Wednesday, August 24, 2011

*VODACM YATOA FURSA KWA WATANZANIA KUWAPIGIA KURA WASHIRIKI WA VODACM MISS TANZANIA

Kampuni ya mawasiliano ya Vodacom, Tanzania imetoa fursa kwa Watanzania kuweza kupiga kura na kuchagua mrembo anayevutia zaidi kati ya warembo 30 wanaoshiriki  shindano la kumsaka Vodacom Miss Tanzania 2011.

Akizungumza na waandishi wa habari, Mkuu wa Udhamini wa Vodacom ,George Rwehumbiza, alisema ili kupiga kura Watanzania watatakiwa kutuma ujumbe mfupi wa maneno wenye neno MREMBO ukifuatiwa na namba ya mshiriki 'mfano  40'  kwenda 15550 ambapo gharama kwa kila ujumbe ni shilingi 150 tu .

Aidha Rwehumbiza, aliongeza kuwa kila ujumbe mfupi utakaotumwa utampatia Mtanzania pointi 10 ambapo wateja 20 watakaobahatika kuwa na pointi nyingi zaidi kila mmoja atajipatia TIKETI mbili za VIP zitakazomwezesha kwenda kushuhudia fainali ya shindano la Vodacom Miss Tanzania 2011, itakayofanyika tarehe 10 mwezi septemba katika ukumbi wa  Mlimani city jijini Dares salaam.

Pia kwa wale watakaohitaji kutoa maoni au mitazamo yao mbalimbali kuhusu Vodacom Miss Tanzania watapata fursa ya kutuma ujumbe mfupi wa maneno wenye neno MREMBO ukifuatiwa na maoni kwenda namba 15550.

Akisisitiza hili  Rwehumbiza, alisema ili kuwafahamu warembo wanaoshindania taji la Vodacom Miss Tanzania 2011, Watanzania wote wanaweza kuangalia kituo cha Televisheni cha STAR TV leo kuanzia muda wa saa moja jioni pamoja na CLOUDS TV muda wa saa tatu usiku kila siku pia soma magazeti ya Mtanzania, The African, Dimba, Rai na Bingwa.
.

No comments:

Post a Comment