Rio Ferdinand Beki aliyetoswa Euro 2012 kwa
fitina
Godlisten Shao na
Mashirika ya Habari.
SIKU ya tarehe 22 Julai mwaka
2002,Rio
Ferdinand alijiunga na klabu ya , Manchester United, kw amkataba wa miaka
mitano na kuwa mchezaji ghali aneyecheza safu ya nyuma katika historia ya
uingereza , akichukua nafasi ya beki
aliyekuwa ghali kipindi cha mwaka 2001 Lilian Thuram.
Ferdinand ambaye ni raia wa uingereza alizaliwa Novemba
7, 1978 katika kitongoji cha
Peckham, mjini London, nchini England,na ni
mchezaji anayecheza nafasi ya nyuma katika klabu ya Manchester United mpaka
sasa na amekuwa mchezaji wa kulipwa kuanzia mwaka 1997.
Beki huyo ambaye alihamishwa kwa ada ya pauni milioni ishirini za uingereza
na kuifanya klabu yake ya awali ya leeds kumtangaza kuwa inamuuza mchezaji huyo
kwa ka zaidi ya pauni milioni thelasini.
Leeds United baadae ilichukua kiasi
hicho chapesa zake za awali kama na kusaidia timu hiyo ambayo ilikuwa na tatizo
la kiuchumi kipindio hicho, na kufanya Ada
kamili ya kumuhamisha mchezaji huyo kwenda Manchester United kuwa Pauni milioni
33.
Ferdinand ambaye alionekana ayuko
vizuri kimchezo mara baaday kucheza chini ya kiwango katika mchezo wa klabu
bingwa barani ulaya mchezo uliozikutanisha timu ya
Manchester United na Real Madrid
Mwaka
2003, alishindwa kufika
mahabara kwa ajili ya vipimo vya kugundua kama
anatumia dawa za kuongeza nguvu au lah ,hali hii ilimtokea pale aliposahau
kutokana nakuwa na harakati nyingi za kuhama makazi yake ya zamani nakuhamia
makazi mapya na baadae kuendelea na shughuli zake zingine.
Hali iliyosabaisha kamati ya nidhamu
ya chama cha soka nchini Uingereza
FA kumtoza
faini ya kutocheza msimu mzima wa ligi na klabu yake kulipa faini ya Pauni
50,000.
Hari ilifanya klabu yake Manchester United
kukata rufaa kw amadai ya kuwa ameonewa kwani mchezaji mwengine kutoka Manchester City ,Christian Negouai, alitozwa faini
ya Pauni 2,000 kwa kutokwenda kupima.
Ingawa ,Rais wa
FIFA Sepp Blatter alitupilia
mbali rufaa hiyo kwa kusema kosa la Ferdinand alifanani na la Negouai ambaye
yeye alichelewa kupima kwa sabau ya tatizo la foleni ya magari hivyo alionesha
nia ya kutaka kwenda kupima wakti yeye aligoma kwenda kupima kwa sabau zake
binafsi nakumuongeze aadhabu ya miezi 12 mingine.
Ferdinand ambaye aliweza kutwa taji la ubingwa wa ligi ku kwa mara ya kwanza
akiwa na klabu ya Manchester
United na kupata medali ya
Carling Cup
2006, na kufuatiwa ushidi wa pili katika kipindi cha 2003 na
2005 FA Cup.
Mnamo 14 Desemba
2005, katika mchezo
dhidi ya Wigan Athletic, Ferdinand aliweza kushinda bao lake la kwanza akiwa na
United , katika mchezo ambao walishinda bao
4–0 . hili lilikuwa goli la kwanza mara baadaya mika mitatu akiwa
Old Trafford.
Baadae akafuatiwa na goli la nguvu la kichwa amabalo alifunga wakati wa mechi
dhidi ya
West Bromwich Albion.na baade
akafunga bao dakika za mwisho katika mchezo dhidi ya mahasimu wao
Liverpool mchezo uliopigwa katika dimba la
Old Trafford,na ndio lilikuwa goli muhimu kwa
United mpaka leo .
Baada ya kuonyesha kiwango kikubwa katika ligi aliweza kuchaguliwa kwenye
kikosi bora cha msimu wa ligi kuu ya uingereza cha mwaka
2006–07.
Ferdinand alianza vizuri msimu wa ligi wa
2007–08, kuwa kati ya mabeki wakutegemewa wa Man United ukilinganisha na
hap awali alipojiunga na klabu hiyo na kuweza kupachika bao lake la kwanza la
msimu katika mechi dhidi ya Aston Vila mchezo uliopigwa,20 Octoba 2007 katika
dimba la Vila
park.
Katika michuano ya
FA Cup mchezo wa
robo fainali uliochezwa ,8marchi dhiodi ya Portsmouth, Ferdinand aliweza kukaa golini
kma Golikipa baada ya kipa tegemezi wa klabu hiyo Edwin van der Sar kutoka
uwanajani mara baada ya kuptwa namajeraha kwani kipindi hicho kipa wa akiba,Tomasz
Kuszczak, kufungwa kwa penati na kupelekea kutolewa katika michuano ya FA CUP.
