Wednesday, May 16, 2012


Rio Ferdinand Beki aliyetoswa Euro 2012 kwa fitina
  Godlisten Shao na Mashirika ya Habari.
SIKU ya tarehe 22 Julai mwaka  2002,Rio Ferdinand alijiunga na klabu ya , Manchester United, kw amkataba wa miaka mitano na kuwa mchezaji ghali aneyecheza safu ya nyuma katika historia ya  uingereza , akichukua nafasi ya beki aliyekuwa ghali kipindi cha mwaka 2001 Lilian Thuram.
Ferdinand ambaye ni raia wa uingereza alizaliwa Novemba  7, 1978 katika kitongoji cha  Peckham, mjini London, nchini England,na ni mchezaji anayecheza nafasi ya nyuma katika klabu ya Manchester United mpaka sasa na amekuwa mchezaji wa kulipwa kuanzia mwaka 1997.
Beki huyo ambaye alihamishwa kwa ada ya pauni milioni ishirini za uingereza na kuifanya klabu yake ya awali ya leeds kumtangaza kuwa inamuuza mchezaji huyo kwa ka zaidi ya pauni milioni thelasini.  
 Leeds United baadae ilichukua kiasi hicho chapesa zake za awali kama na kusaidia timu hiyo ambayo ilikuwa na tatizo la kiuchumi kipindio hicho, na kufanya Ada kamili ya kumuhamisha mchezaji huyo kwenda Manchester United kuwa Pauni milioni 33.
 Ferdinand ambaye alionekana ayuko vizuri kimchezo mara baaday kucheza chini ya kiwango katika mchezo wa klabu bingwa barani ulaya mchezo uliozikutanisha timu ya    Manchester United na Real Madrid 
Mwaka  2003, alishindwa kufika mahabara kwa ajili ya vipimo vya kugundua kama anatumia dawa za kuongeza nguvu au lah ,hali hii ilimtokea pale aliposahau kutokana nakuwa na harakati nyingi za kuhama makazi yake ya zamani nakuhamia makazi mapya na baadae kuendelea na shughuli zake zingine.
 Hali iliyosabaisha kamati ya nidhamu ya chama cha soka nchini Uingereza  FA kumtoza faini ya kutocheza msimu mzima wa ligi na klabu yake kulipa faini ya Pauni 50,000.
Hari ilifanya klabu yake Manchester United kukata rufaa kw amadai ya kuwa ameonewa kwani mchezaji mwengine kutoka Manchester City ,Christian Negouai, alitozwa faini ya Pauni 2,000 kwa kutokwenda kupima.
Ingawa ,Rais wa  FIFA Sepp Blatter alitupilia mbali rufaa hiyo kwa kusema kosa la Ferdinand alifanani na la Negouai ambaye yeye alichelewa kupima kwa sabau ya tatizo la foleni ya magari hivyo alionesha nia ya kutaka kwenda kupima wakti yeye aligoma kwenda kupima kwa sabau zake binafsi nakumuongeze aadhabu ya miezi 12 mingine.  
Ferdinand ambaye aliweza kutwa taji la ubingwa wa ligi ku kwa mara ya kwanza akiwa na klabu ya Manchester United na kupata medali ya   Carling Cup 2006, na kufuatiwa ushidi wa pili katika kipindi cha 2003 na  2005 FA Cup.
Mnamo 14 Desemba  2005, katika mchezo dhidi ya Wigan Athletic, Ferdinand aliweza kushinda bao lake la kwanza akiwa na United , katika mchezo ambao walishinda bao  4–0 . hili lilikuwa goli la kwanza mara baadaya mika mitatu akiwa  Old Trafford.
Baadae akafuatiwa na goli la nguvu la kichwa amabalo alifunga wakati wa mechi dhidi ya   West Bromwich Albion.na baade akafunga bao dakika za mwisho katika mchezo dhidi ya mahasimu wao  Liverpool mchezo uliopigwa katika dimba la  Old Trafford,na ndio lilikuwa goli muhimu kwa United mpaka leo .
Baada ya kuonyesha kiwango kikubwa katika ligi aliweza kuchaguliwa kwenye kikosi bora cha msimu wa ligi kuu ya uingereza cha mwaka  2006–07.
Ferdinand alianza vizuri msimu wa ligi wa  2007–08, kuwa kati ya mabeki wakutegemewa wa Man United ukilinganisha na hap awali alipojiunga na klabu hiyo na kuweza kupachika bao lake la kwanza la msimu katika mechi dhidi ya Aston Vila mchezo uliopigwa,20 Octoba 2007 katika dimba la Vila park.
   
Katika michuano ya  FA Cup mchezo wa robo fainali uliochezwa ,8marchi dhiodi ya Portsmouth, Ferdinand aliweza kukaa golini kma Golikipa baada ya kipa tegemezi wa klabu hiyo Edwin van der Sar kutoka uwanajani mara baada ya kuptwa namajeraha kwani kipindi hicho kipa wa akiba,Tomasz Kuszczak, kufungwa kwa penati na kupelekea kutolewa katika michuano ya FA CUP.
Mnamo  6 April 2008, kweney mchezo dhidi ya Middlesbrough, Ferdinand alitolewa nje kwa matatizo aliyoyapata kwenye mguu . hali hiyo ilimfanya kukosa mchezo war obo fainali ya UEFA ambao ulipigwa 9 april 2008  dhidi ya  A.S. Roma.
Baada ya United' kufungwa bao 2–1 na  Chelsea katika mchezo wa ligi kuu  April 2008 Ferdinand, aliweza kuwa na hasira kutokana na kichapo hicho na kutoamaini kuwa timu hiyo ingeweza kupenya kwenye ukuta wa United  .
Licha ya kuhusishw ana uvumi wa kuhamia klabu ya Barcelona ya nchini ,Hispania  tarehe 16 April 2008 kati ya  Michael Carrick na  Wes Brown, Ferdinand kw apamoja walikubaliana kusaini mkataba mwingine wa miaka mitano kuendelea kucheza United  mkataba amabo uligharimu Pauni milioni 130,000 kwa wiki na mkataba huo utamuweka mchezaji huyo katika timu hiyo ya mashetani wekundu mpaka 2013,mkataba amabao ulisainiwa15 Mei 2008.
Baada ya hapo tarehe  21 Mei 2008, Ferdinand alitajwa kuwa kama nahodha mpya Manchester United  katika mchezo wa klabu bingwa barani ulaya mchezo uliwazikutanisha Manchester United na  Chelsea. Na kufanikiwa kuchukua kombe akiwa na wachzaji wakongwe kama  Ryan Giggs, na  Gary Neville.
Ferdinand ambaye kwa sasa ataweza kuwemo kwenye kikosi cha uingereza kinacho shiriki michuano ya Euro 2012 kutokana kocha mpya wa timu hiyo Roy Hodgson kuhofia timu kushindwa kufanya vizuri katika safu ya nyuma kutokana wailihao kuwa katika ugomvi wa muda mrefu.
Hata hivyo mchezaji huyo ajazungumzia chochote ju ya mahamuzi ya meneja huyo mpya ambaye ameonekana kutegua kiwango hicho.
mwishooo
 
