Mafanikio yanahitaji uvumilivu Mdau wa jirushe ni mwandishi wa habari kutoka New Habari Anapatikana kwa namba 0716 772231 ,Email -humphreyshao@ymail.com/shaohumphrey58@gmail.com kwa mahitaji yoyote ya kuhabarisha ,makala,matukio, picha za harusi na kuandaa event mbalimbali nitwangie
Sunday, May 6, 2012
HILDA NDIYE RED'S MISS USTAWI 2012
MUIGIZAJI MKONGWE KWENYE TASNIA YA BONGO MUVI ,SINTA A.K.A J LO WA BONGO AKIWA NA WANAKAMATI KUJADILI MSTAKABALI WA SHUGHULI WAKATI REASOL
WATU KADHAA AMBAO NI WANAFUNZI WA CHUO CHA USTAWI WAKILA BATA KUSUBILI MCHAKATO WA SHINDANO LA RED'S MISS USTAWI
DULLY SYKES BABA TORIANO AKITOA SHOO WAKATI WA SHINDANO
MAJAJI WA SIKU HIYO WANA HABARI ALFRED LUCAS ,VICKY KIMARO NA JAMES RANGE WAKICHAKALIKA KUJUMLISHA MATOKEO
MKURUGENZI WA JIRUSHEWEEKEND BLOG HUMPHREY SHAO AMABAYE AMEVAA SHATI LA BLUU AKIWA NA WADAU WENGINE KUTOKA USTAWI WAKIFATILIA SHOO KWA UMAKINI MKUBWA.
WATU KADHAA AMBAO NI WANAFUNZI WA CHUO CHA USTAWI WAKILA BATA KUSUBILI MCHAKATO WA SHINDANO LA RED'S MISS USTAWI
DULLY SYKES BABA TORIANO AKITOA SHOO WAKATI WA SHINDANO
MAJAJI WA SIKU HIYO WANA HABARI ALFRED LUCAS ,VICKY KIMARO NA JAMES RANGE WAKICHAKALIKA KUJUMLISHA MATOKEO
MKURUGENZI WA JIRUSHEWEEKEND BLOG HUMPHREY SHAO AMABAYE AMEVAA SHATI LA BLUU AKIWA NA WADAU WENGINE KUTOKA USTAWI WAKIFATILIA SHOO KWA UMAKINI MKUBWA.
Thursday, May 3, 2012
GRAND MALT YAZINDUA TUZO ZA “EXCEL WITH GRAND MALT 2012”.
Kinywaji
maarufu cha Grand Malt leo kimezindua tuzo kwa wanafunzi wa elimu ya
juu zijulikanazo kama “Excel with Grand Malt”, huu ukiwa ni mwaka wa
pili kwa tuzo hizi kutolewa.
Akizungumzia
tuzo hizo, meneja wa kinywaji cha Grand Malt Bi. Consolata Adam
alisema; Excel with Grand Malt ni tuzo za aina yake ambazo zimelenga
kutambua na kuthamini mchango wanaoonesha wanafunzi katika fani
mbalimbali nje ya masomo ya darasani. Tunatambua kuwa kazi kubwa ya
mwanafunzi anapokuwa chuoni ni kuhudhuria vipindi vya darasani na kupata
elimu, bali tunapenda pia kuwatambua wale wachache ambao wanakwenda
mbali zaidi na kufanya mambo ya maendeleo katika mazingira yao ya chuo.
Tuzo
hizi zilianzishwa mwaka jana ambapo tuliweza kufika katika mikoa sita
na kufikia vyuo vipatavyo ishirini. Kwa mwaka huu mchakato utaanza mwezi
Aprili hadi June, na Mikoa itakayohusika ni pamoja na Dar es salaam,
Morogoro, Iringa, Dodoma, Kilimanjaro na Mwanza ambapo vyuo vipatavyo 21
vitashiriki. Kama ilivyokuwa mwaka jana, fani zitakazoshindanishwa ni
Ubunifu (Innovation), Michezo (sports), Utamaduni na burudani (Culture
& Entertainment) na Mazingira na Huduma za jamii (Environment &
social responsibilities). Kama ilivyo ada, washindi katika fani hizi
watajipatia zawadi mbalimbali toka Grand Malt ikiwa ni pamoja na pesa za
kununulia vitabu na vyeti vya ushindi.
Kwa
sasa natangaza rasmi kuwa tunzo hizi zimezinduliwa rasmi na mkoa wa
kwanza utakuwa ni Morogoro ambapo tunatarajia kufanya tamasha kubwa
kwenye viwanja vya chuo kikuu cha SUA siku ya jumamosi kisha jumapili
tutafanya tamasha la ufunguzi kwenye Viwanja vya chuo cha CBE mkoani
Dodoma na kutakuwa na burudani zitakazoongozwa na nguli wa Hip hop
nchini Joh Makini ,zawadi nyingi na zaidi kutakuwa na GrandMalt baridi
na hakutakuwa na kiingilio chochote. Alisema Bi. Consolata.
