Thursday, November 14, 2013

Mlinzi wa kagame mbaroni



Mlinzi wa kagame mbaroni

ALIYEKUWA mlinzi mkuu (bodyguard) wa Raisi wa Rwanda, Paul Kagame, Luteni Joel Mutabazi, ametekwa na kikosi cha jeshi la Uganda na kukabidhiwa kwa Serikali ya Rwanda.

Taarifa za Kiitelejensia zinasema kuwa Luteni Mutabazi ambaye alikuwa akiishi nchini Uganda kwa hati maalumu ya ukimbizi ya Umoja wa Mataifa baada ya kutoroka nchini Rwanda pamoja na aliyekuwa Mkuu wa Majeshi ya nchi hiyo, Faustin Kayumba Nyamwasa.

Luteni Mutabazi alitorokea nchini Uganda Oktoba 2011, baada ya kutoroka jela yenye ulinzi mkali ya kijeshi ya Kami nje ya Mji wa Kigali akishutumiwa akihusishwa na kutoroka kwa mkuu huyo wa majeshi na kukimbilia Afrika Kusini. Alikuwa mlinzi mkuu wa Rais Kagame mpaka mwaka 2010 alipotoroka na kukimbilia Uganda.
Mlinzi huyo pia anashutumiwa na Serikali ya Rwanda kwa kutoa siri kwa Kikosi Maalumu cha Umoja wa Mataifa chini ya Majeshi ya Umoja ya Kulinda Amani Kongo, (MONUSCO) na kuwezesha kuchakazwa na kushindwa kwa kikosi cha M23.

Tayari Serikali ya Uganda imemsimamisha kazi Mkuu wa Intelejensia katika jeshi la Polisi, Joel Aguma, ambaye alihusika ka kumteka na kumkabidhi Luteni Mutabazi kwa Serikali ya Rwanda kwa kutii amri ya Rwanda kwa kukubali hati ya kimataifa ya kukamatwa kwa mlinzi huyo.

Tayari Serikali ya Rwanda imekiri kumkamata Luteni Mutabazi na kuzuiliwa katika jela maalumu ya kijeshi ya nchi hiyo mjini Kigali.

Msemaji wa Polisi wa Rwanda, Damas Gatare amesema kuwa huu ni mpango endelevu wa Rwanda na Uganda wa kukabiliana na maasi na majasusi kutoka sehemu mbali mbali duniani na kuwa sheria itachukua mkondo wake.

Serikali ya Rwanda imesema kuwa Luteni Mutabazi atashitakiwa kwa kosa la ujasusi na uhaini na kuwa hakuna mtu yoyote nchini humo ambaye atafanikiwa kutoroka mkono wa sheria na kuwa itaendelea kuwasaka na kuwarejesha nchini wahalifu wote kutoka nchin hiyo.

Mkuu wa Polisi wa Uganda aliyesimamishwa kazi na ambaye amehusika katika utekaji na kumrudisha Rwanda, Luteni Mutabazi alirudi Uganda Oktoba mwaka huu, baada ya kuhudhuria kozi ya mwaka mmoja ya makamanda katika chuo cha Polisi cha Rwanda na kuibuka kuwa mwanafunzi bora katika kozi hiyo.

Mlinzi huyo alitekwa Agosti 20, mwaka huu, saa 11 jioni kutoka hotelini kwake ambapo alikuwa anataka Skype  na kumfanya atoke chumbani kwake na kwenda sebuleni ili aweze kupata wireless internet.

Ghafla makomando watano wa jeshi la Rwanda wakiwa na bunduki za AK47 walimvamia na aliweza kupigana nao kwa muda mrefu na kuwafanya makomando hao kushindwa kumkamata kutokana na uzoefu wake wa kikomandoo.
Baada ya makomando hao wa Rwanda kupata kipigo walitoa ishara kwa wenzao ambao walikuwa katika gari lililopaki chini na kuja kuwasaidia na kuwafanya makomando wenye nguvu zaidi watatu zaidi kwenda kuwasaidia wenzao na kumuwekea kitambaa chenye dawa na kumbeba na kumuingiza kwenye gari.

Habari za Kiitelejensia zinasema kuwa Mutabazi alichukuliwa na gari lenye nambari UAK 551B na kukimbizwa hadi mpakani na kukabidhiwa kwa serikali ya Rwanda.