Robin van Persie mkali anayesubiriwa  kwa hamu Man City  

Godlistern Shao na Mashirika ya habari
Mashabiki wengi wa klabu ya  Arsenal wamekuwa wakimuona mshambuliaji wa Klabu hiyo Robin van Persie  kuwa ni mchezaji wa kudumu katika klabu hiyo tangu aliposaini kuchezea klabu hiyo mwaka 2004 na ni mbadala wa mshambuliaji wa kidachi  Dennis Bergkamp ambaye alitandika daluga katika masuala ya soka   
Ingawa mshambuliaji huyo amekuwa akisumbuliwa na majeruhi kadhaa marakwa mara kiasi cha kufanya mshambuliaji huyo kucheza kwa kiwango kilichodhaniwa pindi alipokuwa kijiunga na washika bunduki hao wa London.
Pamoja namatatizo yote  yaliyomkuta mchezaji  van Persie bado ameonekana kuweka mguu wake kuwa ndio biashara pekee katika maisha yake mara baada ya kuwa mshambuliaji wa kutumainiwa peke     yake akichukua nafasi ya Emmanuel Adebayor ambaye aliondoka The Gunners na kwenda kujiunga na Man City.

Robin van Persie amabye ni raia wakidachi alizaliwa Agosti 6,1983 katika Mji wa Rotterdam nchini Uholanzi  ambako ndiko alikulia na maisha yake mpira yalipoanzia.
Van Parse amabye kwa sasa anaicheze kalabu ya Arsenala huku akiwa amebakiza mwaka mmoja kumalizika kwa mkataba wake amekuwa yuko njia panda mraa baada ya Mabingwa wapya wa ligi kuu ya Uingereza Man City kumtangazia dau la kung’oa katika klabu hiyo.
Kabala ya kuchezea Arsenal Van Parsie alipata kuchezea klabu ya Feyenoord ya nchini Uolanzi kwa kipindi cha miaka mine kuanzia 2001 hadi 2004 na baade kujiunga na washika bunduki wa London.

 

Van Persie ambaye alikimbia kutoka kwenye familiya yao amabpo kipindi hicho mama yake alikuwa anafanya kazi ya kupaka rangi na baba yake alikuwa mchongaji wa vinyago huko Uholanzi 
Akiwa na umri wa miaka  14 alijiunga na timu ya vijana ya Uholanzi lakini baade alichwa na timu hiyo kutokana na kushindwa kuelewana na makocha wake na kuendelea kubaki kuichezea klabu yake ya Feyenoord. 
Baadae alionekana kuwa na kiwango cha hari ya juu na kuwa mchezaji wa kuanza katika kikosi cha kwanza cha Feyenoord kutokana na matatizo ya kumia marakwamara yalimfanya awe mtu wa kuanzia kikosi  B.
Ingawa watu wengi waliamini kuwa Van Persie  amegombana na kocha wake  Bert van Marwijk ndio sababu ya kumfanya mchezaji wa akiba katika ,pia kocha aliweza kumrejesha mchezaji huyo nyumbani mara baada ya kuonyesha utovu wa nidhamu katika mchezo wa fainali za UEFA mwaka 2003 dhidi ya Real Madrid. .
 Baada ya kufanikiwa kupachika magoli nane katika msimu wa kwanza huku akitokea benchi aliweza kumshawishi kocha wake katika msimu uliofuata wa mwaka 2003-2004 kuwa ndie mchezaji anayeweza kuanza.
Baada ya kucheza kweney klabu hiyo bil;a kuwa na mafanikio yoyote nyota huyo aliweza kuuzwa katika klabu ya Arsenal ambayo alionyesha kuwa na mapenzi nayo siku za nyuma kabla ya kuuzwa katika klabu hiyo.

 

Mwaka 2004 Van Persie aliweza kusaini mkataba wa miaka mine na klabu ya Arsenal  na kufanikiwa kuwa mmoja wa wachezaji waliocheza katika kikosi kilichochukua kombe la FA mwaka 2005 kombe ambalo alijaweza kuchukuliwa tena na klabau hiyo.

Mara baada ya mkataba wake kumalizika mwaka 2009 mshambuliaji huyo aliweza kumshawishi bosi wake Arsene Wanger kumpa mkataba mpya wa miaka minne  ambao utamalizika mwakani
 Mshambuliaji huyo ambaye aliweza kumfurahisha bosi wake pindi alipokuwa uwanjani kutokana na stairi yake ya mchezo lakini alikuja kujitia doa pale alipopatiw akadi nyekundu kwenye mechi kati ya Arsenal na Southampton.
 Maisha yalibadilika na kuw amtu mwneye furaha akiwa na Gunners pale alipoweza kufunga goli pekee la kichwa na kupewa tuzo kuwa goli pekee la msimu katika ligi kuu ya England.
 Mshambuliaji huyu ambaye alikuwa kaichez anafasi ya winga lakini alicaha jkucheza nafasi hiyo mara baada ya kubadilishwa na kocha wake Arsene Wanger mara baada ya kuona kuwa awezi kufua dafu mbele ya Thierry Henry ambaye alikuwa katika kiwango cha juu sana.
 Licha ya kuwa na mafanikio yote hayo mshambuliaji huyu wa kidachi alionekana kuw ana matatizo ya majeruhi mara kwa mara huku akiwa na tatizo la Goti na henka vitu vilivyo msumbua kila mwezi.

