Wednesday, February 20, 2013



Umuhimu wa kutunza Kumbukumbu Tunapoelekea urasimishaji
NA HUMPHREY SHAO

MARA zote tasnia ya sanaa na wasanii wenyewe wamekuwa watu wa kutoa lawama serikalini bila kustadi nini wanatakiwa kufanya hili kuweza kufikia weredi kama ilivyo kwa wasanii wengine wa kimataifa.

Hali hiyo imeelezwa na  mkurugenzi wa utafiti na na mafufunzo kutoka BASATA Godfrey  Lebejo wakati kutoa muadhara katika jukwaa la sanaa linalo andaliwa na BASATA kwa kushirikiana na CAJA uunaofanyika kila jumatatu katika ukumbi wa BASATA juu ya umuhimu wa wasanii kutuinza kumbukumbu tunapoelekea urasimishaji.

Lebejo anaanza kwa kutaja nini kinachotakiwa kumfanya msanii aweze kufanya utafiti wa kazi zake.

Dhana hasa ya tafiti ni kutakiwa kujiuliza maswali ama kuuliza maswali watu wengine kama wanavyofanya wachezaji mpira huku kukiwa na lengo moja la kupata jibu lilo sahii katika kufanikisha kazi yako ya sanaa.

Anataja kuwa chamsingi kinachotakiwa katika kufanya tafiti hili kuweza kupata habari ya kweli kwa ajili ya kuziba pengo lililopo katika tasnia husika, hivyo kusisitiza kuwa kama kuna tafiti inafanyika alafu aishuki chini kwa walengwa hiyo aina maana katika maendeleo ya Tanzania.

“ kama kuna la msingi wasanii wanatakiwa kufanya ni hili hapa la kujiuliza maswali haya (1) Nifanyeje kazi yangu (2) Nani mlaji wa kazi yangu (3) wapi ntauza kazi yangu (4) Soko likoje” alisema Lebejo.

Anawasilisha kuwa tafiti zinatoa hali halisi ya kazi za sanaa na sanaa kwa ujumla kujua ikoje na kutoa majibu nini kifanyike hili matatizo yaweze kuondoka.

Aliongeza kuwa kama msanii lazima ajiulize matatizo  gani yanayo ikabili sanaa na kwa kipindi chote ambacho  msanii yupo sokoni na kama anataka kuingiza kazi sokoni.

Katika urasimishaji wa kazi za sanaa Lebejo alisema kuwa serikali imeamua kurasimisha kazi kwa kuanzia kwenye muziki na filamu kufuatia kuwepo kwa tafiti juu ya hali halisi ya faida za kazi hizi katika kukuza pato la Taifa.

“kwa miaka mingi serikali imeshindwa kutambua jinsi gani sanaa zilivyocghangia katika pato la taifa licha ya kuwepo vyombo mbalimbali vya kusimamia kazi za sanaa hapa nchini” alisema Lebejo.

Alisema kuwa hali hiyo imetokana na serikali kutoingiza urasimu wa kazi za sanaa kuwa rasmi na kupuzia    mchango wake na kutotilia manani.

Alitaja sanaa kama za uchoraji na uchongaji zimekuwa zikingizia taifa fedha nyingi za kigeni kuliko sanaa nyingine huku ufumaji na upikaji wa nguo kama batiki zikifuatia kutokana na wageni wengi wanaofika hapa nchini kupenda bidhaa hizo lakini kiasi chote hicho utambiwa nimapato ya utalii na kusahau umuhimu wa sanaa.

Anatanabaisha kuwa hali hiyo ilitokana na sera ya utamaduni kutotamka sanaa kama kazi kama zilivyo kazi nyingine na kupelekea michango yao kuto onekana.

Mara baada ya kuwepo kwa mkanganyiko na malalamiko mengi kutoka kwa wasanii hapa nchini ilipelekea serikali kufanya tafiti kupitia mtafiti kutoka Chuo kikuu Yehova nisi na kutanabaisha kuwa sanaa inalipa hali iliyopelekea serikali kurasimisha kazi hizo kuanzia julai mwaka huu.