Akielezea
umuhimu wa Tuzo hizo, meneja masoko wa TBL Bw. Fimbo Butallah alisema;
Tunafurahi sana kuona vyuo vyote vilipokea tuzo hizi kwa furaha kubwa,
hii ni kwa sababu wanatambua umuhimu wake. Kupitia tuzo hizi ambazo
zitakuwa zikitolewa kila mwaka, Grand Malt inatoa changamoto kwa vijana
walio vyuoni kuona umuhimu wa kujituma na kufanya mambo mengi na makubwa
zaidi ya kufaulu mitihani ya darasani tu. Tunaomba viongozi wa serikali
za wanafunzi na viongozi wa vyuo kuendelea kutoa ushirikiano kama
walivyofanya mwaka jana ili kuleta ufanisi zaidi katika tuzo za mwaka
huu. Kama ilivyo kawaida, utaratibu utakuwa ule ule ambapo wanchuo
watapendekeza majina ya vijana wanaoamini kuwa wamefanya mambo makubwa
ndani ya vyuo vyao katika tasnia zilizotajwa hapo awali, kisha kufuatiwa
na kipindi cha kupiga kura ambapo washindi watapatikana. Alimaliza Bw.
Butallah
Kwa
upande wake meneja mahusiano na mawasiliano wa Tbl Bi Edith Mushi
Alisema GrandMalt kwa kuzingatia umuhimu wa juhudi za serikali katika
kuhamasisha jamii kutunza mazingira kwa kupanda miti mwaka huu Grand
Malt itafanya zoezi maalum kwenye kila chuo kwa kupanda miti imara
itakayosaidia kutunza na kuboresha mazingira ya vyuo hivyo ili kuandaa
mazingira bora ya kusomea ya wanafunzi wa sasa na wa vizazi vijavyo
ambapo mkoani Dodoma zoezi hilo litafanyika jumatatu May 07,2012 katika
vyuo vya UDOM na CBE tawi la Dodoma na Mkoani Morogoro zoezi hilo
litafanyika kwenye vyuo vya SUA na Mzumbe siku ya jumanne May 08,2012
asubuhi, kisho zoezi hilo litaendelea katika mikoa ya
Iringa,kilimanjaro,Mwanza na Dar Es Salaam.
Wednesday, May 2, 2012
Eleven killed in Egypt clashes over army rule
CAIRO (Reuters) - Eleven people were killed and more than 160 wounded near Egypt's Defence Ministry on Wednesday after armed men assaulted protesters demanding an end to army rule, prompting two Islamist candidates to suspend their presidential election campaigns.
Unidentified "thugs" armed with guns or batons attacked demonstrators who included hundreds of ultraconservative Salafi Islamists protesting at the exclusion of their candidate from this month's vote, state news agency MENA reported.
The violence casts a deep shadow over the presidential election due on May 23 and 24, with a run-off in June, and highlights the fragility of Egypt's transition to democracy, which has been punctuated by violence and political bickering.
Security and medical sources gave a toll of 11 dead and over 160 wounded in the clashes outside the Defence Ministry in central Cairo's Abbasiya district. The fighting raged on unabated through the morning, but subsided in the afternoon.
"Where is the army? Why are they not stopping these people?" cried a bystander as the violence persisted. Shots rang out as young men dashed back and forth across debris-scattered streets, hurling rocks, glass and petrol bombs.
"Down, down with military rule," yelled protesters.
Wounded men were hauled away as others filled bottles with petrol while shots rang out. A Reuters witness saw some combatants carrying guns and one with a sword.
The army sent in extra vehicles and troops, but pledged in a statement not to disperse peaceful demonstrators. Continued...
SERIKALI YATAKIWA KUACHA KUINGILIAKAZI ZA TUME YA KATIBA
SERIKALI imetakiwa kuacha kuiingilia kazi za Tume ya
Mabadiliko ya Katiba na badala yake iwape uhuru wa kufanyakazi hiyo kwa ufasaha
na kuandaa katiba wanayoitaka wananchi.
Hayo yamesemwa jana na Mwenyekiti wa Tume hiyo, Jaji Joseph
Sinde Warioba wakati wa uzinduzi wa tume hiyo na kukabidhiwa jengo la kufanyia
kazi hiyo.
Mwenyekiti huyo amesema isije ikafika wakati tume ikashindwa
kufanyakazi ipasavyo kwa sababu ya maslahi ya watu wachache kwani kufanya hivyo
itakuwa ni kuingilia uhuru wa tume na kuwanyima haki wananchi ya kupendekeza
katiba waipendayo.
“ Nyie mliotuchagua tunaomba tafadhari mtupe nafasi isije
ikaja leo au kesho mnaanza kutusumbua tupindishe kilichopo kwa madai mna watu
wenu ndani ya tume naomba ieleweke kuwa tume si ya kikundi fulani ni ya
wananchi hivyo hatutaki kufanyakazi kwa
presha ya watu fulani,”amesema Warioba.