 

Van Persie aliweza kuonyesha uwezo wa hali ya juu katika timu yake ya Tiafa kuanzia mkwa 2006 katika mashindano ya kuwania kufuzu fainali za kombe la Dunia mara baada ya kushinda mechi dhidi ya Roamania na Finland.
Pia aliweza kucheza mechi zote nne katika fainali za kombe la Dunia 2006 kama kiungo wa kutumainiwa wa Uholanzi ,pindi timu hiyo ilipopangwa na timu ngumu kama Argentina na Ivory Coast.    
Miaka miwili badae katika michuano ya Euro 2008, Van Persie alifanikiwa kushinda magoli mawili na kuifanya timu hiyo kutinga atua ya robo fainali kabla ya kutolewa na Urusi.  .
Akiwa anacheza kama winga na mshambuliaji katika timu yake ya Taifa  , Van Persie alioweza kupewa heshima ya hali ya juu na mashabiki wa mpira wan chi hiyo hasa kwa ufundi wake wa kutengeneza magoli akiwa na klabua yake na timu ya Taifa .
Haliweza kuisadia timuyake kutinga hatua ya fainali katika michuano ya kombe la Dunia ya mwaka  2010 kabala ya kufungwa na mabingwa wa kombe hilo kwa sasa Hispania na laiweza kufunga bao moja katika michuano hiyo bao alilofunga kwenye mechi dhini ya Cameroon.
Mchezaji huyu ambaye ameonekana kufanya makubwa katika msimu huu uliomalizika katika ligi kuu ya uingereza kwa kuweza kutwa tuzo ya kiatu cha dhahabu tuzo ambayo ajawahi kuipata maishani mwake.

Van persie ambaye ameweza kufunga mabao 30katika msimu huu na kufikia rekodi iliyowekjwa katika klabu ya Arsenal na mkongwe Thierry Henry msimu wa 2003/04 na pia aliweza kutwa tuzo ya mchezaji bora wa mwaka tuzo inayotolewa na chama cha waandishi wa habari nchini Uingereza.

Hata hivyo yeye ajaonyesha nia ya kuhama klabu yake ya Arsenal licha ya dau nono alilotangaziwa na Man City huku wakala wake akimshawishi kukubalina na hofa hiyo ambayo ni mara tatu ya mkataba wake wa awali.



Sunday, May 13, 2012


HONGERA Taifa Queens kwa Ushindi mliouapata

Na Godlistern Shao

HIVI karibuni mashindano ya mchezo wa mpira wa pete kwa bara la Afrika  yamemalizika hapa nchini  mashindano ambayo yalzikutanisha takribani nchini nane na nchi ya Malawi ikatawazwa kuwa bingwa wa mashindano hayo ikufuatiwa na Tanzania.

Ushindi huo wa Tanzania kushika nafasi ya pili unadhidi kudhiirisha kuwa taifa letu limeweka vipaumble katika umuhimu wa michezo kwa jamii kwa kuenzi historia ya binadamu watanzania nao pia walikuwa wakishiriki katika michezo mbalimbali katika makabila yao.

kwani katika jamii yoyote ambayo imekamilika uwa inaungansishwa na mambo mengi moja wapo ni Michezo, michezo hii inasaidia wananchi kujenga kujiamini na kuwa utambulisho wa jamii fulani.

Kwa bahati mbaya kuna michezo ambayo aikupewa kipaumble katika taifa letu kiasi cha kutishia kupotea licha ya kuwa na masahbiki wengi na kukaa midomoni mwa watu kila siku.

Kwani katika taifa letu michezo ambayo imekuwa mdomoni mwa watu na inayoweza kugawa jinsia mbili tofauti za Me/Ke ni kati ya mchezo wa mpira wa miguu na Netbal.
    .

lakini baadae tukabahatika kuletewa Michezo mingine kutoka mataifa ya magharibi ,mchezo kama  ngumi, mpira wa meza, mpira wa mikono, mbio za baiskeli.

Mchezo wa netiboli ni moja kati ya michezo ilijichuklia umaharufu mkubwa hapa nchini kiasi cha kutwala kwenye michezo mingi ya mashule hapa nchini .

Mchezo huu ambao ulihasisiwa mnao mwaka 1890 nchini England na huchezwa kwa dakika 60 huku nchi za Autralia, New Zealand na England zikitawala kwa kucheza mchezo huo duniani.

Nchini Tanzania mchezo huo wa netiboli uliingia baada ya vita ya kwanza ya dunia wakati Tanzania ilipokuwa chini ya ukoloni wa mwingereza  na mchezo huo kupata umaarufu mkubwa nchini.

Mchezo huu ambao uliingia nchini kwa lengo la kujifurahisha tu hasa watu waliga kutoka kwa wageni makanisani na walimu wa seminari, lakini  baadaye ulianza kuchezwa kwenye shule za msingi na ndiyo maana katika kipindi cha nyuma karibu shule zote za msingi zilikuwa na viwanja vya mchezo wa netiboli.

Pia wachezaji wa timu mbalimbali za netiboli au wachezaji wa timu ya taifa walikuwa wakipatikana kuanzia katika ngazi za chini kabisa hapa nazungumzia kuanzia ngazi ya mashule hadi vyuoni.

Chama cha mchezo wa netiboli Tanzania CHANETA kiliweza kuhasisiwa mnamo mwaka  1966, ambapo mchezo huo ulipata umaarufu mkubwa sana kiasi cha kuwa na mvuto kwa kila mwanadada kutamani kuwa mchezaji mahiri wa netball .

Kipindi hicho ambacho kulikuwa na mashindano mengi ya mchezo huu nchini na kulikuwa na ligi yenye mvuto wa kipekee kwa mashabiki na wachezaji na timu zilikuwa zikishindana katika kiwango cha juu na kuwa na timu kali za netiboli kama Bandari, Posta, Bima na nyingine nyingizilizokuwa zikitamba kipindi hicho.

kuanzia miaka ya tisini  umaarufu wa mchezo wa netiboli nchini ulianza kupotea baada ya kufanyika ubinafsishaji wa mashirika ya umma na kupelekea timu nyingi za mashirika kufa na kupoteza hazina kubwa ya wachezaji wa mchezo huu. .

