Wednesday, May 16, 2012


Rio Ferdinand Beki aliyetoswa Euro 2012 kwa fitina
  Godlisten Shao na Mashirika ya Habari.
SIKU ya tarehe 22 Julai mwaka  2002,Rio Ferdinand alijiunga na klabu ya , Manchester United, kw amkataba wa miaka mitano na kuwa mchezaji ghali aneyecheza safu ya nyuma katika historia ya  uingereza , akichukua nafasi ya beki aliyekuwa ghali kipindi cha mwaka 2001 Lilian Thuram.
Ferdinand ambaye ni raia wa uingereza alizaliwa Novemba  7, 1978 katika kitongoji cha  Peckham, mjini London, nchini England,na ni mchezaji anayecheza nafasi ya nyuma katika klabu ya Manchester United mpaka sasa na amekuwa mchezaji wa kulipwa kuanzia mwaka 1997.
Beki huyo ambaye alihamishwa kwa ada ya pauni milioni ishirini za uingereza na kuifanya klabu yake ya awali ya leeds kumtangaza kuwa inamuuza mchezaji huyo kwa ka zaidi ya pauni milioni thelasini.  
 Leeds United baadae ilichukua kiasi hicho chapesa zake za awali kama na kusaidia timu hiyo ambayo ilikuwa na tatizo la kiuchumi kipindio hicho, na kufanya Ada kamili ya kumuhamisha mchezaji huyo kwenda Manchester United kuwa Pauni milioni 33.
 Ferdinand ambaye alionekana ayuko vizuri kimchezo mara baaday kucheza chini ya kiwango katika mchezo wa klabu bingwa barani ulaya mchezo uliozikutanisha timu ya    Manchester United na Real Madrid 
Mwaka  2003, alishindwa kufika mahabara kwa ajili ya vipimo vya kugundua kama anatumia dawa za kuongeza nguvu au lah ,hali hii ilimtokea pale aliposahau kutokana nakuwa na harakati nyingi za kuhama makazi yake ya zamani nakuhamia makazi mapya na baadae kuendelea na shughuli zake zingine.
 Hali iliyosabaisha kamati ya nidhamu ya chama cha soka nchini Uingereza  FA kumtoza faini ya kutocheza msimu mzima wa ligi na klabu yake kulipa faini ya Pauni 50,000.
Hari ilifanya klabu yake Manchester United kukata rufaa kw amadai ya kuwa ameonewa kwani mchezaji mwengine kutoka Manchester City ,Christian Negouai, alitozwa faini ya Pauni 2,000 kwa kutokwenda kupima.
Ingawa ,Rais wa  FIFA Sepp Blatter alitupilia mbali rufaa hiyo kwa kusema kosa la Ferdinand alifanani na la Negouai ambaye yeye alichelewa kupima kwa sabau ya tatizo la foleni ya magari hivyo alionesha nia ya kutaka kwenda kupima wakti yeye aligoma kwenda kupima kwa sabau zake binafsi nakumuongeze aadhabu ya miezi 12 mingine.  
Ferdinand ambaye aliweza kutwa taji la ubingwa wa ligi ku kwa mara ya kwanza akiwa na klabu ya Manchester United na kupata medali ya   Carling Cup 2006, na kufuatiwa ushidi wa pili katika kipindi cha 2003 na  2005 FA Cup.
Mnamo 14 Desemba  2005, katika mchezo dhidi ya Wigan Athletic, Ferdinand aliweza kushinda bao lake la kwanza akiwa na United , katika mchezo ambao walishinda bao  4–0 . hili lilikuwa goli la kwanza mara baadaya mika mitatu akiwa  Old Trafford.
Baadae akafuatiwa na goli la nguvu la kichwa amabalo alifunga wakati wa mechi dhidi ya   West Bromwich Albion.na baade akafunga bao dakika za mwisho katika mchezo dhidi ya mahasimu wao  Liverpool mchezo uliopigwa katika dimba la  Old Trafford,na ndio lilikuwa goli muhimu kwa United mpaka leo .
Baada ya kuonyesha kiwango kikubwa katika ligi aliweza kuchaguliwa kwenye kikosi bora cha msimu wa ligi kuu ya uingereza cha mwaka  2006–07.
Ferdinand alianza vizuri msimu wa ligi wa  2007–08, kuwa kati ya mabeki wakutegemewa wa Man United ukilinganisha na hap awali alipojiunga na klabu hiyo na kuweza kupachika bao lake la kwanza la msimu katika mechi dhidi ya Aston Vila mchezo uliopigwa,20 Octoba 2007 katika dimba la Vila park.
   
