Tuesday, September 13, 2011

WAANDISHI WAFANYA ZIARA KWENEYE NDEGE

Bw.Abdul Aziz Alhai Kulia akizungumza na wandishi wa habari
yake  Dubai, leo imekuwa mwenyeji  wa wawakilishi kutoka vyombo mbalimbali vya habari na mawakala wa usafiri katika kuwafahamisha huduma zake na shughuli wazifanyazo  Tanzania.
Akizungumza baada ya ziara ya ndege ya
Emirates wenyeji wa wadau wa usafiri Tanzania
DAR ES SALAAM, TANZANIA: Sept 13, 2011: kampuni ya Emirates ya kimataifa yenye makao Emirates katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere ' Meneja wa Emirates bwana  Abdul Aziz Al Hai alisema ziara ilikuwa na nia ya kuleta uzoefu wa Emirates na ukarimu wake  kwa wakala wa usafiri na wanahabari, kama wadau wakuu wa biashara ya usafiri wa anga. 
Ziara hii ni muhimu kwetu kwani tunataka kujenga mahusiano  na washirika wetu wa kibiashara na vyombo vya habari hapa nchini Tanzania. Kwa uzoefu wa ndege za  Emirates na bidhaa zake zenye ubora na kupata kujua ubora wa huduma zetu ambazo tungependa wakala wa usafiri  na vyombo vya habari  hapa Tanzania kuufahamu ubora wa bidhaa  zetu” alisema Al Hai. 
Aliendelea kusema: “Emirates, tunaendelea kutafuta njia mpya za kufanya kazi na washirika wetu ili kuboresha huduma zetu kwa wateja wetu. kwakuwa tunafanya kazi na  mawakala wa usafiri tunataka wateja wetu kuwa na uzoefu mzuri na  Emirates kuanzia wanaponunua tiketi kwao. Pia tunatambua mchango wa vyombo vya habari ulioutoa na unaoendelea kuutoa  kwa kuujulisha umma kuhusu biashara zetu hapa Tanzania”.  
Bwana Al Hai alibainisha kwamba tangu Emirates imeanza shughuli zake hapa Tanzania, biashara ya usafiri wa anga  imekuwa ikiongezeka, na kuongeza kuwa Tanzania ni soko muhimu kwa Emirates katika kanda ya Afrika Mashariki.
“Tumeona ukuaji mkubwa hapa  Tanzania ambapo umeongeza mapato ya Emirates katika kanda ya Afrika Mashariki. Kufanya kazi na mawakala wa usafiri katika vituo vyote ambapo nguvu ya kusafiri kwetu kunaendana  na ubora wa Emirates unaotoa kwa raia wa nchi hii,” alisema.
Aliongezeakwa kusema  ahadi ya Emirates kwa utoaji wa huduma zenye viwango vya juu umeonekana kwenye tuzo 400 za ubora wa kimataifa iliyozipata  tokea ilipoanza huduma zake miaka 25 iliyopita.
Bwana Al Hai pia alibainisha kwamba Emirates imeorodhesha idadi ya ofa maalumu kwa wasafiri wa Tanzania,kuanzia kifurushi cha kituo cha Dubai  mpaka Summer Smiles, na vimebuniwa kusaidia familia kukutana pamoja na kufurahia ubora unaotolewa na Dubai.


“Kwa sasa Dubai ni sehemu yenye punguzo la pekee kuliko sehemu nyingine yoyote.Taarifa ya fedha tuliyorekodi mwaka jana imetusaidia kuanzisha mipango yakinifu.Thamani Ya wateja wetu wa Tanzania inatazamia kuleta ofa maalumu kwa miezi michache ijayo,” alisema

Emirates ni moja ya mashirika ya ndege yanayokua kwa kasi duniani  ambapo kwa sasa inatoa huduma kwa vituo 114 katika nchi 67, ripoti ya mwaka wa fedha iliyopita inaonyesha faida kamili ni dola milioni 964 kwa ongezeko la idadi ya abiria.Ndege  imebeba abiria milioni 31.4 kwa mwaka 2010 -2011 mpaka asilimia 14.5 kuanzia mwaka 2009-2010 na tani milioni  1.8 za mizigo, mpaka asilimia 11.8 katika kipindi hicho.
“Mafanikio yetu yametokana na dhamira yetu ya kuongoza sekta hii kwa ubunifu. Tunafanya mambo kwa utofauti. Tunaelewa umuhimu wa kuendelea kuwa wabunifu katika kutimiza mahitaji wa wateja wetu.Hii imetuwezesha sisi kuwa mstari wa mbele katika soko na tunatazamia maendeleo mapya kwa mwaka huu kutoka kwenu kama washirika wetu,” alisema.
Shirika hili la ndege  lilianza kutoa huduma zake hapa Tanzania mwaka 1997 na sasa linatoa huduma za kila siku katika kiwanja cha kimataifa cha  Mwalimu Julius Nyerere na Dubai

……….End……….

No comments:

Post a Comment