Hali hiyo ambayo ilikuja na uharibifu mkubwa wa miundo mbinu ya mchezo huo kutokana na kupoteza mvuto kiasi cha wadau kushindwa tena kujitokeza katika kuinua kiwango cha wachezaji chipukizi na hali ya ushindani kwenyeligi ikashuka.

 Hata hivyo hiyo aikuwa sumu ya kutosha kuumaliza mchezo huo kwani uliweza kufufuka tena na kushika kaasi ya ajabu  lakini ulikumbwa na  migogoro katika safu ya uongozi ya chama cha mchezo huo CHANETA.

hata migogoro hiyo amabyo aikuweza kudumu kwa muda mrefu ,ilipotea na bade kujitokeza wadau ambao walijitoa kusaidia mchezo huu kwa hari na mali ,hapa sitosita kumtaja ,Mama Anna Bayi,Anna Kibira ,Da Rose Mkisi na wengine wengi amabo walijifunga kibwebwe kuhakikisha kuwa mchezo huu unarudi katika hadhi yake .

Kwa kufanya hilo CHANETA wameweza kuwa wenyeji wa michuano ya kimataifa mara mbili mfululuzo ,kwa kuandaa michuano ya Afrika amabyo imemelizika hivi karibuni katika uwanja wa Taifa.

Mwishoni mwa mwaka Juzi na serikali ilimleta kocha wa kigeni kutoka Australia, Simone Macknnis kwa ajili ya kufundisha timu ya taifa ya mchezo wa netiboli, lakini aliifundisha kwa miezi michache na kuondoka kwa sababu hakuridhishwa na huduma alizokuwa akipewa.

Lakini hata hivyo mchezo wa netiboli nchini uliendelea kuchezwa na hivi karibuni tumeshuhudia wake wa viongozi wa ngazi za juu serikalini wakijitolea kwa hali na mali kuhamasisha wadau kusaidia timu iweze kuwafanya vizuri katika mashindano ya kimataifa.

Nichukue nafasi hii kuwapongeza Mama Tunu Pinda,Salma Kikwete na Mama Asha Bilal kwa kuweza kuitia hamasa timu yetu na kuweza kushika nafasi ya pili katika mashindano haya makubwa ya kimataifa yaliyofanyika katika Ardhi yetu.

 Licha ya kukosekana kwa wadhamini wa kuendesha mashindano hayo, Chaneta kwa kushirikiana na wadau mbalimbali waliweza kuandaa mashindano hayo ambayo yamemalizika kwa uasalama kabisa bila ya wachezaji kuwa na malalamiko yoyote yale .
 

Na katika kuthibitisha hili timu yetu ya taifa ya Taifa Queens imeweza kutufuta machozi kwa kushika nafasi ya pli katika mashindano ya Afrika huku nafasi ya kwanza ikishikwa na malwai hivyo tunakila sababu ya kuwapongeza dada zetu.
 
Kwa mujibu wa viongozi wa Chaneta mashindano hayo ndio yanayotumika kupanga ni nafasi gani timu inatakiwa kukaa kwenye viwango vya kimataifa .

Chaneta ili weza kupata wachezaji kutoka katika timu za vilabu lakini bado kuna changamoto ya ushiriki mchache wa timu za mtaani kucheza mchezo huo kama ilivyokuwa zamani.

Kwani hata yale mashirika ya umma ambayo yalikuwa yakitoa timu hivi sasa hayana timu tena na badala yake zimebakia timu za majeshi na tasisi chache amabzo zimejifunga kibwebwe kuendeleza mchezo huu.

kwa ustadi huu na kusababisha kuwapo na timu za majeshi nyingi kama ,JKT Mbweni, Jeshi Stars, Hamambe Mbeya, Polisi Dsm, Polisi Arusha, Polisi Mwanza, Polisi Pwani, Tamisemi, Uhamiaji, Magereza, JKT Ruvu, Filbert Bayi na CMTU Dsm.

Timu za Jeshi ambazo kila mwaka zimekuwa mstali wa mbele katika kuonyesha umahiri wake mwaka huu ziliendelea kutoa wachezaji wa timu ya taifa na tumaini la kuwepo timu katika vitongoji vyetu kufutika.

Kwa hili sio la kuilaumu CHANETA,bali ni mfumo wa mitaala uliowekwa katika shule zetu za msingi hadi sekondari kwa kumkosesha motto kupata fursa ya kujifunza michezo .

Timu kama JKT Mbweni ambayo inaongozwa na mfungaji mahiri   Mwanaidi Hassan ambaye ameweza kuwa msaada mkubwa katika timu yetu ya taifa kutokana na umahiri wake wa kufunga magoli na kutumia vizuri mwili wake pindi anapokuwa uwanjani. 

 
Timu kama Filbert Bayi amabyo uwa inaundwa na wanafunzi wa shule ya msingi na sekondari za Filbert Bayi bado aitoshi kuwa timu ya mtaani kuzalisha wachezaji watakaocheza timu ya taifa .

 Hivyo ni vema serikali ikaangalia utaraitibu mwingine wakuhakikisha kuwa mchezo huu unarudi katika nafasi yake kama ilivyokuw awali kwani kuna wachezaji wa kutosha mtaani ambao awajapata fursa.