Lebejo alieleza kuwa serikali imeamua kutatua matatizo yaliyopo katika sekta ya sanaa kupita urasimishaji hivyo kutokana na matokeo ya matatizo yaliyopo katika sanaa.

“licha ya kuwepo kwa urasimishaji wa kazi za sanaa lakini bado kuna jambo gumu sana linalo onekana kwa wasanii wengi wa Tanzania kuwa ni wagumu kutunza kumbukumbu za kazi zao na matokeo ya kazi hizo hali iliyosababisha kuwepo na mgogoro mkubwa juu ya swala zima la haki miliki” alisema Lebejo.

Alitaja kuwa waimbaji wengi watanzania wamekuwa wakitumia haki miliki za watu na za mataifa mengine katika nyimbo zao hivyo taifa litakapoingia katika mchakato wa urasimishaji wa kazi hakuna nyimbo ya mtu yenye midundo itakayopigwa hapa nchini.

Alitaja mfano kuwa nyimbo nyingi za muziki wa injili zimeelemea katika midundo ya Afrika kusini na mingine Makhirikhiri na kusahau kuwa hiyo ni haki ya watu na utamaduni wao hivyo sheria itawataka kutumia midundo za makabila ya watanzania.

  Alisema kuwa midundo na maanzari za nje ya nchi kubanwa hali hiyo itawafanya wasanii wa kitanzania na waandaaji wanaochipua kama uyoga kuwa wabunifu.

Hilo litakwenda sambamba na wasanii wenyewe kujitambua kwa kuweza kuandaa taharifa zao binafsi ‘cv’ hili kufanya kutambulika kirahisi na watu wakimataifa.

Hali hiyo ilikwenda sambamba na wachangiaji mbalimbali kutoa maoni yao juu ya mada hiyo katika kufikia malengo ya kimataifa kwa wasanii wa ndani.

Sacha Emanuel ni mwandishi wa script na katibu wa shirikisho la wandishi wa Muswada ‘script’ wilaya ya ilala alishangazwa na mashirikisho kuwa mstari wa nyuma katika kutoa elimu nakupokea mafunzo yanayotolewa na basata kuwafikishia wasanii.

“shida ipo sana hapa nchini kwani wandishi wa miswada na waongozaji ambao mara zote wamekuwa watu wa kukopi vitu kutoka nje ya nchi kutokana na kuwa wavivu wa kufanya tafiti” alisema Sacha.

Nae Amisa Sambwe alitaka wasanii kujiuliza na kujisomea hili kujua ni tafiti gani wanatakiwa kufanya na kwa wakati gani zifanyike.

NA HUMPHREY SHAO

JINA la Isike Samweli  sio jina geni kwa wale wapenzi tunaofatilia kwa karibu sana filamu za hapa nchini na hata kung’amua ni msani gani anafanya vizuri licha ya kutokuwa na jina kubwa katika tasnia hii ya filamu.

Hivi karibuni nilipata nafasi ya kutembelea maeneo ya kariakoo kumuona rafiki yangu mwenye asili ya kihindi nayefahamika kwa jina la Purteshi kwa wale wadau wa filamu wanamjua mtu huyu ndipo nilipopata fursa ya kumuona kijana huyu katika ofisi hizo bila kung’amua ni nani.

Sekunde chache baadae anawasili msanii wa filamu mwingine Lucknes Mokiwa ambaye ni rafiki yangu wa karibu na kunitambulisha kuwa huyu ndio Isike, mtayarishjai mdogo kulikoi wote hapa Tanzania  nilishtuka kwani yupo tofauti na jinsi jina lake nilivyokuwa nikilisoma katika filamu mbalimbali.

Kama ilivyozoeleka hapa nchini ni vigumukuamini kijana mdogo wa miaka 19 kuwa mtayarishaji wa filamu nyingi ambazo hata hao wasanii maharufu awajafikia.
 
