Saturday, January 25, 2014

MCEZAJI BORA WA TENISI ALIYENIVUTIA KATIKA MASHINDANOYA WATOTO


Dk. Ali Shein kumnadi mgombea Kiembesamaki

Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Kiembesamaki-Januari 26.
Dk. Ali Mohamed Shein, atakuwa mgeni rasmi na kumandi Mahomoud Thabit Kombo


Dk. Ali Shein kumnadi mgombea Kiembesamaki
Na Andrew Chale, Zanzibar
MAKAMO Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar ambaye pia ni Rais wa Serikali ya Mapinduzi,  Dk. Ali Mohammed Shein  kesho Januari 26, anatrajiwa kumnadi mgombea wa Uwakilishi wa jimbo la Kiembesamaki, Mahmoud Thabit Kombo, katika uchaguzi mdogo unaoendelea kwenye jimbo hilo.
Katika tarifa yake, Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Vuai Ali Vuai alisema kuwa, Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar,  Dk Shein atakuwa mgeni rasmi kwenye mkutano huo wa nne wa hadhara kwenye kampeni hizo zinazoendelea.
Na kuongeza kuwa, Dk. Shein atawahutubia wananchi sambamba na kumnadi, Mgombea huyo wa nafasi ya uwakilishi, Mahmoud Thabit Kombo, anayewania nafasi hiyo kwenye jimbo hilo la Kiembesamaki.
Vuai aliwataka wananchi wa jimbo hilo kujitokeza kwa wingi ilikusikiliza sera na ilani za chama hicho katika utekelezaji wake iliwakichague chama cha Mapinduzi kwa misingi imara ya kuwaletea maendeleo.
Aidha, kwa upande wake,  Mahmoud Thabit Kombo aliwaomba wananchi wa jimbo hilo, kumpigia kura hiyo Februari mbili, ili akawawakilishe kwenye Baraza la Wawakilishi.
“Nawaomba Wanakiembesamaki, kutumia fursa ya kipekee ya kunichagua ilikuweza kuwawakilisha kwenye BAraza, hakika  chama chetu ni sikivu na daima kipo na wananchi katika kuwatetea na kuwaletea maendeleo” alisema, Mahmoud.
Kampeni za uchaguzi mdogo wa jimbo la Kiembesamaki, zilianza Januari 21, ambapo zinatarajia kumalizika Februari Mosi, mwaka huu huku wananchi wakitarajia kupiga kura ya chaguzi huo, Februari mbili.
Mwisho



YANGA YAISULUBU ASHANTI BAO 2-1







Thursday, January 23, 2014

EU YAPIGA JEKI WATOTO TANZANIA

 EU1: Mkuu wa Ushirikiano kutoka Umoja wa Nchi za Ulaya Tanzania Eric Beaume (kushoto) akibadilishana hati ya makubaliano ya Mradi wa Kupambana na Ukatili kwa Watoto  na Mwakilishi wa UNICEF hapa nchini Jama Gulaid, kutoka kushoto ni Mkurugenzi Mkazi wa Plan International Tanzania Jorgen Haldorsen, Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dkt. Seif Rashid na Mkurugenzi Mkazi wa Save the Children International Tanzania Steve Thome wakishuhudia makabidhiano ya hati hiyo jana jijini Dar es Salaam
U4: Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dkt Seif Rashid (aliyeko mstari wa mbele katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Wadau wa Mradi wa kutokomeza Ukatili kwa Watoto mara baada ya kutia saini msaada kutoka Umoja wa nchi za Ulaya jana jijini Dar es Salaam.