Amesema kazi waliyopewa ni ngumu hivyo wana imani serikali
itawapa ushirikiano wa kuwafikia wananchi wote ili waweze kutoa maamuzi yao na kuandaa katiba
yenye maslahi ya umma.
Kwa upande wake Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue
amesema Serikali imeandaa mazingira safi
ya kuhakikisha tume hiyo inafanyakazi kwa ufanisi zaidi.
Amesema kuwa serikali
imetekeleza ahadi aliyoitoa rais alipoiapisha tume hiyo Aprili 13 mwaka huu ya
kuhakikisha tume hiyo inafanyakazi kwenye mazingira stahiki yenye ulinzi wa
kutosha, usalama , na vifaa vya mawasiliano na vya kutunzia kumbukumbu vya
kisasa.
Pia serikali imenunua magari 30, kwa ajili ya tume hiyo ili
kuweza kuwafikia wananchi kwa urahisi na kuepuka vikwazo katika utendaji wa
kazi hiyo na fungu maalum la fedha limetengwa..
“ Serikali imedhamiria kuipa uhuru tume, kuwapa sehemu nzuri
ya kufanyiakazi pamoja na nyumba za kuishi wana tume ambao wanatoka nje ya Dar
es Salaam,”amesema Sefue.
Naye Waziri wa Katiba na Sheria, Cellina Kombani amesema umuhimu wa mabadiliko ya katiba ya
nchi ni mkubwa na wananchi wana matumaini na tume na ndiyo maana ilipotangazwa
hakuna malalamiko yaliyojitokeza.
Ameitaka tume hiyo ijipange vyema ili kuhakikisha inatoa
elimu ya katiba iliyopo ili wananchi waweze kutoa maoni ya katiba waipendayo
kwani muundo wa katiba hiyo ni jambo nyeti na lenye kuleta msisimuko.
“ Nina imani amani itatawala
na uwazi, kwani mchakato huu ni wa kuboreha mazuri, kuondoa mapungufu pia ni
kujipima tulikotoka na tuendako kwani nia si kuvunja umoja wetu bali mawazo ya
wananchi yataheshimiwa, “amesema Kombani.
Kombani ameongeza kuwa tume hiyo ndiyo nguzo ya mchakato wa
katiba mpya huku akisisitiza kufanikiwa au kutofanikiwa kutatokana na tume hiyo
kutekeleza majukumu yao
kwa kuwashirikisha wananchi bila ubaguzi.
“ Kazi hii inahitaji ushirikiano zaidi nafahamu kuna kipindi
mtakwazika na kutamani kuimbia kazi hii lakini mkiwashirikisha wananchi
mtafikia muafaka na hatimaye tutapata katiba inayostahili,”amesema Kombani.
Wakati huohuo, Waziri wa Katiba na Sheria Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar,
Abubakari Khamis Bakari amesema tume imepewa kazi ngumu ya kuwaelimisha
wananchi kwani wengi wao hawajui maana ya muungano.
Amesema ili katiba iwe yenye kukidhi haja ni muhimu wananchi
wakapewa fursa ya kutoa maoni ambayo yataisaidia tume hiyo kurahisisha kazi yao.
Amewatahadharisha wananchi kuacha kutumia mchakato huo kama njia ya kuibomoa nchi na badala yake fursa hiyo itumike kuunda
katiba yenye mantiki na inayokubaliwa na watu wote.
Hata hivyo hafla hiyo iliingiliwa na dosari baada ya
jenereta lililopo jirani na jengo hilo kulipuka
jana asubuhi na kusababisha umeme katika jengo hilo kukatika
hivyo kufanya hafla hiyo kuendeshwa bila vipaza sauti.
mwisho







|
V/S
|




|
MAPAMBANO YOTE NI KAMA IFUATAVYO;-
RAMADHAN KUMBELE(DAVIS CORNER-TANDIKA) v/s JAMES MOKIWA(CHICHI MAWE GYM
KARIM SALUM”paquiao” v/s ANORD YOHANA”biggie’(CHICHI MAWE GYM)
DOI MIYEYUSHO(CHICHI MAWE GYM) v/s JUMANNE MTENGELA (MABIBO GYM)
JAFAR MAJIA”mr nice” v/s DAUD MUHUNZI (MSISIRI GYM)
DOTO KIPACHA V/S JOSEPH RICHARD
FRANCIS SUBA v/s JOSEPH PITER”mbowe’-(MKONO WA CHUMA)
SADAT MIYEYUSHO(CHICHI MAWE GYM) v/s SWEDI HASSAN(dame gym-nomo camp)
MARTIN RICHARD(BigRight Boxing) v/s YOHANA THOBIAS(CHICHI MAWE GYM
|





|
V/S
|
|
V/S
|
|
V/S
|
Subscribe to:
Posts (Atom)