Mnamo
6 April 2008, kweney mchezo
dhidi ya Middlesbrough, Ferdinand alitolewa
nje kwa matatizo aliyoyapata kwenye mguu . hali hiyo ilimfanya kukosa mchezo
war obo fainali ya UEFA ambao ulipigwa 9 april 2008
dhidi ya
A.S. Roma.
Baada ya United' kufungwa bao 2–1 na
Chelsea katika mchezo wa
ligi kuu
April 2008 Ferdinand, aliweza
kuwa na hasira kutokana na kichapo hicho na kutoamaini kuwa timu hiyo ingeweza
kupenya kwenye ukuta wa United
.
Licha ya kuhusishw ana uvumi wa kuhamia klabu ya Barcelona ya nchini ,Hispania
tarehe 16 April 2008 kati ya
Michael Carrick na
Wes Brown, Ferdinand kw apamoja walikubaliana
kusaini mkataba mwingine wa miaka mitano kuendelea kucheza United
mkataba amabo uligharimu Pauni milioni 130,000
kwa wiki na mkataba huo utamuweka mchezaji huyo katika timu hiyo ya mashetani
wekundu mpaka 2013,mkataba amabao ulisainiwa15 Mei 2008.
Baada ya hapo tarehe
21 Mei 2008,
Ferdinand alitajwa kuwa kama nahodha mpya
Manchester United
katika mchezo wa klabu
bingwa barani ulaya mchezo uliwazikutanisha Manchester United na
Chelsea. Na kufanikiwa kuchukua kombe akiwa na
wachzaji wakongwe kama
Ryan Giggs, na
Gary Neville.
Ferdinand ambaye kwa sasa ataweza kuwemo kwenye kikosi cha uingereza kinacho
shiriki michuano ya Euro 2012 kutokana kocha mpya wa timu hiyo Roy
Hodgson kuhofia timu kushindwa kufanya vizuri katika
safu ya nyuma kutokana wailihao kuwa katika ugomvi wa muda mrefu.
Hata hivyo mchezaji huyo ajazungumzia
chochote ju ya mahamuzi ya meneja huyo mpya ambaye ameonekana kutegua kiwango
hicho.
mwishooo
Robin
van Persie mkali anayesubiriwa kwa hamu Man City
Godlistern
Shao na Mashirika ya habari
Mashabiki wengi wa klabu ya
Arsenal
wamekuwa wakimuona mshambuliaji wa Klabu hiyo Robin van Persie
kuwa ni mchezaji wa kudumu katika klabu hiyo
tangu aliposaini kuchezea klabu hiyo mwaka 2004 na ni mbadala wa mshambuliaji
wa kidachi
Dennis Bergkamp ambaye
alitandika daluga katika masuala ya soka
Ingawa mshambuliaji huyo amekuwa akisumbuliwa na majeruhi kadhaa marakwa
mara kiasi cha kufanya mshambuliaji huyo kucheza kwa kiwango kilichodhaniwa
pindi alipokuwa kijiunga na washika bunduki hao wa London.
Pamoja namatatizo yote
yaliyomkuta mchezaji van Persie
bado ameonekana kuweka mguu wake kuwa ndio biashara pekee katika maisha yake
mara baada ya kuwa mshambuliaji wa kutumainiwa peke yake
akichukua nafasi ya Emmanuel Adebayor ambaye aliondoka The Gunners na kwenda
kujiunga na Man City.
Robin
van Persie amabye ni raia wakidachi alizaliwa Agosti 6,1983 katika Mji wa Rotterdam nchini
Uholanzi ambako ndiko alikulia na maisha
yake mpira yalipoanzia.
Van
Parse amabye kwa sasa anaicheze kalabu ya Arsenala huku akiwa amebakiza mwaka
mmoja kumalizika kwa mkataba wake amekuwa yuko njia panda mraa baada ya
Mabingwa wapya wa ligi kuu ya Uingereza
Man City
kumtangazia dau la kung’oa katika klabu hiyo.
Kabala
ya kuchezea Arsenal Van Parsie alipata kuchezea klabu ya Feyenoord ya nchini
Uolanzi kwa kipindi cha miaka mine kuanzia 2001 hadi 2004 na baade kujiunga na
washika bunduki wa London.
Van Persie ambaye alikimbia kutoka kwenye familiya yao amabpo kipindi hicho
mama yake alikuwa anafanya kazi ya kupaka rangi na baba yake alikuwa mchongaji
wa vinyago huko Uholanzi
Akiwa na umri wa miaka
14 alijiunga
na timu ya vijana ya Uholanzi lakini baade alichwa na timu hiyo kutokana na
kushindwa kuelewana na makocha wake na kuendelea kubaki kuichezea klabu yake ya
Feyenoord.
Baadae alionekana kuwa na kiwango cha hari ya juu na kuwa mchezaji wa kuanza
katika kikosi cha kwanza cha Feyenoord kutokana na matatizo ya kumia
marakwamara yalimfanya awe mtu wa kuanzia kikosi
B.