MWISHO



Na Jennifer Ullembo

MSANII wa muziki wa kizazi kipya, Omary Nyembo ‘Ommy Dimpoz’, anatarajia kuachia albamu yake ya kwanza, Januari au Februari mwakani.

Akizungumza na Rai jana, msanii huyo alisema, albamu hiyo ni ya kwanza tangu, alipoanza kujihusisha na masuala ya muziki wa bongo fleva.

Alisema albamu hiyo itakuwa na nyimbo 10, huku nyimbo zake zote zilizoweza kutamba na kumtambulisha zikiwa ndani yake.

“Nilianza na Nainai, hata zile zilizofatia na hizi za sasa hivi, zitakuwemo kwenye albamu yangu hii, mpya mbayo ni mara kwanza kuachia kwa kipindi kirefu,”alisema Ommy Dimpoz.

Msanii huyo alisema, anatarajia kumuachia jukumu la kutafuta jina la albamu, meneja wake Mubenga, ambapo kama albamu hiyo itachelewa haitavuka siku ya Valentine mwakani.


Na Jennifer Ullembo

MSANII wa muziki wa kizazi kipya,  Sunday Mangu ‘Linex’, anatarajia kutambulisha, msanii mpya  ambaye ametokea, kwenye kundi lake la Sauti za Afrika ‘VOA’.

Akizungumza na Rai jana, Linex alisema, msanii huyo atajulikana kama Ssen Lubi na tayari amefanikiwa kufanya wimbo wake, alioupa jina la ‘Kiroho Safi’.

Linex alisema, Lubi ni msanii mpya , ambaye amekuzwa na kupewa mafunzo zaidi, kupitia kundi lao la VOA.

“Msanii huyu ni mpya, najivunia kuvumbua kipaji hichi, anatarajia kuachia wimbo wake mpya wa Kiroho Safi, ambao amemshirikisha Chege Chigunda,”alisema Linex.
  
 Msanii huyo alisema, anaowamba wadau wa muziki kukipokea kipaji kipya, huku akihahidi kuendelea kuibua vipaji vya wasanii wengine wachanga.

Na Jennifer Ullembo
WASANII wa muziki wa kizazi kipya, Chege Chugunda ‘Chege’ na  ‘Temba’, wanatarajia kuachia wimbo wao mpya, uliopewa jina la ‘Kama Kasuku’.

Akizungumza na Rai jana, mmoja wa wasanii hao Chege, alisema kuwa tayari wameingia studio juzi, kuandaa kazi hiyo inayotarajiwa kuachiwa, kabla ya kumalizika kwa mwaka.

Chege alisema, ushirikiano ambao wamekuwa, wakiufanya kwa pamoja na Temba, umeweza kuwaongezea umaarufu zaidi, kwenye kazi zao.

“Tumepanga kumaliza mwaka huu, kwa kuachia wimbo wetu mpya wa Kama Kasuku, mashabiki wajiande kusikia kazi nzuri kutoka kwetu,”alisema Chege.

Msanii huyo aliendelea kusema, mbali na kuachia kazi hiyo ya Kama Kasuku, wanatarajia kufanya shoo mbalimbali za mwisho wa mwaka, ambapo tayari wameanza kupokea  maombi kutoka kwa mashabiki.

MAKAMU WA RAIS GHARIB BILAL NA JAJI MANETO WATO POLE KATIKAMSIBA WA DK MVUNGI






UMASKINI BADO TATIZO NCHINI



ufunguzi kil maathon









Mbunge wa Temeke Abasi Mtemvu akabidhiwa Tuzo ya Heshima na Dk Rahabu Mgunduzi wa Dawa ya Fitarawa

 Mtemvu akiwa na Dk Rahabu pamoja na Catherine Kahabi


 Mtevu na Dk Rahabu


 mtemvu akikabidhiwa tuzo yake






Roverr Community showcase the talents of Sober House art programs both from Zanzibar and Tanzania Mainland

 Abdalahman Abdalah Chair man akionyesha bahadhi ya kazi zilizofanyw ana vijana walio acha uteja.
 Mrembo huyu ambaye alikuwa Nesi kisha kujiingiza katika Dawa za kulevya
 Kucos mtaalamu wa michoro na ufinyangaji akiw ana kinyago chakecha malezi ya mama na mtoto
 computer akiwa katika kazi za kinadada