mwishooo

FID Q mama akupenda niwe mwanamuziki
Na Godlistern Shao
KITU chochote kile kinaweza kuchukuliwa kama kazi ya sanaa, ila inategemea mtazamo wa hadhira ukoje juu ya kitu au kazi husika. Kwa upande mwingine, historia  hasa za jamii au vikundi vya jamii vilivyokuwa na vinavyoendelea kukandamizwa kwa namna moja au nyingine  husema vingine.
Sanaa imekuwa ni mojawapo ya zana zinazotumiwa kufungua macho na fikra za watu kwenye jamii mbalimbali, katika vipindi tofauti. Mfano mzuri ni ndugu zetu wa Afrika Kusini. Wakati wa utawala wa kibaguzi , watu waliokuwa wanaangaliwa kama viongozi walikuwa hawaruhusiwi kukutana au kuongea na mtu zaidi ya mmoja kwa wakati mmoja. Lakini harakati zao hazikugota; waligeukia sanaa  wakatumia kazi za sanaa kuamsha watu.
Kwa hapa nyumbani, historia sio tofauti sana. Wazazi wetu waliokuwa kwenye harakati za kuusaka Uhuru walitumia mpaka ngonjera za mashuleni kuwasilisha sera za TANU, ASP na vyama vingine vya siasa.
Kizazi chetu, cha vijana wa sasa, kina changamoto zake. Na bahati nzuri Fid Q analitambua hilo. Yeye aliamua kutumia sanaa kuwaamsha vijana, tangu alipoingia kwenye Hip Hop takribani miaka 15 iliyopita.
Miaka nenda rudi, anaendelea kufanya anachodhani ni sahihi na inabidi kifanywe. Ametoka mbali.
Tulifanikiwa kulonga naye, na hakusita kuongelea jinsi alivyoanza, kazi zake kwa ujumla na mipango yake ya hapo baadae.
 “Fid Q dot com’ ni wimbo ambao ulinifungulia njia kwa roho safi na kunifanya nipewe heshima iliyoniendeleza mpaka hapa nilipo. Kabla ya ‘Fid Q dot com’ nilitoa ‘Huyu na Yule’ ambayo nilimshirikisha Mr. Paul na Squeezer, nitakuwa mchoyo wa fadhila kama nitasita kusema hii ilinitambulisha vyema kwenye medani ya muziki wetu.
Tofauti iliyopo kati ya ‘dot com’ na ‘Huyu na Yule’ ni kuwa, ‘dot com’ ilikuwa ni kama kitu kipya zaidi masikioni mwa watu, na kitu kipya mara zote husisimua! Ni wimbo ambao nitatumbuiza kwenye tamasha la kesho na kesho kutwa, na bado watu wakaruka nayo utadhani imetoka jana tu.
 Ngoma hii ilinipa, na bado inanipa, heshima kwa wapenzi wa muziki, hata emcees niliowakuta na mpaka waliofuatia ,Ni moja kati ya nyimbo chache ambazo zimebahatika kutochuja, na kama tukisema zinazeeka basi sio vibaya kama nikiifananisha na muwa. Namaanisha, itazeeka na utamu wake”.Alileza Fid Q

Analeza kuwa Siku zote wasanii chipukizi ’ huwaambia wasijaribu kuwa mimi, kwa sababu hata hapa nilipo sipo ninapohitaji kubakia. Na kinachonifanya niendelee kuwepo ni kile kiburi changu cha kutohofia kupitwa ilimradi muda usiniache.
“Na pia Paul Robeson ameshawahi kunena haya: “Sanaa kazi yake si kuonesha tu hali ya dunia ilivyo sasa tu; bali inavyopaswa kuwa na itakavyokuwa baadae.”
Sababu hiyo ya msingi imempelekea kuamini ya kwamba wanamuziki na wasanii wote kwa ujumla tuna jukumu la kuwa wajenzi wa  kesho njema kuliko hata wanaotutawala.
 Anaweka wazi kuwa  mama yake  hakupenda awe mwanamuziki. Na alipopata ruksa ya kutembelea studio alikutana na vikwazo ambavyo kila msanii anayefanya hip hop yenyewe lazima atakuwa ameshakutana navyo.
Vikwazo hivyo ni pamoja na kuambiwa apunguze ukali wa maneno au kufanya mashairi mepesi yasiyoumiza vichwa vya wasikilizaji’.
Kwa kweli, kwa kupitia vipingamizi hivi, vimfanya kujifunza uandishi fulani hivi. Yaani kwa mfano hata kama anakosoa jambo fulani, hatahakikisha linaruka kwa kasi ya kifaru aliyejeruiwa lakini linatua kiulaini kama sponji.
Ndio maana anaweza kutoka na ngoma inayoongelea matatizo na bado watu wakaiimba na kucheza wakiwa vilabuni na kwenye madisko mbalimbali.

Anasema kuwa moja ya vitu ambavyo vilimtia moyo aendelee kufanya mziki siku aliyosikia mama yake mzazi akisema anaipenda nyimbo yake ya  ‘Usinikubali Haraka’  na kumlazimu atenge masaa matatu ya kujiuliza alifikiria nini mpaka akaandika ule wimbo.Na pili, je ni kweli mama yangu kaliona hilo?
“ Unajua siku zote unapofanya kazi yenye malengo ya kuigusa dunia, huwa inafikia kipindi ile dunia nayo huwa inataka kukugusa wewe mhusika mkuu. Fid Q ni msanii kama wasanii wengine, hivyo na mimi huwa nakutana na mikasa mbalimbali katika maisha, lakini pale linapokuja suala la kutafuta mwenza wa kuishi naye kwenye raha na shida, ndipo huwa najikuta  nina kuwa mzito”
 Na kueleza kuwa watu wengi upenda  kuwa na tabia ya kuhukumu vitu kama tulivyo na sio kama vilivyo, hivyo basi amegundua hiyo tabia ipo kwenye mapenzi pia.
 Na kusema kuwa mtu upendwa kwa kile alichokuwa nacho na sio yeye kama yeye na hicho kinapelekea wapendanao wengi kuuziana kanyaboya. Na kunipa  msemo wa haraka haraka haina baraka, ili muda zaidi upate kutengwa kwa ajili ya kitu chenye manufaa.
Wimbo wake wa pili anaoupenda  ni Propaganda… wazo lilomjia baada ya kughairi kutoka na Darwin’s Naitmea  na alifurahishwa na jinsi alivyoweza kucheza karibu na mada ya kwanza kabisa.

Wa tatu ni Fei. “Ukiusikiliza vizuri utagundua upendo nilionao juu ya mwanangu, na pia historia fupi ya mahusiano yaliyopo kati yangu na baba yangu mzazi.”

Aliweka wazi Maslahi ndio kitu pekee kinachowaumiza watu wengi lakini  hipo siku watu watatambua nini wanatakiw akufanya katika muziki wa hippop hapa nchini .Miaka kumi ijayo hip hop ya Bongo itakuwa kubwa zaidi ya vile ilivyo hivi sasa, na ningependa ipewe kipaumbele zaidi kwa sababu ni hii hii hip hop ndio ina uwezo wa kupunguza au kuondoa ujinga kwa asilimia 50 au hata 70, kama wanafunzi walioko mashuleni wataendelea kulega kwenye masomo yao ya kila siku.