Isike ambaye alizaliwa Septemba mwaka 1993 na kupata elimu ya msingi katika shule ya msingi Magomeni na badae aliweza kucahaguliwa kujiunga na sekondari ya goba ambayo wilaya kinondoni.

Anaeleza kuwa hapo awali aliweza kujiusiha na utangazaji wa vipindi vya watoto lakini alipokuwa darasa la saba aliweza kushawishika moja kwa moja kujiunga na sanaa ya uigizaji.




“kama kuna mtu mwenye bahati ni mimi kwani niliweza kuingia kwenye sanaa kwa mguu wa kulia katika kikundi cha shirikisho na mara baada ya miezi sita niliweza kuchaguliwa kucheza igizo la ukumu ya tunu ambalo liliweza kunitambulisha huku kampuni ya kwanza kufanya nao kazi ilikuwa ni Benchmark” Alisema Isike.

 Alinieleza akiwa na umri wa miaka 16  aliweza kuandaa filamu yake hapo akiwa na  kuwa kama mtayarishaji wa kwanza mtoto hapa nchini.

Akiwa kidato cha kwanza Filamu hiyo ilikwenda kwa jina la ‘2 sister’ iliweza kuwashirikisha wasanii kama Masinde, penina na Hidaya Njaidi kisha kufuatiwa na filamu iliyokwenda kwa jina la ‘Missed Call’ ambayo iliwashirikisha Hashimu Kambi ,Tekla Mjata, Komando Yoso.

Mara baada ya kufanikiwa kuuza filamu hizo huku akitumia njia ya kusambaza mwenyewe  aliweza kupata mafanikio makubwa ambayo kamwe hato ya sahau maisha ni mwake.

“kama nilivyo kueleza mimi nilifiwa na wazazi wangu wote wawili nikiwa darasa la nne hivyo fedha hizo ziliwezesha kuanza kujitegemea kwa kupanga chumba changu mwenyewe na kuanza kujilipia ada yangu ya shule na kuacha kukaa kwa mjomba yangu ambaye alikuwa akinilea kwani mtazamo wake na wangu ulikuwa tofauti katika sanaa” alisema Isike.


Anaeleza kipato hicho kilimfanya aweze kuisadia familia yake pia na muda mchache baadae mwaka 2010 aliweza kupata mkataba na kampuni ya KAPIKO na kutenegenza filamu iliyokwenda kwa jina la ‘Love in School’.

Filamu hii ambayo aliweza kumshirikisha Flora Mvungi, Hidaya Njaidi Iliweza kufanya vizuri sokoni kuliko alivyotegemea na kupewa nafasi ya kufanya filamu nyingine katika kampuni hiyo ya KAPIKO.

‘The impact’ ndo jina la filamu hiyo ambayo iliweza kumshirikisha mwanadada mahiri Jackline Wolper, Hashim Kambi, Flora Mvungi nayo iliweza kufanya vema na kumpeleka katika ukurasa mpya wa maisha ya sanaa.


Mara baada ya hapo aliweza kupumzika kwa kipindi cha miezi minne kwa ajili ya kujiandaa na mitihani ya kidato cha nne.

Anaeleza kuwa kila kazi inachangamoto yake hasa kwa wakati uliopo Isike anakiri kuwa aliweza kupata changamoto kubwa sana kwa kucheleweshewa malipo yake na


bahadhi ya kampuni alizoingia nazo mkataba kulingana na umri wake kiasi cha kumkera sana.

Lakini anakiri kuwa amekuwa akiheshimiwa na wasani wakubwa kuliko alivyotegemea hali inayomfanya ajisikiea bora zaidi kuliko hapo awali.


