeleza Mama Mipango.

Hivyo ni muhimu serikali ikatenga fungu kwa ajili ya kuenzi sanaa ya ngoma hapa nchini hili kujenga sura ya utaifa kwa kurthisha kizazi chetu ngoma za asili.

Anaeleza kuwa Sanaa ya ngoma inarithiwa na sanaa hii ni raisi kurithi kuliko sanaa yoyote ile hapa duniani Tanzania ilitumia ngoma katika kudai uhuru na kuwfariji mashujaa mabalimbali walipotoka vitani hivyo basi ni vema utaratibu huu wa kutumia ngoma ukaendelezwa kwa kupitia wasanii wetu wa ngoma za asili.

Ni vema serikali ikavuta kumbukumbu hapo awali kupita radio ya taifa TBC watu waliweza kuwasilisha ngoma za asili kama sehemu ya burudani kwa watanzania na umma mkubwa ukaburudika na kuelimika na ngoma kupita TBC enzi za mzee moris watu walipigiwa ngoma kujua kua kunajambo linataraji kusemwa.

"Ngoma za asili zimetoa mchango mkubwa katika taifa hili ngoma imechochea kudumisha amani Tanzania bara na visiwani zimefanikiwa kuleta maendeleo makubwa sana hapa nchini na kujenga dhana nzima ya uzalendo "Anaeleza Mama Mipango.

Hivyo basi ni vema ngoma zikaanza kutumika katika kampeni ya kilimo kwanza kama sehemu ya kuleta maendeleo hapa nchini ikiwa na lengo la kuongeza tija na hamasa katika kampeni hii ya kilimo katika sehemu husika kutumia ngoma za asili katika makabila yetu.

Ngoma za asili za makabila miamoja na ishirini zimechezwa hapa nchini hivyo basi kama zitatumika kama zilivyotumika hapa nchini wasanii na vijana wetu wataweza kujiajiri kwa kutumia ngoma za asili.

Anaeleza kuwa kuna ngoma za ndani ambazo zilitumika kwa ajili ya kuwafunda Vijana hili waelewe maadili mema hivyo basi ni vema wataalamu wa ngoma hizi wakapatiwa eleimu ya kisasa zaidi hili waweze kutoa na elimu ya maisha kulingana na hali halisi ya kisasa.

Anaeleza kuwa ngoma hizi ni darasa tosha ambalo linaweza kutumika kuikwamua jamii yetu katika majanga mabalimbali hili kuokoa uchumi wa taifa hili.

Ngoma za unyago zinataumika kukataza mabaya yote na matendo machafu na mambo mengine ambayo hayakubaliki hivyo basi ngoma hizi zikitumika vizuri itasidia hata kupunguza migomo ya wanafunzi katika shule zetu.

Anaeleza kuwa ngoma za asili zinanafasi kubwa kurekebisha mambo maovu ambayo ni kero katika jamii inayotuzunguka.

Mwisho ninapenda kuwaasa wasanii wenzangu ili tufanye kazi zetu ipasavyo ni lazima tujitambue ni nani katika jamii inayotuzunguka hivyo ni vema tuanze kutoa elimu ya ngoma za asili na tusiwe tegemezi.

mwishoooooooo
Na Humphrey Shao.

IMEELEZWA kuwa  tatizo la mimba za utotoni na utoro mashuleni katika mkoa wa Ruvuma unasababishwa na hali ya umasikini wa kipato cha  wananchi wa mkoa huo.

Hayo yamesemwa na wadau na wanaharakati wa mkoa wa ruvuma ambao walihudhuria Warsha ya siku nne iliyo andaliwa na Mtandao wa Jinsia Tanzania(TGNP) Mkoani hapo katika taharifa yao iliyotumwa katika vyombo vya habari jana.


Wameeleza kuwa Pia tatizo hili linasababishwa na wananafunzi kutembea umbali mkubwa kutoka nyumbani kwenda shuleni na Wanafunzi kukosa huduma muhimu na  hasa chakula cha mchana shuleni na kuwasababishia kukutana na vishawishi wakati wakitafuta chakula .

"Sisi wanajamii kutoka katika Mashirika  yasiyo ya kiserikali na Taasisi nyingine za kutetea Haki za Binadamu na Usawa wa Kijinsia,  tumeshiriki warsha ya uraghibishi ya kujenga nguvu ya pamoja  iliyoendeshwa na Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) kuanzia tarehe 28 Juni hdi 1 Julai,2011, na kuibua mambo mbalimbali yanayoikumba jamii ya mkoa wetu Kwa pamoja  tunaitaka serikali kusikiliza kilio chetu juu ya changamoto zinazoukumba mkoa wetu na kuchukua hatua za haraka"walieleza wanaharakati hao.

Pia wameitaka serikali kuangalia upya na kufutatilia kwa umakini suala la ugawaji wa pembejeo za kilimo  ili zipatikane kwa wakati na usawa kwa kila mmoja  kama wakulima na kushughulikia pembejeo zipatikane kwa wakati unaofaa badala ya kuechelewa.

Pia waliitaka Serikali kuhakikisha kuwa mbolea inaletwa  mwezi wa nane hadi wa kumi ili tunapokwenda mashambani kulima tuwe  tumeshapata mbolea na tunaitaka serikali kufuaatilia  zoezi zima la ugawawaji wa mbolea na ujazwaji kwenye mifuko kwani kuna baadhi ya mifuko inakuwa  pungufu ipo chini ya  kilo.50, mingine inachanganywa na mbolea ya minjingu.

Aidha waliipongeza serikali lakini kwa kuwa imejitahidi kwa kiasi kikubwa kuhamasisha Kilimo kwa nguvu zote  kwa ajili ya kuzalisha chakula cha kutosha na kuweka wazi kuwa zoezi  hilo limefanikiwa na sasa mkoa wa Ruvuma umeweza kuwa miongoni mwa mikoa michache inayoweza kulisha chakula nchi nzima na hata nje ya nchi.


Mbali na hayo yote wameeleza changamoto kubwa kwa wakulima wadogo Ruvuma ambazo ni  Serikali itutafutie masoko ya kueleweka ambapo baada ya kuvuna  wakulima waweze kuuza mazao yao kwa haki bila kulanguliwa.

Walimaliza kwa kuelaza kuwa ni vema Serikali idhibiti walanguzi wanaopita mashambani kununua mazao na kuhakikisha inadhibiti bei za chakula masokoni ili mkulima apate faida ya kile alichovuna na asiingie hasara kubwa na kusema kuwa Soko la sodeco bei zake bado  haziendani na hali halisi ya   bei za chakula hali inayo fanya wakulima tumekuwa tukilanguliwa na kulazimishwa kuuza kwa bei kidogo.

Mwishoooooo