Fid Q ambaye ameonekana kuwa na taswira tofauti ya swala la msanii kuw anaalbamu na kueleza kuwa  albamu kwake  huwa naichukulia kama “audio book”… Yaani sio suala la kukusanya nyimbo  tu kupeleka kwa sokoni kwa mashabiki .
Na kusema kuwa hali hiyo inatokea mara nyingi sana ; unakuta mtu anatoka na albumu, ngoma ya kwanza inasema ‘Umeniacha’, ya pili ‘Sikutaki Tena’ ya tatu ‘Nataka Mpenzi’, ya nne ‘Unanichosha’. Halafu unakuta album labda inaitwa ‘Toba’.
 KitaaOLOJIA ni albamu mpya ya Fid Q ambayo imekusanya kuanzia album ya kwanza ambayo ni ‘Vina Mwanzo Kati na Mwisho’ na ya pili ambayo ni ‘Propaganda’, sasa Kitaa inakuja kukamilisha ule uprofesa wake wa chuo kikuu cha ghetto, kwa kuwaletea simulizi na mafunzo niliyokutana nayo mitaani… kwa kupitia mambo yaliyompata uzoefu katika maisha yake binafsi.
Alabamu ambayo anatarajia kuipakua Augosti 13 mwaka huu na kusema soko la bongo liko tayari kuipokea na lishakaa mkao wa kula kwa ajili ya albamu hiyo.
 Fid Q ambaye ameamua kuja kivingine katika kuhakikisha kuwa mziki wa Hippop unakuwa kwa kuandaa kipindi cha televisheni kitakacho tambulika kama FidStlye Friday .
Anaeleza kuwa FidStyle Friday itaanza kurushwa kwenye kituo kimoja cha televisheni hapa nyumbani. Na pia yupo katika maongezi na mmiliki mmoja wa televisheni ya kujitegemea iliyopo nchini Ujerumani kwa kuwa hata na wao wamevutiwa na yaliyomo kwenye FidStyle Friday.
Halikadhalika alitoa wito kwa mashabiki waendelee kusikiliza kwa umakini, wawe wadadisi ikiwezekana wafanye utafiti wa kila kauli itakayowavutia kwenye tungo za hip hop kwa sababu hiyo ndio njia pekee ya kuelewa uwezo wa msanii.
Anaeleza kuwa  yeye ni mshabiki namba moja wa Prof. J… Mpaka leo bado anajivunia kununua ile album yake ya ‘Machozi, Jasho na Damu Huwa haimchoshi kuisikiliza na ameridhika nayo kabisa. Kiasi kwamba huwa aoni kama jamaa anakosea kwa kunata kwenye midundo ya kapuka na mingineyo.
 Msanii mwingine ni Hasheem Dogo. Nikki Mbishi Mc pekee ambaye anamshangaza kila siku kwa ubunifu wake, na One The Incredible,kwa matumizi yaek ya Kiswahili fasaha na ule uandishi wake wa kugushi kushoto kisha anaelekea kulia mwingine ni  Stereo pamoja na Jay Mo.  


Sunday, May 6, 2012

WAVESHWA MATAJI MISS USTAWI

HUMPHREY SHAO
Duly Sykes AKIPAGAWISHA MASHABIKI WALIOFIKA KWENYE SHOO
HUMPHREYSHAO
 WADAU KADHAA WALIOFIKA SIKU YA SHOO WAKIJIACHIA KWENYE DANCING FLOO
HUMPHREYSHAO
 MREMBO NDENENSIAH MBOWE ALIYECHUKUA NAFASI YA TATU AKIVISHWA TAJI NA ALIYEKUWA MISS USTAWI NAMBA TATU MWAKA JANA
HUMPHREY SHAO
 MWENDOWA PHOTO SHOOT WAREMBO WATATU WAKATIKAKTI HILDA,NANCY NA NDENENSIAH
HUMPHREY SHAO
HUMPHREY SHAO
 NANCY AKIPOKEA CHEKI YAKE YA SHILINGI LAKI TATU KAMA MSHINDI WA PILI
HUMPHREY SHAO
 BURUDANI TU NA MASMILE
HUMPHREY SHAO
 NDENENSIAH MBOWE AKIPOKEA HUNDI YAKE YA SHILINGI LAKI MBILI KAMA MSHINDI WA PILI
HUMPHREY SHAO
 MKURUGENZI WA JIRUSHEWEEKEND HUMPHREY SHAO KATIKA PICHA YA PAMOJA NA MREMBO NDENENSIAH MBOWE AMBAYE NI MKURUGENZI MSAIDIZI WA JIRUSHEWEEKEND

HILDA AKIKABIDHIW AZAWADI YAKE YA LAPTOP NA MGENI RASMI


HILDA NDIYE RED'S MISS USTAWI 2012

 MUIGIZAJI MKONGWE KWENYE TASNIA YA BONGO MUVI ,SINTA A.K.A J LO WA BONGO AKIWA NA WANAKAMATI KUJADILI MSTAKABALI WA SHUGHULI WAKATI REASOL
 WATU KADHAA AMBAO NI WANAFUNZI WA CHUO CHA USTAWI WAKILA BATA KUSUBILI MCHAKATO WA SHINDANO LA RED'S MISS USTAWI
 DULLY SYKES BABA TORIANO AKITOA SHOO WAKATI WA SHINDANO
 MAJAJI WA SIKU HIYO WANA HABARI ALFRED LUCAS ,VICKY KIMARO NA JAMES RANGE WAKICHAKALIKA KUJUMLISHA MATOKEO
MKURUGENZI WA JIRUSHEWEEKEND BLOG HUMPHREY SHAO AMABAYE AMEVAA SHATI LA BLUU AKIWA NA WADAU WENGINE KUTOKA USTAWI WAKIFATILIA SHOO KWA UMAKINI MKUBWA.

Thursday, May 3, 2012

AND 1 ilivyowakuna wabongo last week





GRAND MALT YAZINDUA TUZO ZA “EXCEL WITH GRAND MALT 2012”.

Kinywaji maarufu cha Grand Malt leo kimezindua tuzo kwa wanafunzi wa elimu ya juu zijulikanazo kama “Excel with Grand Malt”, huu ukiwa ni mwaka wa pili kwa tuzo hizi kutolewa.