Katika michuano ya  FA Cup mchezo wa robo fainali uliochezwa ,8marchi dhiodi ya Portsmouth, Ferdinand aliweza kukaa golini kma Golikipa baada ya kipa tegemezi wa klabu hiyo Edwin van der Sar kutoka uwanajani mara baada ya kuptwa namajeraha kwani kipindi hicho kipa wa akiba,Tomasz Kuszczak, kufungwa kwa penati na kupelekea kutolewa katika michuano ya FA CUP.
Mnamo  6 April 2008, kweney mchezo dhidi ya Middlesbrough, Ferdinand alitolewa nje kwa matatizo aliyoyapata kwenye mguu . hali hiyo ilimfanya kukosa mchezo war obo fainali ya UEFA ambao ulipigwa 9 april 2008  dhidi ya  A.S. Roma.
Baada ya United' kufungwa bao 2–1 na  Chelsea katika mchezo wa ligi kuu  April 2008 Ferdinand, aliweza kuwa na hasira kutokana na kichapo hicho na kutoamaini kuwa timu hiyo ingeweza kupenya kwenye ukuta wa United  .
Licha ya kuhusishw ana uvumi wa kuhamia klabu ya Barcelona ya nchini ,Hispania  tarehe 16 April 2008 kati ya  Michael Carrick na  Wes Brown, Ferdinand kw apamoja walikubaliana kusaini mkataba mwingine wa miaka mitano kuendelea kucheza United  mkataba amabo uligharimu Pauni milioni 130,000 kwa wiki na mkataba huo utamuweka mchezaji huyo katika timu hiyo ya mashetani wekundu mpaka 2013,mkataba amabao ulisainiwa15 Mei 2008.
Baada ya hapo tarehe  21 Mei 2008, Ferdinand alitajwa kuwa kama nahodha mpya Manchester United  katika mchezo wa klabu bingwa barani ulaya mchezo uliwazikutanisha Manchester United na  Chelsea. Na kufanikiwa kuchukua kombe akiwa na wachzaji wakongwe kama  Ryan Giggs, na  Gary Neville.
Ferdinand ambaye kwa sasa ataweza kuwemo kwenye kikosi cha uingereza kinacho shiriki michuano ya Euro 2012 kutokana kocha mpya wa timu hiyo Roy Hodgson kuhofia timu kushindwa kufanya vizuri katika safu ya nyuma kutokana wailihao kuwa katika ugomvi wa muda mrefu.
Hata hivyo mchezaji huyo ajazungumzia chochote ju ya mahamuzi ya meneja huyo mpya ambaye ameonekana kutegua kiwango hicho.
mwishooo
 
Robin van Persie mkali anayesubiriwa  kwa hamu Man City  

Godlistern Shao na Mashirika ya habari
Mashabiki wengi wa klabu ya  Arsenal wamekuwa wakimuona mshambuliaji wa Klabu hiyo Robin van Persie  kuwa ni mchezaji wa kudumu katika klabu hiyo tangu aliposaini kuchezea klabu hiyo mwaka 2004 na ni mbadala wa mshambuliaji wa kidachi  Dennis Bergkamp ambaye alitandika daluga katika masuala ya soka   
Ingawa mshambuliaji huyo amekuwa akisumbuliwa na majeruhi kadhaa marakwa mara kiasi cha kufanya mshambuliaji huyo kucheza kwa kiwango kilichodhaniwa pindi alipokuwa kijiunga na washika bunduki hao wa London.
Pamoja namatatizo yote  yaliyomkuta mchezaji  van Persie bado ameonekana kuweka mguu wake kuwa ndio biashara pekee katika maisha yake mara baada ya kuwa mshambuliaji wa kutumainiwa peke     yake akichukua nafasi ya Emmanuel Adebayor ambaye aliondoka The Gunners na kwenda kujiunga na Man City.

Robin van Persie amabye ni raia wakidachi alizaliwa Agosti 6,1983 katika Mji wa Rotterdam nchini Uholanzi  ambako ndiko alikulia na maisha yake mpira yalipoanzia.
Van Parse amabye kwa sasa anaicheze kalabu ya Arsenala huku akiwa amebakiza mwaka mmoja kumalizika kwa mkataba wake amekuwa yuko njia panda mraa baada ya Mabingwa wapya wa ligi kuu ya Uingereza Man City kumtangazia dau la kung’oa katika klabu hiyo.
Kabala ya kuchezea Arsenal Van Parsie alipata kuchezea klabu ya Feyenoord ya nchini Uolanzi kwa kipindi cha miaka mine kuanzia 2001 hadi 2004 na baade kujiunga na washika bunduki wa London.

