Monday, November 21, 2011

Makamu Waziri wa Biashara wa Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China Mheshimiwa Jiang Yaoping(kulia) akitoa zawadi kwa  Waziri wa Fedha Mustafa Mkulo (kushoto ) jana jijini Dar es salaam mara baada ya kutia saini   hati ya mikataba mitatu(3 )ya mikopo isiyo na riba yenye thamani ya Dola za Kimarekani milioni 89.8 na barua ya msaada wa ujenzi wa Kituo cha Mikutano cha Mwalimu Nyerere kwa thamani ya Dola milioni 5.6  jana jijini Dar es salaam .
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Mandeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe, akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maadhimio ya Kamati kuu ya chama hicho moja wapo kwenda kumuona Rais Jakaya Kikwete kuhusu muswada wa katiba. Mazungumzo hayo yalifanyika makao Makuu ya Chama hicho Dar es Salaam jana. (Wengine katika picha toka kushoto) ni Makamu Mwenyekiti wa Chama hicho zanzibarSaid Issa Mohamed na Katibu Mkuu wa Chamam hicho Dk. Willbroad Slaa
Wajumbe wa Kikao cha cha Kamati Kuu cha Chama  cha Mapinduzi   wamesimama  kwa ajili ya kuwakalibisha viongozi wa ngazi za juu wa chama hicho walipokuwa wakiingia ukumbini kwa ajili ya  kufunguliwa na Mwenyekiti wake , Jakaya Kikwete.

Sunday, November 13, 2011

STAR TIMES YATEMBELEWA NA MJUMBE WA KAMATI KUU TOKA CHINA


Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Kikomunisti cha China Bw. Liu Yunshan kulia akipata maelezo
akiangalia mitambo ya kurusha matangazo ya Kampuni ya Star Media
Wafanyakazi wa kituo cha StarTimes wakisubiri kumpokea Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Kikomunisti cha China Bw. Liu Yunshan baada ya kuwasili nchini kwa mwaliko wa Chama cha Mapinduzi Dar es Salaam juzi
Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Kikomunisti cha China Bw. Liu Yunshan kulia akielekezwa Mitambo ya Star Times na Ofisa Mtendaji Mkuu. William Lan inavyofanya kazi alipotembelea

Thursday, November 10, 2011

 VIJANA WA TEYODEN AMBAO WALIOSHIRIKI TAMASHA MABADIKO YA TABIA NCHI LILOFANYIKA KATIKA VIWANJA VYA DONBOSCO UPANGA
 EDUARD MAGIGE ,ANETH ANANIA WAKIFUATILIA KWA MAKINI MADA ZILIZO KUWA ZIKITOLEWA KATIKA TAMASHA LA VIJANA.
BAADHI YA VIJANA WAKIWA KATIKA PICHA YA PAMOJA NA MAKAMU WA RAIS WA TANZANIA DK.GHARIB BILAL.(PICHA ZOTE KWA  HISANI YA TEYODEN)

Tuesday, November 8, 2011


ARUSHA KIMENUKA WAFUASI WA CHADEMA WATAWANYWA KWA MABOMU

Wafuasi wa CHADEMA wakiwa nje ya Mahakama jijini Arusha leo.