MKUTANO MKUU WA NGUMI ZA KULIPWA

MKUTANO   MKUU  WA  NGUMI   ZA  KULIPWA

Siku ya terehe 1 ya mwezi wa pili katika ukumbi wa vijana hall kinondoni KUANZIA SAA TATU NA NUSU ,kutakuwepo na mkutano mkubwa wa wanamasumbwi wote ulioitishwa na orgnaizesheni ya ngumiza kulipwa Tanzania (TPBO) kwa lengo la kuwakutanisha mapromota wote,mabondia na makocha  wa ngumi wote kwa lengo la kujadili ngumi za kulipwa zinapoelekewa,kujuana na kuelimishana sheria za ngumi za kulipwa  zinavyotumika kinyume na sasa ,sheria nyingi zinafungiwa macho na kutumia uzoefu zaidi kuendesha mgumi nchini.  Mkutano huo ulioitishwa na Rais wa TPBO bw  Yasin Abdallah akishirikiana  na Ibrahim kamwe na Mapromota wa ngumi chini ya ufadhili wa kitwe Traders unatarajiwa  kuwa mkutano wa kwanza  kuwakutanisha mapromota wote pamoja na  mabondia wa ngumi  za kulipwa wa hapa nchini ili kuboresha ngumi na kuhamasisha wadhamini na makampuni wajitokeze kuudhamini mchezo huo ,ambao ndio mchezo unaoliletea mataji na  sifa Tanzania katika medani za kimataifa lakini hauna udhamini  wowote ,mpaka sasa ni mchezo  ambao unaojiendesha wenyewe kwa nguvu za  wadau wachache wachovu  na mabondia wenyewe ambao uwezo wao ni mdogo sana kukikidhi matakwa kamili ya mchezo wenyewekam ilivyo kwa wenzetu,ni mchezo  ambao una huduma nyingi zinazohitaji nguvu ya wadhamini ili  uendelee kuboreka zaidi.
Akizungumza na vyombo vya habari katibu wa ngumi za kulipwa nchini bw Ibrahim kamwe , amesema imewaalika viongozi wa baraza la michezo (BMT), na viongozi wengine wote wa ngumi za kulipwa watakuwepo kama vile Emmanuel mlundwa,names kavishe,  makaranga,Onesmo ngowi,kinyogoli,  matumla, Zuwena kibena(mama zugo) na viongozi wadau wa karibu na ngumi wamealikwa kuhudhulia mkutano huo ambao utafanyika Siku ya terehe moja ya mwezi wa pili katika ukumbi wa vijana hall kinondoni. hivyo kamwe alimaliza kwa kuwaomba kila anaejijua kuwa yeye ni bondia wa ngumi za kulipwa na promota wangumi  ahudhurie bila kukosa mkutano huu muhimu sana kwa wamasumbwi ya nchi  yetu.

mapambano ya ngumi mbagal azak hem


Bondia Abuu Abas kushoto akioneshana umwamba wa kutupiana makonde na Abdul Zugo wakati wa uhamasishaji wa tuzo za PSPF Boxing Award zilizofanyika katika viwanja vya Zakhem Mbagala Dar es salaam tuzo hizo zinafika tamati january 25 katika ukumbi wa PTA Sabasaba Zugo alishinda kwa K,o ya raundi ya pili picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

Wednesday, January 22, 2014

ASUTWA USIKU KUCHWA KWA KUMNYANYASA MDOGO WAKE WA MIAKA SABA

 MDADA ANAYEDAIWA KUMTESA MDOGO WAKE NDO HUYO
 WATU WAKIWA WAMEJAZANA NJE YA NYUMBA ALIYOPANGA


 MJUMBE AKITAKA AMTOE NDANI
 MTO AKIWA AMESHIKWA NA WAKAZI WA ENEO HILO KEKO

USAJILI WA OKWI YANGA WAZUIWA


USAJILI WA OKWI YANGA WAZUIWA
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limesimamisha usajili wa mshambuliaji Emmanuel Okwi kutoka Uganda katika timu ya Yanga wakati likisubiri ufafanuzi kutoka Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA).

Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya TFF iliyokutana leo (Januari 22 mwaka huu) kupitia masuala mbalimbali, imesimamisha usajili huo baada ya kubaini kuwa Okwi aliruhusiwa kuichezea SC Villa ya Uganda kwa kibali maalumu kutoka FIFA.

Okwi ambaye aliingia mgogoro na klabu yake ya Etoile du Sahel ya Tunisia aliruhusiwa na FIFA kuchezea SC Villa kwa kibali maalumu (provisional permit) cha miezi sita ili kulinda kiwango chake wakati suala lake dhidi ya Etoile du Sahel likishughulikiwa na shirikisho hilo la kimataifa.