Akizungumzia tuzo hizo, meneja wa kinywaji cha Grand Malt Bi. Consolata Adam alisema; Excel with Grand Malt ni tuzo za aina yake ambazo zimelenga kutambua na kuthamini mchango wanaoonesha wanafunzi katika fani mbalimbali nje ya masomo ya darasani. Tunatambua kuwa kazi kubwa ya mwanafunzi anapokuwa chuoni ni kuhudhuria vipindi vya darasani na kupata elimu, bali tunapenda pia kuwatambua wale wachache ambao wanakwenda mbali zaidi na kufanya mambo ya maendeleo katika mazingira yao ya chuo.

Tuzo hizi zilianzishwa mwaka jana ambapo tuliweza kufika katika mikoa sita na kufikia vyuo vipatavyo ishirini. Kwa mwaka huu mchakato utaanza mwezi Aprili hadi June, na Mikoa itakayohusika ni pamoja na Dar es salaam, Morogoro, Iringa, Dodoma, Kilimanjaro na Mwanza ambapo vyuo vipatavyo 21 vitashiriki. Kama ilivyokuwa mwaka jana, fani zitakazoshindanishwa ni Ubunifu (Innovation), Michezo (sports), Utamaduni na burudani (Culture & Entertainment) na Mazingira na Huduma za jamii (Environment & social responsibilities). Kama ilivyo ada, washindi katika fani hizi watajipatia zawadi mbalimbali toka Grand Malt ikiwa ni pamoja na pesa za kununulia vitabu na vyeti vya ushindi.

Kwa sasa natangaza rasmi kuwa tunzo hizi zimezinduliwa rasmi na mkoa wa kwanza utakuwa ni Morogoro ambapo tunatarajia kufanya tamasha kubwa kwenye viwanja vya chuo kikuu cha SUA siku ya jumamosi kisha jumapili tutafanya tamasha la ufunguzi kwenye Viwanja vya chuo cha CBE mkoani Dodoma na kutakuwa na burudani zitakazoongozwa na nguli wa Hip hop nchini Joh Makini ,zawadi nyingi na zaidi kutakuwa na GrandMalt baridi na hakutakuwa na kiingilio chochote. Alisema Bi. Consolata.

Akielezea umuhimu wa Tuzo hizo, meneja masoko wa TBL Bw. Fimbo Butallah alisema; Tunafurahi sana kuona vyuo vyote vilipokea tuzo hizi kwa furaha kubwa, hii ni kwa sababu wanatambua umuhimu wake. Kupitia tuzo hizi ambazo zitakuwa zikitolewa kila mwaka, Grand Malt inatoa changamoto kwa vijana walio vyuoni kuona umuhimu wa kujituma na kufanya mambo mengi na makubwa zaidi ya kufaulu mitihani ya darasani tu. Tunaomba viongozi wa serikali za wanafunzi na viongozi wa vyuo kuendelea kutoa ushirikiano kama walivyofanya mwaka jana ili kuleta ufanisi zaidi katika tuzo za mwaka huu. Kama ilivyo kawaida, utaratibu utakuwa ule ule ambapo wanchuo watapendekeza majina ya vijana wanaoamini kuwa wamefanya mambo makubwa ndani ya vyuo vyao katika tasnia zilizotajwa hapo awali, kisha kufuatiwa na kipindi cha kupiga kura ambapo washindi watapatikana. Alimaliza Bw. Butallah

Kwa upande wake meneja mahusiano na mawasiliano wa Tbl Bi Edith Mushi Alisema GrandMalt kwa kuzingatia umuhimu wa juhudi za serikali katika kuhamasisha jamii kutunza mazingira kwa kupanda miti mwaka huu Grand Malt itafanya zoezi maalum kwenye kila chuo kwa kupanda miti imara itakayosaidia kutunza na kuboresha mazingira ya vyuo hivyo ili kuandaa mazingira bora ya kusomea ya wanafunzi wa sasa na wa vizazi vijavyo ambapo mkoani Dodoma zoezi hilo litafanyika jumatatu May 07,2012 katika vyuo vya UDOM na CBE tawi la Dodoma na Mkoani Morogoro zoezi hilo litafanyika kwenye vyuo vya SUA na Mzumbe siku ya jumanne May 08,2012 asubuhi, kisho zoezi hilo litaendelea katika mikoa ya Iringa,kilimanjaro,Mwanza na Dar Es Salaam.

Wednesday, May 2, 2012

Eleven killed in Egypt clashes over army rule



 Photo



CAIRO (Reuters) - Eleven people were killed and more than 160 wounded near Egypt's Defence Ministry on Wednesday after armed men assaulted protesters demanding an end to army rule, prompting two Islamist candidates to suspend their presidential election campaigns.
Unidentified "thugs" armed with guns or batons attacked demonstrators who included hundreds of ultraconservative Salafi Islamists protesting at the exclusion of their candidate from this month's vote, state news agency MENA reported.
The violence casts a deep shadow over the presidential election due on May 23 and 24, with a run-off in June, and highlights the fragility of Egypt's transition to democracy, which has been punctuated by violence and political bickering.
Security and medical sources gave a toll of 11 dead and over 160 wounded in the clashes outside the Defence Ministry in central Cairo's Abbasiya district. The fighting raged on unabated through the morning, but subsided in the afternoon.
"Where is the army? Why are they not stopping these people?" cried a bystander as the violence persisted. Shots rang out as young men dashed back and forth across debris-scattered streets, hurling rocks, glass and petrol bombs.
"Down, down with military rule," yelled protesters.
Wounded men were hauled away as others filled bottles with petrol while shots rang out. A Reuters witness saw some combatants carrying guns and one with a sword.
The army sent in extra vehicles and troops, but pledged in a statement not to disperse peaceful demonstrators.   Continued...

SERIKALI YATAKIWA KUACHA KUINGILIAKAZI ZA TUME YA KATIBA


SERIKALI imetakiwa kuacha kuiingilia kazi za Tume ya Mabadiliko ya Katiba na badala yake iwape uhuru wa kufanyakazi hiyo kwa ufasaha na kuandaa katiba wanayoitaka wananchi.

Hayo yamesemwa jana na Mwenyekiti wa Tume hiyo, Jaji Joseph Sinde Warioba wakati wa uzinduzi wa tume hiyo na kukabidhiwa jengo la kufanyia kazi hiyo.

