Wednesday, August 24, 2011

*VODACM YATOA FURSA KWA WATANZANIA KUWAPIGIA KURA WASHIRIKI WA VODACM MISS TANZANIA

Kampuni ya mawasiliano ya Vodacom, Tanzania imetoa fursa kwa Watanzania kuweza kupiga kura na kuchagua mrembo anayevutia zaidi kati ya warembo 30 wanaoshiriki  shindano la kumsaka Vodacom Miss Tanzania 2011.

Akizungumza na waandishi wa habari, Mkuu wa Udhamini wa Vodacom ,George Rwehumbiza, alisema ili kupiga kura Watanzania watatakiwa kutuma ujumbe mfupi wa maneno wenye neno MREMBO ukifuatiwa na namba ya mshiriki 'mfano  40'  kwenda 15550 ambapo gharama kwa kila ujumbe ni shilingi 150 tu .

Aidha Rwehumbiza, aliongeza kuwa kila ujumbe mfupi utakaotumwa utampatia Mtanzania pointi 10 ambapo wateja 20 watakaobahatika kuwa na pointi nyingi zaidi kila mmoja atajipatia TIKETI mbili za VIP zitakazomwezesha kwenda kushuhudia fainali ya shindano la Vodacom Miss Tanzania 2011, itakayofanyika tarehe 10 mwezi septemba katika ukumbi wa  Mlimani city jijini Dares salaam.

Pia kwa wale watakaohitaji kutoa maoni au mitazamo yao mbalimbali kuhusu Vodacom Miss Tanzania watapata fursa ya kutuma ujumbe mfupi wa maneno wenye neno MREMBO ukifuatiwa na maoni kwenda namba 15550.

Akisisitiza hili  Rwehumbiza, alisema ili kuwafahamu warembo wanaoshindania taji la Vodacom Miss Tanzania 2011, Watanzania wote wanaweza kuangalia kituo cha Televisheni cha STAR TV leo kuanzia muda wa saa moja jioni pamoja na CLOUDS TV muda wa saa tatu usiku kila siku pia soma magazeti ya Mtanzania, The African, Dimba, Rai na Bingwa.
.

BASATA YAHIMIZA MSHIKAMANO WA WASANII

Katibu wa Shirikisho la Filamu (TAFF) Wilson Makubi akizungumza na wadau wa Jukwaa la Sanaa kuhusu uzoefu wake katika Bajeti ya Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo iliyowasilishwa hivi karibuni. Wengine kulia kwake ni Katibu wa Shirikisho la Sanaa za Maonyesho Dennis Mango na Rais wa Shirikisho la Sanaa za Ufunfi, Adrian Nyangamale