Katika FIFA kuna kesi tatu kuhusiana na suala la mchezaji huyo. Wakati Okwi ameishitaki klabu hiyo FIFA kwa kutomlipa mshahara, Etoile du Sahel imemshitaki mchezaji huyo kwa utoro. Nayo Simba imeishitaki Etoile du Sahel kwa kushindwa kuilipa ada ya mauzo ya mchezaji huyo ambayo ni dola za Marekani 300,000.

Hivyo, TFF imeiandikia FIFA kutaka kujua iwapo mchezaji huyo anaweza kucheza Ligi nchini Tanzania wakati Etoile du Sahel ikiwa imefungua kesi katika shirikisho hilo la kimataifa ikidai Okwi bado ni mchezaji wake.

MECHI ZA TANZANIA PRISONS YAZASOGEZWA
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limesogeza mbele mechi za raundi ya 14 na 15 zinazoihusu timu ya Tanzania Prisons zilizokuwa zichezwe Januari 25 na 29 mwaka huu.

Awali Tanzania Prisons ilitakiwa kutafuta uwanja mwingine wa kuchezea mechi hizo dhidi ya Ruvu Shooting na JKT Ruvu kutokana na Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine kutokuwa tayari kwa Ligi Kuu ya Vodacom wikiendi hii.

Mechi hizo sasa zitachezwa kati ya Februari 6 na 8 mwaka huu kwenye uwanja huo huo wa Kumbukumbu ya Sokoine.

Boniface Wambura Mgoyo
Ofisa Habari na Mawasiliano
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
  • 1 Attachment

sherehe za kumpongeza naibu waziri wa maliasili katika hoteli ya traventine


 akisalimiana na moja wa wazee wa mkoa wa dar es salaam wanaotokea mufindi
 akiwa na mkewe mkubwa
 akimnywesha mwanwe wa mwisho kwamke mdogo
akisalimiana na mmoja wa wageni waalikwa

ZIARA YA KAMATI YA BUNGE YA MAENDELEO YA JAMII KWA WILAYA YA KINONDONI NA ILALA

 WAZIRI SOPHIA SIMBA AKISEMA NENO
 WAJUMBE WA KAMTI HIYO WAKITAFAKARI RIPOTI MBOVU YA WILAYA YA ILALA
 Capt Joh Komba akiwa na Mh Obama wakijaribu kutaza ripoti kwa kina
 afisa maendeleo ya jamii wa kinondoni akiwa silisha mada


 maua daftarai na mkurugenzi wa manispaa ya kindoni
 mh mkulo
 naibu meya kinondo songolo

Kinondoni; Vijana wa kiume wazito kujitokeza katika huduma za mikopo

Na Humphrey Shao, Dar es Salaam
HALMASHAURI ya manispaa ya Kinondoni  kama ilivyo kwa halmashauri zote nchini imekuwa ikitekeleza majukumu yake kwa jamii ikiwemo kuwezesha vikundi vya wanawake na vijana kwa kuwapatia mikopo yenye masharti nafuu kupitia mifuko ya mikopo mbalimbali tangu mwaka 1995.
 Moja ya mifuko hiyo ni mfuko wa kuendeleza wanawake uitwao WDF mfuko ambao unatekelezwa kwa kushirikiana na wizara maendeleo ya jamii jinsia na watoto.
Wizara ambayo inakopesha fedha kwa manispaa nayo inakopesha kwa vikundi vya uchumi vya wanawake na kusimamia marejesho yake ikiwa na lengo la kumkomboa mwanamke aliye katika hali ya chini.
Hivi karibuni nilipata fursa ya kutembelea manispaa ya kinondoni nikiwa na kamati ya bunge inayoshugulika na huduma za jamii ikiongozwa na mwanamama mahiri D.k Maua Daftari akiwa kama mwenyekiti.