NA Mwandishi Wetu, Arusha
ASKARI wa kutuliza ghasi wa mkoani Arusha wamewatawanya wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kwa Mabomu yaliyorindima katikati ya Jiji la Arusha kuanzia saa 11 Asubuhi baada ya wanachama na wapenzi wa chama hicho kufanya mkesha huku waliwasha moto wa matairi na wengine wakiyashambulia magari jambo lililowafanya Polisi kuchukua maamuzi magumu kwa kuwatawanya wafuasi hao kwa  mabomu ya machozi na baadhi ya viongozi wa chama hicho kushikiliwa na polisi akiwamo katibu mkuu wa chama hicho, Wilbroad Slaa .
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, Kamanda wa polisi mkoa wa Arusha, Akili Mpwapwa, alisema kuwa walifanyakazi ya ziada kuwatawanya wafuasi hao waliokuwa wamedhamiria kuvunja vioo vya magari na kuharibu mali za raia pamoja na uvunjifu wa amani kwa raia waliokuwa wanapita kwenye maeneo ya karibu na maeneo ya uwanja huo.
"Kwa bahati mbaya wakati tukiwakamata baadhi ya wahusika, Mwenyekiti wa Chama hicho, aliingia mitingi na kutokomea kusikojulikana" alisema Kamanda
Hali si shwari nje viwanja vya mahakama ilikuwa ni ya vurugu na kelele hadi mwenyekiti wa chama hicho alipowaamuru kukutana viwanja vya NMC na ndipo kukawa na hali shwari na shughuli za mahakama kuendelea kama kawaida kulikohanikizwa na kelele za people power.

STARS HIYO NDJAMENA

 
STARS KWENDA N’DJAMENA KESHO
Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) inatarajia kuondoka kesho (Novemba 9 mwaka huu) saa 9 alasiri kwa ndege ya Kenya Airways kwenda N’Djamena kwa ajili ya mechi ya kwanza ya mchujo ya Kombe la Dunia dhidi ya Chad itakayochezwa Novemba 11 mwaka huu.
 
Msafara wa Stars wenye watu 40 ukiongozwa na Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya TFF, Eliud Mvella utawasili N’Djamena kesho hiyo hiyo saa 1.15 usiku kwa saa za huko ambapo kwa hapa nyumbani ni saa 3.15 usiku.
 
Wachezaji katika msafara huo watakuwa wote 21 walioko kambini, watu sita kutoka Benchi la Ufundi wakiongozwa na Kocha Jan Poulsen, wajumbe wawili wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT) na washabiki.
 
Stars ambayo iliagwa jana saa 1 usiku kwa kukabidhiwa bendera na Mwenyekiti wa BMT, Dioniz Malinzi itarejea nchini Novemba 13 mwaka huu saa 7.25 mchana kwa ndege ya Ethiopian Airlines na kwenda moja kwa moja kambini New Africa Hotel kujiandaa kwa mechi ya marudiano itakayochezwa Novemba 15 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
 
MICHUANO YA UHAI CUP 2011
Timu 15 zinazoshiriki michuano ya mwaka huu ya Kombe la Uhai zimepangwa katika makundi matatu ambapo mechi zitachezwa katika viwanja viwili; Uwanja wa Karume na Uwanja wa Azam ulioko Chamazi, Mbande.
 
Mashindano hayo yanashirikisha timu zenye umri chini ya miaka 20 za klabu zote 14 za Ligi Kuu ya Vodacom wakati timu mwalikwa mwaka huu ni timu ya Taifa kwa vijana wenye umri chini ya miaka 17 (Serengeti Boys).
 
Mabingwa watetezi Ruvu Shooting Stars ndiyo wanaoongoza kundi A katika michuano hiyo inayodhaminiwa na Kampuni ya Said Salim Bakhresa kupitia bidhaa yake ya maji Uhai. Timu nyingine katika kundi hilo ni Oljoro JKT, Kagera Sugar, Azam na Mtibwa Sugar.
 
Kundi B lina timu za JKT Ruvu Stars, Polisi Dodoma, Moro United, Yanga na Villa Squad wakati kundi C ni Simba, Coastal Union, Toto Africans, African Lyon na Serengeti Boys. Mbali ya sh. milioni moja za maandalizi kwa kila timu, mdhamini pia anatoa zawadi kwa washindi watatu wa kwanza, mchezaji bora, mfungaji bora, timu yenye nidhamu na nauli za kuja Dar es Salaam na kurudi kwa timu kutoka mikoani.
 