 

Van Persie ambaye alikimbia kutoka kwenye familiya yao amabpo kipindi hicho mama yake alikuwa anafanya kazi ya kupaka rangi na baba yake alikuwa mchongaji wa vinyago huko Uholanzi 
Akiwa na umri wa miaka  14 alijiunga na timu ya vijana ya Uholanzi lakini baade alichwa na timu hiyo kutokana na kushindwa kuelewana na makocha wake na kuendelea kubaki kuichezea klabu yake ya Feyenoord. 
Baadae alionekana kuwa na kiwango cha hari ya juu na kuwa mchezaji wa kuanza katika kikosi cha kwanza cha Feyenoord kutokana na matatizo ya kumia marakwamara yalimfanya awe mtu wa kuanzia kikosi  B.
Ingawa watu wengi waliamini kuwa Van Persie  amegombana na kocha wake  Bert van Marwijk ndio sababu ya kumfanya mchezaji wa akiba katika ,pia kocha aliweza kumrejesha mchezaji huyo nyumbani mara baada ya kuonyesha utovu wa nidhamu katika mchezo wa fainali za UEFA mwaka 2003 dhidi ya Real Madrid. .
 Baada ya kufanikiwa kupachika magoli nane katika msimu wa kwanza huku akitokea benchi aliweza kumshawishi kocha wake katika msimu uliofuata wa mwaka 2003-2004 kuwa ndie mchezaji anayeweza kuanza.
Baada ya kucheza kweney klabu hiyo bil;a kuwa na mafanikio yoyote nyota huyo aliweza kuuzwa katika klabu ya Arsenal ambayo alionyesha kuwa na mapenzi nayo siku za nyuma kabla ya kuuzwa katika klabu hiyo.

 

Mwaka 2004 Van Persie aliweza kusaini mkataba wa miaka mine na klabu ya Arsenal  na kufanikiwa kuwa mmoja wa wachezaji waliocheza katika kikosi kilichochukua kombe la FA mwaka 2005 kombe ambalo alijaweza kuchukuliwa tena na klabau hiyo.

Mara baada ya mkataba wake kumalizika mwaka 2009 mshambuliaji huyo aliweza kumshawishi bosi wake Arsene Wanger kumpa mkataba mpya wa miaka minne  ambao utamalizika mwakani
 Mshambuliaji huyo ambaye aliweza kumfurahisha bosi wake pindi alipokuwa uwanjani kutokana na stairi yake ya mchezo lakini alikuja kujitia doa pale alipopatiw akadi nyekundu kwenye mechi kati ya Arsenal na Southampton.
 Maisha yalibadilika na kuw amtu mwneye furaha akiwa na Gunners pale alipoweza kufunga goli pekee la kichwa na kupewa tuzo kuwa goli pekee la msimu katika ligi kuu ya England.
 Mshambuliaji huyu ambaye alikuwa kaichez anafasi ya winga lakini alicaha jkucheza nafasi hiyo mara baada ya kubadilishwa na kocha wake Arsene Wanger mara baada ya kuona kuwa awezi kufua dafu mbele ya Thierry Henry ambaye alikuwa katika kiwango cha juu sana.
 Licha ya kuwa na mafanikio yote hayo mshambuliaji huyu wa kidachi alionekana kuw ana matatizo ya majeruhi mara kwa mara huku akiwa na tatizo la Goti na henka vitu vilivyo msumbua kila mwezi.

 

Van Persie aliweza kuonyesha uwezo wa hali ya juu katika timu yake ya Tiafa kuanzia mkwa 2006 katika mashindano ya kuwania kufuzu fainali za kombe la Dunia mara baada ya kushinda mechi dhidi ya Roamania na Finland.
Pia aliweza kucheza mechi zote nne katika fainali za kombe la Dunia 2006 kama kiungo wa kutumainiwa wa Uholanzi ,pindi timu hiyo ilipopangwa na timu ngumu kama Argentina na Ivory Coast.    
Miaka miwili badae katika michuano ya Euro 2008, Van Persie alifanikiwa kushinda magoli mawili na kuifanya timu hiyo kutinga atua ya robo fainali kabla ya kutolewa na Urusi.  .
Akiwa anacheza kama winga na mshambuliaji katika timu yake ya Taifa  , Van Persie alioweza kupewa heshima ya hali ya juu na mashabiki wa mpira wan chi hiyo hasa kwa ufundi wake wa kutengeneza magoli akiwa na klabua yake na timu ya Taifa .
Haliweza kuisadia timuyake kutinga hatua ya fainali katika michuano ya kombe la Dunia ya mwaka  2010 kabala ya kufungwa na mabingwa wa kombe hilo kwa sasa Hispania na laiweza kufunga bao moja katika michuano hiyo bao alilofunga kwenye mechi dhini ya Cameroon.
Mchezaji huyu ambaye ameonekana kufanya makubwa katika msimu huu uliomalizika katika ligi kuu ya uingereza kwa kuweza kutwa tuzo ya kiatu cha dhahabu tuzo ambayo ajawahi kuipata maishani mwake.

Van persie ambaye ameweza kufunga mabao 30katika msimu huu na kufikia rekodi iliyowekjwa katika klabu ya Arsenal na mkongwe Thierry Henry msimu wa 2003/04 na pia aliweza kutwa tuzo ya mchezaji bora wa mwaka tuzo inayotolewa na chama cha waandishi wa habari nchini Uingereza.

Hata hivyo yeye ajaonyesha nia ya kuhama klabu yake ya Arsenal licha ya dau nono alilotangaziwa na Man City huku wakala wake akimshawishi kukubalina na hofa hiyo ambayo ni mara tatu ya mkataba wake wa awali.



No comments:

Post a Comment