Monday, December 16, 2013

.YANGA IMETIMIA


Mchezaji mpya wa Yanga Hassan Dilunga Kushoto akijaribu kuchukua mpira wa kutoka kwa kiungo wa Timu hiyo Athuman Iddi(Chuji) Wakati wa mazoezi ya timu hiyo, wachezaji hao ambao wamejiunga na kikosi hich jana mara baada ya kumalizika kwa mashindano ya Chalenji. Picha na Humphrey Shao.




Na Humphrey Shao, Dar es Salaam

KOCHA wa klabu ya Yanga Ernie Brandts amesema ameridhishwa na kiwango kilichionyeshwa na mchezaji wa timu hiyo wakati wa mazoezi na kumtaja ni mmoja kati ya wachezaji wenye uhakika wa namba katika kikosi cha kwanza.
Brandts alisema hayo alipiokuwa akizungumza na Rai mara baada ya kumalizika kwa mazoezi ya timu hiyo katika viwanja vya bora kijitonyama.

“Kila mchezaji ananafasi ya kucheza kikosi cha kwanza lakini Yule anayeonyesha uwezo na juhudi mara zote ndio ushikilia hiyo namba, hivyo kwa dilunga kwake ni mwanzo mzuri kama nilivyomuaona tangu awali naamini ataleta mabadiliko makubwa” alisema Brandts.

Alisema kuwa kwa sasa timu yake iko vizuri na inajiandaa na mchezo wake wa kirafiki dhidi ya timu ya Simba unaotambulika kw ajina la nani mtani jembe.

Aliongeza kuwa kwa sasa ni mapema sana kuzungumzia mchezo huo kwani nasubiri wachezaji wangu wote watimie ndio nitakuw ana kauli kwa ajili ya mchezo huo.
Mwisho

Na Humphrey Shao, Dar es Salaam
Beki wa kulia wa klabu ya Yanga Rajabu Zahir ameumia goti la kushoto wakati akiwa mazoezini na timu hiyo nakupelekea kutolewa nje.
Kwa mujibu wa taharifa ya daktari wa timu hiyo Nassoro Matyuza alisema kuwa maumivu hayo sio makubwa sana hivyo anahitaji mapumziko ya siku moja kwa ajili ya kujiweka sawa.

“Maimivu yake sio makubwa hivyo nawatoa hofu wapenzi wa yanga kuwa muda mfupi tu atakuw afiti hivyo tgemeeni kumona katika michezo inayokuja “ alisema matuzya .

Mbali na huyo wachezaji wengine ambao walikaa nje kwa ajili ya mejeruhi ni Salum Telela na Nadir Haroub ‘Canavaro’ ambao wao walikuwa nje ya uwanja.

Wachezaji Kelvin Yondani,Emmanuel Okwi pamoja na Amisi Kiiza ambao bado awajaripoti kikosini mpaka sasa.




Mshambuliaji wa klabu ya Yanga Said Bahanuzi akimpa mwili kiungo wa timu hiyo Haruna Niyonzima wakati wa Mazoezi ya timu hiyo katika viwanja vya bora kijitonyama. Picha Na Humphrey Shao.

Saturday, December 14, 2013