Campaign Against Malaria yenyewe inatoa seti moja ya jezi kwa kila timu inayoshiriki mashindano hayo ambayo yataanza Novemba 12 na kumalizika Novemba 13 mwaka huu.
 
Kila siku kutakuwa na mechi tatu katika kila uwanja. Siku ya ufunguzi Toto Africans itacheza na Serengeti Boys saa 3 asubuhi Uwanja wa Karume, Ruvu Shooting Stars vs Oljoro JKT (saa 8 mchana- Karume) na Kagera Sugar vs Azam (saa 10 jioni- Karume).
Simba vs Coastal Union (saa 3 asubuhi- Chamazi), JKT Ruvu Stars vs Polisi Dodoma (saa 8 mchana- Chamazi) na Moro United vs Yanga (saa 10 jioni- Chamazi).
 

*RUFANI YA MICHAEL WAMBURA

Kamati ya Nidhamu na Usuluhishi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imesema haina mamlaka (jurisdiction) ya kusikiliza shauri lililowasilishwa mbele yake na aliyekuwa mgombea uenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Mara (FAM), Michael Richard Wambura.
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa kamati hiyo, Kamishna Mstaafu wa Polisi Alfred Tibaigana, Wambura aliwasilisha rufani mbele yao akipinga uamuzi wa Kamati ya Uchaguzi ya TFF kumuengua kugombea uongozi katika chama hicho.
Tibaigana alisema Kamati yake ambayo ina wajumbe saba, kabla ya kusikiliza shauri hilo ilitaka kwanza kujua kama ina mamlaka (jurisdiction) hayo. Kamati ilizitaka pande zote (bothi parties)- mlalamikaji na mlalamikiwa kueleza kama ina jurisdiction au la.
Mwanasheria wa Wambura, Audax Kahendaguza aliwasilisha hoja zake za kwa nini anadhani Kamati ina mamlaka ya kusikiliza shauri hilo wakati Katibu Mkuu wa TFF, Angetile Osiah alieleza kwa nini anaamini Kamati hiyo haina mamlaka hayo.
Baada ya hapo, Kamati ilizitoa nje pande zote mbili na baadaye kufanya uamuzi. Uamuzi wa Kamati kuwa haina mamlaka hayo ulikariri Ibara ya 12(4) ya Kanuni za Uchaguzi za wanachama wa TFF inayosema: “The decisions of the TFF Elections Committee are final and conclusive and shall not be monitored by any body.”
STARS KWENDA N’DJAMENA KESHO
Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) inatarajia kuondoka kesho (Novemba 9 mwaka huu) saa 9 alasiri kwa ndege ya Kenya Airways kwenda N’Djamena kwa ajili ya mechi ya kwanza ya mchujo ya Kombe la Dunia dhidi ya Chad itakayochezwa Novemba 11 mwaka huu.
Msafara wa Stars wenye watu 40 ukiongozwa na Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya TFF, Eliud Mvella utawasili N’Djamena kesho hiyo hiyo saa 1.15 usiku kwa saa za huko ambapo kwa hapa nyumbani ni saa 3.15 usiku.
Wachezaji katika msafara huo watakuwa wote 21 walioko kambini, watu sita kutoka Benchi la Ufundi wakiongozwa na Kocha Jan Poulsen, wajumbe wawili wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT) na washabiki.
Stars ambayo iliagwa jana saa 1 usiku kwa kukabidhiwa bendera na Mwenyekiti wa BMT, Dioniz Malinzi itarejea nchini Novemba 13 mwaka huu saa 7.25 mchana kwa ndege ya Ethiopian Airlines na kwenda moja kwa moja kambini New Africa Hotel kujiandaa kwa mechi ya marudiano itakayochezwa Novemba 15 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
MICHUANO YA UHAI CUP 2011
Timu 15 zinazoshiriki michuano ya mwaka huu ya Kombe la Uhai zimepangwa katika makundi matatu ambapo mechi zitachezwa katika viwanja viwili; Uwanja wa Karume na Uwanja wa Azam ulioko Chamazi, Mbande.
Mashindano hayo yanashirikisha timu zenye umri chini ya miaka 20 za klabu zote 14 za Ligi Kuu ya Vodacom wakati timu mwalikwa mwaka huu ni timu ya Taifa kwa vijana wenye umri chini ya miaka 17 (Serengeti Boys).
Mabingwa watetezi Ruvu Shooting Stars ndiyo wanaoongoza kundi A katika michuano hiyo inayodhaminiwa na Kampuni ya Said Salim Bakhresa kupitia bidhaa yake ya maji Uhai. Timu nyingine katika kundi hilo ni Oljoro JKT, Kagera Sugar, Azam na Mtibwa Sugar.
Kundi B lina timu za JKT Ruvu Stars, Polisi Dodoma, Moro United, Yanga na Villa Squad wakati kundi C ni Simba, Coastal Union, Toto Africans, African Lyon na Serengeti Boys. Mbali ya sh. milioni moja za maandalizi kwa kila timu, mdhamini pia anatoa zawadi kwa washindi watatu wa kwanza, mchezaji bora, mfungaji bora, timu yenye nidhamu na nauli za kuja Dar es Salaam na kurudi kwa timu kutoka mikoani.
Campaign Against Malaria yenyewe inatoa seti moja ya jezi kwa kila timu inayoshiriki mashindano hayo ambayo yataanza Novemba 12 na kumalizika Novemba 13 mwaka huu.
Kila siku kutakuwa na mechi tatu katika kila uwanja. Siku ya ufunguzi Toto Africans itacheza na Serengeti Boys saa 3 asubuhi Uwanja wa Karume, Ruvu Shooting Stars vs Oljoro JKT (saa 8 mchana- Karume) na Kagera Sugar vs Azam (saa 10 jioni- Karume).
Simba vs Coastal Union (saa 3 asubuhi- Chamazi), JKT Ruvu Stars vs Polisi Dodoma (saa 8 mchana- Chamazi) na Moro United vs Yanga (saa 10 jioni- Chamazi).
Powered by Sorec
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

