Friday, August 19, 2011

Kuna Taarifa Za Ki-Intelijensia; Gaddafi Kuikimbia Libya Siku Chache Zijazo

| Friday, August 19, 2011

Kwa mujibu wa taarifa za Kiintelijensia zilizoripotiwa na Televisheni  ya NBC ya Marekani. Kanali Muammar
Gaddafi anapanga kuikimbia Tripoli akiwa na familia yake. Huenda akakimbilia Tunisia. Hii inatokana na matukio ya hivi karibuni kwenye medani ya kijeshi ambapo Gaddafi ameupoteza mji muhimu ki mkakati . Ni mji wa Zawiyah unaonekana pichani chini ambao sasa unapepea bendera ya Libya ya kabla ya ujio wa Gaddafi. Kutoka Zawiyah, vikosi vinavyopambana na Gaddafi sasa vimebaki na Tripoli kama target. Kuanguka kwa Zawiyah kutoka mikononi mwa Gaddafi kunaweza kuchochea  maasi  zaidi ndani ya jeshi la Gaddafi na hata kuwatia moyo Walibya walioko Tripoli kuamka na kumpinga Gaddafi wazi wazi. Na tusubiri tuone.

No comments:

Post a Comment