Mkongwe wa muziki wa dansi nchini Kassim Mapili akieleza jinsi viongozi wa mashirikisho ya sanaa nchini walivyopata fursa ya kuongea na Waziri Mkuu Mh. Mizengo Pinda kuhusu umuhimu wa sekta ya sanaa wakati walipomtembelea bungeni Dodoma hivi karibuni.
Wadau wa Jukwaa la Sanaa wakiwa wamesimama kumkumbuka Msanii Mahadiya Ally aliyefariki Dunia Usiku wa kuamkia Jumapili na kuzikwa Jumatatu wiki hii Mkoani Tanga.
Na Mwandishi Wetu
Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) limewataka wasanii kujenga ushirikiano kupitia vyama na mashirikisho yao ili kuhakikisha kunakuwa na mfumo rasmi na unaoeleweka wa uendeshaji wa tasnia ya sanaa nchini.
Rai hiyo imetolewa na Katibu Mtendaji wa BASATA, Ghonche Materego wakati akiliahirisha Jukwaa la Sanaa linalofanyika kila Jumatatu kwenye Ukumbi wa Baraza hilo ambapo alisema kwamba,wasanii wamekuwa walalamishi tu pasipokuchukua hatua na kuleta mabadiliko ndani ya tasnia.
“Wasanii turudi nyuma katika vyama vyetu, tujiulize kama vyama vyetu viko hai na sisi tuko ndani. Tumekuwa tukilalamika sana, malalamiko mengine ni sahihi na mengine si sahihi. Wakati umefika  wa kuleta mabadiliko” alisema Materego.
Aliongeza kwamba,uwepo wa wasanii wengi hapa nchini pasipokuwa na mfumo unaowaunganisha na kuwaweka pamoja hakutakuwa na maana yoyote hivyo kuna kila sababu ya wasanii wenyewe kuamka na kuujenga mfumo huo.
“Hebu hapa tujiulize ni wasanii wangapi wako katika vyama? Sasa ni kwa vipi sauti yako itasikika wakati hauko katika umoja? Ni lazima turudi nyuma na tujipange katika vyama vyetu na kuyapa nguvu mashirikisho. Tusizungumzie mfumo wakati sisi wenyewe tuko nje ya mfumo” alitoa rai Materego.
Alizidi kueleza kwamba, BASATA katika mwaka huu wa fedha imejipanga kuendesha chaguzi za mashirikisho yote ya sanaa nchini na kuwataka wasanii kujipanga katika vyama vyao na kuhakikisha vinakuwa hai kwa ajili ya kujenga mfumo utakaoleta mageuzi ya maendeleo katika tasnia hii.
Aidha,alisikitishwa na tabia ya wasanii kutokuwa katika vyama na badala yake kukaa pembeni na kutupa lawama au kukosoa mwenendo wa tasnia pasipokuzingatia kwamba wao wanapaswa kuwa sehemu ya mabadiliko na kupaza sauti zao wakiwa ndani ya mfumo.
“Tuanze kujiuliza sauti zetu zinasikika katika vyama vyetu? Kama hauko katika chama wewe ndiye unayekwamisha ujenzi wa mfumo. Wakati umefika tusiwe watu wa kulalamika bali kuleta mabadiliko ya kweli tukiwa katika umoja wetu” alihitimisha Materego.
Awali katika program ya wiki hii,Viongozi wa mashirikisho ya wasanii nchini walipata fursa ya kuwasilisha uzoefu wao kuhusu bajeti ya Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo iliyosomwa bungeni hivi karibuni.

Monday, August 22, 2011

ULEVI KUPINDUKIA WASABABISHA AJALI ENEO LA MAMA JOHN MBEYA

Askari wa usalama barabarani mkoani Mbeya akitoa kibao cha namba ya gari lililopata ajali maeneo ya Mama John jijini mbeya, ajali hiyo imetokea jana usiku baada ya dereva wa gari hilo aina ya Toyota Corola kuzidiwa kilevi na kukosa mwelekeo na kutumbukia katika dalaja.
Huwezi amini hii gari imeingiaje hapa kwakweli madereva kuweni makini barabarani pombe ni hatari ukiona umelewa acha kuendesha gari
Baadhi ya wananchi wakiangalia gari iliyotumbukia darajani Mama John jijini Mbeya

Sunday, August 21, 2011

UTAWALA WA GADDAFI UMEANGUKA!


Kila chenye mwanzo kina mwisho. Blogu hii iliandika siku chache zilizopita juu ya kuwepo kwa taarifa za Ki-Intelijensia zilizotabainisha kuwa utawala wa Gaddafi ungeanguka ndani ya siku chache. Na imekuwa hivyo.

Usiku wa kuamkia leo wapiganaji waliokuwa wakipambana na vikosi vya Gadaffi hatimaye wameitwaa Tripoli.  Walibya kwa mamia  waaripotiwa kuingia mitaani kusheherekea ukombozi kutoka kwa utawala wa kidikteta na kikandamizaji. Watu wameonekana wakichoma moto picha za Gaddafi.

Inasemekana wana wa Gaddafi akiwamo Seif Islam ambaye alitarajiwa angemrithi baba yake wako sasa wamekamatwa na wapiganaji hao. Gaddafi mwenyewe hajulikani alipo. Uwanja wa ndege wa Libya kuna ndege mbili ambazo zinadhaniwa Gaddafi angezitumia kuondoka nchini akiwa na familia yake. Gaddafi angekimbilia wapi? Nchi za Zimbabwe na Angola zinatajwa kuwa zingeweza kuwa kimbilio la Gaddafi. Taarifa zaidi zitawajia kadri zitakavyopatikana.