Mwenyekiti huyo amesema isije ikafika wakati tume ikashindwa kufanyakazi ipasavyo kwa sababu ya maslahi ya watu wachache kwani kufanya hivyo itakuwa ni kuingilia uhuru wa tume na kuwanyima haki wananchi ya kupendekeza katiba waipendayo.

“ Nyie mliotuchagua tunaomba tafadhari mtupe nafasi isije ikaja leo au kesho mnaanza kutusumbua tupindishe kilichopo kwa madai mna watu wenu ndani ya tume naomba ieleweke kuwa tume si ya kikundi fulani ni ya wananchi  hivyo hatutaki kufanyakazi kwa presha ya watu fulani,”amesema Warioba.

Amesema kazi waliyopewa ni ngumu hivyo wana imani serikali itawapa ushirikiano wa kuwafikia wananchi wote ili waweze kutoa maamuzi yao na kuandaa katiba yenye maslahi ya umma.

Kwa upande wake Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue amesema Serikali imeandaa mazingira safi ya kuhakikisha tume hiyo inafanyakazi kwa ufanisi zaidi.

Amesema  kuwa serikali imetekeleza ahadi aliyoitoa rais alipoiapisha tume hiyo Aprili 13 mwaka huu ya kuhakikisha tume hiyo inafanyakazi kwenye mazingira stahiki yenye ulinzi wa kutosha, usalama , na vifaa vya mawasiliano na vya kutunzia kumbukumbu vya kisasa.

Pia serikali imenunua magari 30, kwa ajili ya tume hiyo ili kuweza kuwafikia wananchi kwa urahisi na kuepuka vikwazo katika utendaji wa kazi hiyo na fungu maalum la fedha limetengwa..

“ Serikali imedhamiria kuipa uhuru tume, kuwapa sehemu nzuri ya kufanyiakazi pamoja na nyumba za kuishi wana tume ambao wanatoka nje ya Dar es Salaam,”amesema Sefue.

Naye Waziri wa Katiba na Sheria, Cellina Kombani  amesema umuhimu wa mabadiliko ya katiba ya nchi ni mkubwa na wananchi wana matumaini na tume na ndiyo maana ilipotangazwa hakuna malalamiko yaliyojitokeza.

Ameitaka tume hiyo ijipange vyema ili kuhakikisha inatoa elimu ya katiba iliyopo ili wananchi waweze kutoa maoni ya katiba waipendayo kwani muundo wa katiba hiyo ni jambo nyeti na lenye kuleta msisimuko.

“ Nina imani amani  itatawala na uwazi, kwani mchakato huu ni wa kuboreha mazuri, kuondoa mapungufu pia ni kujipima tulikotoka na tuendako kwani nia si kuvunja umoja wetu bali mawazo ya wananchi yataheshimiwa, “amesema Kombani.

Kombani ameongeza kuwa tume hiyo ndiyo nguzo ya mchakato wa katiba mpya huku akisisitiza kufanikiwa au kutofanikiwa kutatokana na tume hiyo kutekeleza majukumu yao kwa kuwashirikisha wananchi bila ubaguzi.

“ Kazi hii inahitaji ushirikiano zaidi nafahamu kuna kipindi mtakwazika na kutamani kuimbia kazi hii lakini mkiwashirikisha wananchi mtafikia muafaka na hatimaye tutapata katiba inayostahili,”amesema Kombani.


Wakati huohuo, Waziri wa Katiba na Sheria Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Abubakari Khamis Bakari amesema tume imepewa kazi ngumu ya kuwaelimisha wananchi kwani wengi wao hawajui maana ya muungano.

Amesema ili katiba iwe yenye kukidhi haja ni muhimu wananchi wakapewa fursa ya kutoa maoni ambayo yataisaidia tume hiyo  kurahisisha kazi yao.


Amewatahadharisha wananchi kuacha kutumia mchakato huo kama njia ya kuibomoa nchi  na badala yake fursa hiyo itumike kuunda katiba yenye mantiki na inayokubaliwa na watu wote.

Hata hivyo hafla hiyo iliingiliwa na dosari baada ya jenereta lililopo jirani na jengo hilo kulipuka jana asubuhi na kusababisha umeme katika jengo hilo kukatika  hivyo kufanya hafla hiyo kuendeshwa bila vipaza sauti.

mwisho

BOXING   MAWE   NGUMI
V/S   
JAMES MOKIWA V/S RAMA KUMBELE
UBINGWA WA T.P.B.O
MAPAMBANO YOTE NI KAMA IFUATAVYO;-

RAMADHAN KUMBELE(DAVIS CORNER-TANDIKA) v/s JAMES MOKIWA(CHICHI MAWE GYM

KARIM SALUM”paquiao” v/s ANORD YOHANA”biggie’(CHICHI MAWE GYM)

DOI MIYEYUSHO(CHICHI MAWE GYM) v/s JUMANNE MTENGELA (MABIBO GYM)

JAFAR MAJIA”mr nice” v/s DAUD MUHUNZI (MSISIRI GYM)
DOTO KIPACHA  V/S  JOSEPH RICHARD
FRANCIS SUBA v/s JOSEPH PITER”mbowe’-(MKONO WA CHUMA)

SADAT MIYEYUSHO(CHICHI MAWE GYM) v/s SWEDI HASSAN(dame gym-nomo camp)

                                             MARTIN RICHARD(BigRight Boxing) v/s YOHANA THOBIAS(CHICHI MAWE GYM

HEAVY WEIGHT
ANORD "BIGGIE V/S KARIM "PAQUIAO"KIINGILIO;
KAWAIDA TSH 4,000/=
VITI MAALUM TSH 6,000/=JUMAPILI kuanzia saa 10jioni.20/5/2012 VIJANA HALL-KINONDONINJOO USHUHUDIE MAWE YA NGUVU MABONDIA WAMEJIANDAA VYA KUTOSHA NA WAMEAHIDI LAZIMA MTU ALALE.
PIA KUTAKUWA NA MAONESHO YA WAJASILIAMALI,ASASI ZA KIJAMII NA KIUCHUMI ZITAKUWEPO KUELEZEA KAZI ZAO
V/S   
V/S   
KUTAKUWEPO NA PROJECTOR ITAKAYOONESHA MAPAMBANO YA FRANCIS MIYEYUSHO
YAKIWEMO NA MBWANA MATUMLA i,ii & iii NA MENGINE YA HAPA NA ULAYA
V/S