Anatanabaisha kuwa mara baada kumaliza mitihani yake ya kidato cha nne aliweza kujiunga na kampuni ya PAPAZI ambayo iliweza kusaini nae mkataba kisha kufanya nao kazi ambapo mwaka 2012 aliweza kutoka na filamu iliyokwenda kwa jina la ‘Ivan Tears’  na kufanya poa katika soko la filamu.

Alitaja filamu hiyo iliyiomshirikisha mwanadada shilole na baadae kutoa filamu ya ‘loose control’ ambayo ilimshirikisha Catty ,Tecla Mjata, Kojack na Steve wamaisha Plus hapo ndio ulikuwa mwisho wa kufanyakazi na PAPAZI.


Baadae alifanya filamu ya ‘Jealous’ iliyowashirikisha Mainda , Hashimu Kambi na Hidaya Njaidi ambayo iliweza kusambazwa na kampuni ya Pastor Muyamba.

Hata hivyo nyota ilizidi kung’ara kwa kijana huyu kufanikiwa kupata mkataba na Kampuni ya SPLASH kwa kuanza na filamu ya Oxygen ambayo mwanadada Elizabeth Michael ‘LULU’alicheza kama star.

Filamu hiyo iliyofanya vema sokoni ilimfanya kuongezewa muda wa kufanya filamu nyingine na kampuni hiyo ndipo mwezi janauri mwaka huu alitoka na filamu inayokwenda kwa jina la lonely.

Filamu ambayo amefanya na hemedi suleimani na wengine wengi kuwa gumzo katika mitaa yote ya jiji la Dar es Salaam.

Filamu nyingine ambazo ameweza kufanya ni kama ‘Sad Moment’ na kukiri kuwa nidhamu na uti ndio silaha ya mafanikio katika kazi zake za sanaa licha ya watu kuongea mengi na kusahau nini wanatakiwa kufanya.

“kiukweli nitakuwa mnafiki nisipo washukuru wasanii wenzangu kama Dotnata, Jackline Wolper, Lucknes Mokiwa na wengine wengi kwa kuwa msaada mkubwa kwangu kwani wao ndio wamekuwa watu wa kunitia moyo kila siku.

Anaeleza kuwa ndoto zake ni kufika mbali na kimataifa zaidi kwani tayari njia imepatikana na kikubwa anachojivunia ni umri wake ambao unamruhusu kufanya mambo makubwa.


MWAJAUMA JIMAMA AIPAMBA MASHAUZI TCC

Mnenguaji Maarufu nchini Mwajuma Thabiti ' Mwajuma jimama' akifanya vitu vyake mbele ya mwimbaji wa bendi ya Mashauzi Classic, Isha Ramadhani wakati bendi hiyo ilipofanya onesho lake katika ukumbi wa TCC Chang'ombe Dar es salaam 
Mmoja wa mashabiki wa fani ya unenguaji  kulia akimpingia makofi baada ya kumtunza Mnenguaji Maarufu nchini Mwajuma Thabiti ' Mwajuma jimama' ambaye anaonekana akifanya vibwanga vyake  wakati wa maonesho ya bendi ya Mashauzi Classic katika ukumbi wa TCC Chang'ombe Dar es salaam
Mnenguaji Maarufu nchini Mwajuma Thabiti ' Mwajuma jimama' akifanya vitu vyake mbele ya mwimbaji wa bendi ya Mashauzi Classic, Isha Ramadhani wakati bendi hiyo ilipofanya onesho lake katika ukumbi wa TCC Chang'ombe Dar es salaam 
Isha Ramadhani kushoto akiwa na mnenguaji maarufu Mwajuma Thabiti ' Mwajuma Jimama'
Mnenguaji Maarufu nchini Mwajuma Thabiti ' Mwajuma jimama' akifanya vitu vyake mbele ya mwimbaji wa bendi ya Mashauzi Classic, Isha Ramadhani wakati bendi hiyo ilipofanya onesho lake katika ukumbi wa TCC Chang'ombe Dar es salaam pich

Friday, February 15, 2013

mwanaeme mwenye mataiti aishangaza Dunia