MSONDO YATOA TUZO ya the Best Rhumba Group katika East Africa Music



BENDI ya mziki ya msondo ngoma imepata TUZO ya the Best Rhumba Group katika East Africa Music Awards mashindano yariyofanyika Nairobi Kenya na kukusanyika kwa bendi za Afrika Mashariki na bendi ya msondo kuibuka Kidedea katika mashindano hayo akisibitisha ushindi uho meneja wa bendi Saidi KIbiriti alipokuwa akiongea na Msemaji wa Bendi hiyo, Rajabu Mhamila , Super D

Alisema wameshinda tuzo hiyo na watahakikisha wanaionesha kwa mashabiki wa bendi hiyo ili kudhirisha kuwa bendi ipo ng'ang'ari popote duniani mana bendi imekamilika kila idara alisema Super D (pichani)

Bendi hiyo itanza mazoezi siku ya jumatatu kwa ajili ya kujiandaa na sikukuu ya Iddi inayotarajia kufanyika wiki ijayo ambapo wanaingia kambini kusuka vibao vipya ikiwemo na kuvifanyia kazi vile vya Zamani

Super D alisema bendi hiyo siku ya Iddi Mosi itapiga katika viwanja vya TTC Chang'ombe ambapo mashabiki watapata kuona tuzo hiyo ya Afrika Mashariki walioitwaa hivi karibuni na kupata fulsa ya kupiga nayo picha katika viwanja hivyo

Bendi hiyo inayotamba na vibao vyake vipya vya Suluu uliotungwa na Shabani Dede na Nadhili ya Mapenzi uliotungwa na Juma Katundu




Rajabu Mhamila 'Super D'
Photojournalist at Majira, Business Times
Email.superdboxingcoach@gmail.com
www.burudan.blogspot.com
Mob;+255787 406930
+255774406938
Po.Box. 15493
Dar es Salaam Tanzania

Friday, August 19, 2011


AY FT LAMYIA & ROMEO - SPEAK WITH YA BODY VIDEO

SPEAK WITH YA BODY
May be he should be Named "Ruler and Conquerer"...well he ruled Bongo for a long time and ended up conquering it. Any Objection?Naah, ofcoz there isn't any otherwise what would our boy be doing in the U.S and not even visiting, Woooorkiing!!! This is an International hit from ours truly, A.y featuring Lamyia and Romeo. Lamyia from Checkmate and Romeo from No Limit Record Label in the United States. For some Unusual Reasons No Limit got hold of AY Cd and liked the Vibe and decide to invite him in North America for couple of records with legend baby superstar Romeo formerly known as LIL ROMEO. The beat was sick already and what A.y and the rest did is taking the music to the I.C.U. We All have to admit this track makes u wanna press play again, n again n again.

Check out new video by AY on 
http://ay.co.tz/  or http://youtu.be/eH4-qHrb4Ms
CREDITS:

Song: SPEAK WIT YA’ BODY
Artist: AY FEAT. ROMEO AND LAMYIA
Written By: Ambwene Yesayah, Lamyia and Romeo
Ay Vocals Recorded By: Pancho Latino At B’Hits Studio 2,Dar Es Salaam.
Produced By:RILEY FROM CHECKMATE
Mixed and Mastered By: RILEY FROM CHECKMATE

MANAGER- HEMDEE
VIDEO BY OUTLIERS
DIRECTORS-WILLIAM TIKKI & SHAI
 
Hope Ya’ll going to have fun.
Life’s Too Short…Make The most of it.
Kuna Taarifa Za Ki-Intelijensia; Gaddafi Kuikimbia Libya Siku Chache Zijazo

| Friday, August 19, 2011

Kwa mujibu wa taarifa za Kiintelijensia zilizoripotiwa na Televisheni  ya NBC ya Marekani. Kanali Muammar
Gaddafi anapanga kuikimbia Tripoli akiwa na familia yake. Huenda akakimbilia Tunisia. Hii inatokana na matukio ya hivi karibuni kwenye medani ya kijeshi ambapo Gaddafi ameupoteza mji muhimu ki mkakati . Ni mji wa Zawiyah unaonekana pichani chini ambao sasa unapepea bendera ya Libya ya kabla ya ujio wa Gaddafi. Kutoka Zawiyah, vikosi vinavyopambana na Gaddafi sasa vimebaki na Tripoli kama target. Kuanguka kwa Zawiyah kutoka mikononi mwa Gaddafi kunaweza kuchochea  maasi  zaidi ndani ya jeshi la Gaddafi na hata kuwatia moyo Walibya walioko Tripoli kuamka na kumpinga Gaddafi wazi wazi. Na tusubiri tuone.