Ingawa watu wengi waliamini kuwa Van Persie
amegombana na kocha wake
Bert van Marwijk ndio sababu ya kumfanya
mchezaji wa akiba katika ,pia kocha aliweza kumrejesha mchezaji huyo nyumbani
mara baada ya kuonyesha utovu wa nidhamu katika mchezo wa fainali za UEFA mwaka
2003 dhidi ya Real Madrid. .
Baada ya kufanikiwa kupachika magoli
nane katika msimu wa kwanza huku akitokea benchi aliweza kumshawishi kocha wake
katika msimu uliofuata wa mwaka 2003-2004 kuwa ndie mchezaji anayeweza kuanza.
Baada ya kucheza kweney klabu hiyo bil;a kuwa na mafanikio yoyote nyota huyo
aliweza kuuzwa katika klabu ya Arsenal ambayo alionyesha kuwa na mapenzi nayo
siku za nyuma kabla ya kuuzwa katika klabu hiyo.
Mwaka 2004 Van Persie aliweza kusaini mkataba wa miaka mine
na klabu ya Arsenal na kufanikiwa kuwa
mmoja wa wachezaji waliocheza katika kikosi kilichochukua kombe la FA mwaka
2005 kombe ambalo alijaweza kuchukuliwa tena na klabau hiyo.
Mara baada ya mkataba wake kumalizika mwaka 2009
mshambuliaji huyo aliweza kumshawishi bosi wake Arsene Wanger kumpa mkataba
mpya wa miaka minne ambao utamalizika
mwakani
Mshambuliaji huyo ambaye aliweza
kumfurahisha bosi wake pindi alipokuwa uwanjani kutokana na stairi yake ya mchezo
lakini alikuja kujitia doa pale alipopatiw akadi nyekundu kwenye mechi kati ya
Arsenal na Southampton.
Maisha yalibadilika na kuw amtu
mwneye furaha akiwa na Gunners pale alipoweza kufunga goli pekee la kichwa na
kupewa tuzo kuwa goli pekee la msimu katika ligi kuu ya England.
Mshambuliaji huyu ambaye alikuwa
kaichez anafasi ya winga lakini alicaha jkucheza nafasi hiyo mara baada ya
kubadilishwa na kocha wake Arsene Wanger mara baada ya kuona kuwa awezi kufua
dafu mbele ya Thierry Henry ambaye alikuwa katika kiwango cha juu sana.
Licha ya kuwa na mafanikio yote hayo
mshambuliaji huyu wa kidachi alionekana kuw ana matatizo ya majeruhi mara kwa
mara huku akiwa na tatizo la Goti na henka vitu vilivyo msumbua kila mwezi.
Van Persie aliweza kuonyesha uwezo wa hali ya juu katika
timu yake ya Tiafa kuanzia mkwa 2006 katika mashindano ya kuwania kufuzu
fainali za kombe la Dunia mara baada ya kushinda mechi dhidi ya Roamania na Finland.
Pia aliweza kucheza mechi zote nne katika fainali za kombe la Dunia 2006
kama kiungo wa kutumainiwa wa Uholanzi ,pindi timu hiyo ilipopangwa na timu
ngumu kama Argentina na Ivory Coast.
Miaka miwili badae katika michuano ya Euro 2008, Van Persie alifanikiwa
kushinda magoli mawili na kuifanya timu hiyo kutinga atua ya robo fainali kabla
ya kutolewa na Urusi.
.
Akiwa anacheza kama winga na mshambuliaji katika timu yake ya Taifa
, Van Persie alioweza kupewa heshima ya hali
ya juu na mashabiki wa mpira wan chi hiyo hasa kwa ufundi wake wa kutengeneza
magoli akiwa na klabua yake na timu ya Taifa .
Haliweza kuisadia timuyake kutinga hatua ya fainali katika michuano ya kombe
la Dunia ya mwaka
2010 kabala ya
kufungwa na mabingwa wa kombe hilo kwa sasa
Hispania na laiweza kufunga bao moja katika michuano hiyo bao alilofunga kwenye
mechi dhini ya Cameroon.
Mchezaji huyu ambaye ameonekana kufanya makubwa katika msimu
huu uliomalizika katika ligi kuu ya uingereza kwa kuweza kutwa tuzo ya kiatu
cha dhahabu tuzo ambayo ajawahi kuipata maishani mwake.
Van persie ambaye ameweza kufunga mabao 30katika msimu huu
na kufikia rekodi iliyowekjwa katika klabu ya Arsenal na mkongwe Thierry Henry
msimu wa 2003/04 na pia aliweza kutwa tuzo ya mchezaji bora wa mwaka tuzo
inayotolewa na chama cha waandishi wa habari nchini Uingereza.
Hata hivyo yeye ajaonyesha nia ya kuhama klabu yake ya
Arsenal licha ya dau nono alilotangaziwa na Man City
huku wakala wake akimshawishi kukubalina na hofa hiyo ambayo ni mara tatu ya
mkataba wake wa awali.