Dk Maua ambaye alichukua fursa yakuwapongeza viongozi wa manispaa hiyo kwa kazi ngumu wanayofanya na kuwataka kuongeza mkazo zaidi katika harakati za kumkomboa mwanamke kupitia mikopo inayotolewa na wizara.
Mara baada ya kusema hayo Dk Maua alimtaka kaimu afisa maendeleo wa jamii wa Manispaa ya kinondoni Mwajuma Magwiza kueleza ni namna gani walivyoweza kutumia mikopo ya awali kutoka serikalini kuwafikia wanawake.
Magwiza anasema kuwa kupitia mfuko wa WDF Manispaa ya kindoni ilipokea jumla ya kiasi cha shilingi milioni 18,84000.00.
Anasema fedha hizo ambazo zilitumika katika kukopesha vikundfi mbalimbali lakini kufika mwaka 2003 kiasi cha fedha shilingi 4,531338.00 hakikuweza kurejeshwa kutokana na sababu mbalimbali za wakopaji wa mfuko wa WDF.
Magwiza anasema kuwa katika kuendeleza mfuko huu wamekutana na changamoto mbalimbali ikiwemo ya bahadhi ya wakopaji kutopatikana katika maeneo waliyokuwepo.
“Wananchi wengi wanaimani kuwa fedha hizi zinazotolewa kwa mkopo kwa lengo la kumsaidia wanawake azitakiwi kurudishwa jambo linalochangia kwa kiasi kikubwa kukwamisha mradi kukua kwa kasi iliyopangwa’’anasema Magwiza.
Anasema kuwa pia waliweza kutoa mikopo kupitia mfuko wa maendeleo ya wanawake na vijana ulionzishwa na tume ya jiji la Dar es Salaam.
Anasema katika mfuko huo Manispaa ya kinondoni iliweza kupata shilingi 56,380,000 ambazo zilianza kukopeshwa kwa vikundi vya ujasiliamali vya wanawake na vijana.
“Kwa ujumla hali ya utoaji na urejeshwaji wa mikopo kwa kila mwaka tangu mikopo ilipoanza mwaka 1998 hadi mwaka 2006 na fedha ya yote ya mtaji iliyokopeshwa ni shilingi 387,124,000.00 amabpo kiasi cha marejesho kilikuwa ni 157,469,346.00 huku kiasi kilichobaki kwa wadaiwa kilikuwa 231,654,654.00”anasema Magwiza.
Anasema kuwa mbali ya matatizo yote hayo jumla ya wakazi wa kinondoni wanawake kwa vijana walionufaika ni 9,752 huku kati ya hao wanawake walikuwa 7,250.

Anasema katika kufanikisha huduma hiyo ya utoaji mikopo kwa wananchi wake manispaa hiyo imeweza kuingia ubia na benki ya wananchi ya Dar es Salaam hili wananchi waweze kupata mikopo kupitia benki hiyo.
Mbali na mikopo ubia huo ulikwenda sambamba na kutoa elimu ya ujasiliamali kwa wanawake na vikundi vya hili waweze kuwa na nidhamu na fedha wanazokopa.
Anasema katika kutekeleza hilo Halmashauri ya Manispaa ya kinondoni imefungua mfuko wa akaunti ya mikopo  ya wanawake na vijana katika benki ya wananchi wa Dar es Salaam.
Anasema katika mwaka wa fedha wa 2011 mpaka 2014 jumla ya kiasi cha fedha cha shilingi milioni 440,000,000 zilitengwa kwa ajili ya mikopo ya Vijana na wanawake.
Anasema licha ya manispaa kutenga kiasi hicho cha fedha bado kuna kundi la Vijana wa kiume ambalo limekuwa zito kujitokeza kuomba mikopo hiyo ambayo inatolewa kwa vikundi na mtu mmoja mmoja.
Anasema kupiti utaratibu huo wameweza kupata mafanikio makubwa ikiwemo na kuimarisha na kukuza uhusiano na ushirikiano kati ya serikali na wakazi wa Manispaa ya kinondoni.
Anaweka wazi kuwa Halmashauri inakusudia kuendelea kutenga fedha za mikopo katika bajeti zijazo hili kuongeza thamani ya mfuko huo ambao umeonekana kuwa tija kwa wakazi wa kinondoni hivyo kiasi cha shilingi milioni 500,000,000 kitaongezwa ifikapo mwaka wa fedha wa 2015/2016.
Hivyo aliwataka vijana kuongeza juhudi za kupeleka maombi hasa wakiwa katika vikundi hili waweze kupatiwa fedha hizo kwa haraka kuliko vile wanavyofikiri kukaa vijiweni.
Anaweka wazi kuwa hiyo ndio fursa pekee ya kumkomba kijana wasasa ambaye anatakiwa kujikita katika ujasiliamali.
mwisho



MOTO ULIVYO WAKA KATIKA NGUZO YA KWA MTOGOLE