Thursday, November 3, 2011

BONDIA ALAN KAMOTE KUMVAA MKENYA JUMAPILI

Rais wa Oganaizesheni ya ngumi za kulipwa Tanzania , Yasin Abdallah , amesema  novemba 6 mwaka huu bondia machachali kutoka Tanga Allan Kamote atapambana na bondia Fredrick Nyakesa kutoka kenya katika mpambano wa kimataifa wa kirafiki utakaofanyika katika ukumbi wa Ridoch mkoa wa Tanga na mabondia hawo watapambana katika pambano la raundi 8 la uzito wa kilogram 61.2 light weigth yasin alisema kutakua na mapambano ya utangulizi mengine yatakayowakutanisha mabondia kutoka tanga na Dar es salaam

Katika Mchezo huo kutakua na DVD za mafunzo ya mchezo wa ngumi pamoja na kutambua sheria zake mbalimbali zitakazokua zikisambazwa na kocha wa mchezo huo Rajabu Mhamila 'Super D Boxing Coach' kwa ajili ya kuwapa mambondia mbalimbali mbinu za mchezo na mashabiki kujua sheria za masumbwi.

Super D alisema katika DVD hizo kutakuwa na mapambano mengi ambayo yanaweza kutumika kama mafunzo muhimu kwa mabondia ,makocha marefa pamoja na mashabiki wa mchezo kujua sheria mbalimbali.

'' Kuna mapambano kama ya akina Amir Khan, Manny Paquaio, Floyd Maywhether, David Haye, Mohamedi Ali pamoja na mtanzania Roja mtagwa anaefanya shughuli zake Marekani,

DVD hizo ni nzuri na hata walio tayari tayali katika mchezo huo wanatakiwa kujua sheria na mafunzo ya ngumi mana zinafundisha mambo mengi '' alisema Super D